Rais Samia katika Uzinduzi Zanzibar akosoa kuchukua waliofeli kuwa walimu asema ndio wanadumisha elimu nchini

Rais Samia katika Uzinduzi Zanzibar akosoa kuchukua waliofeli kuwa walimu asema ndio wanadumisha elimu nchini

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais Samia Suluhu Hassan akishiriki Uzinduzi wa Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation - Zanzibar

Rais ahuzunika kwa kufeli sana kwa mkoa anaotokea, Kusini Unguja.

Rais Samia azungumzia ubovu wa matokeo Zanzibar ambapo alitoa maelekezo na sasa ufaulu kwa wanafunzi umeongezeka. Amezungumzia kufeli kwa wanafunzi Zanzibar na amepongeza juhudi za asasi za kiraia na serikali katika kuongeza ufaulu akitolea mfano wa matokeo ya 2020.

Rais amesema ni aibu kwa mkoa ambao anatoka Rais wa JMT(Kusini Unguja) kuwa na ufaulu duni ukilinganisha na mikoa mingine.

Rais ametoa wito wa kuwa na performance appraisal na vipimo tofauti na sasa ambapo walimu wamepewa ajira za maisha hivyo hubweteka na kusababisha elimu kuwa duni kwa kuwa hawajitumi kazini.

Rais amekosoa suala la kuchukua wanafunzi waliofanya vibaya darasani, badala yake walimu wazuri wawe ni wale ambao wamefaulu vizuri ili kuboresha elimu nchini.

Bila kulea watoto vizuri tutazalisha Panya Road

Rais atoa wito kwa wazazi kuhusu mkakati wa kutokomeza zero Zanzibar kwa kuwataka wazazi washiriki kutambua maendeleo ya elimu ya watoto wao, badala ya kuwaachia walimu peke yao.

Ili mwanafunzi aweze kufaulu inategemea pande tatu, wazazi, walimu na serikali. Rais amesema. Amesisitiza watu wote tushiriki kulea ili tung'ae bila kulea vizuri tutazalisha panya road wa kike na wa kiume.
FVmFdyhWUAAhQgF.jpg

 
Rais Samia Suluhu Hassan akishiriki Uzinduzi wa Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation - Zanzibar

Rais ahuzunika kwa kufeli sana kwa mkoa anaotokea, Kusini Unguja.

Rais Samia azungumzia ubovu wa matokeo Zanzibar ambapo alitoa maelekezo na sasa ufaulu kwa wanafunzi umeongezeka. Amezungumzia kufeli kwa wanafunzi Zanzibar na amepongeza juhudi za asasi za kiraia na serikali katika kuongeza ufaulu akitolea mfano wa matokeo ya 2020.

Rais amesema ni aibu kwa mkoa ambao anatoka Rais wa JMT(Kusini Unguja) kuwa na ufaulu duni ukilindanisha na mikoa mingine.

Rais ametoa wito wa kuwa na performance appraisal na vipimo tofauti na sasa ambapo walimu wamepewa ajira za maisha hivyo hubweteka na kusababisha elimu kuwa duni kwa kuwa hawajitumi kazini.

Rais amekosoa suala la kuchukua wanafunzi waliofanya vibaya darasani, badala yake walimu wazuri wawe ni wale ambao wamefaulu vizuri ili kuboresha elimu nchini.

Bila kulea watoto vizuri tutazalisha Panya Road

Rais atoa wito kwa wazazi kuhusu mkakati wa kutokomeza zero Zanzibar kwa kuwataka wazazi washiriki kutambua maendeleo ya elimu ya watoto wao, badala ya kuwaachia walimu peke yao.

Ili mwanafunzi aweze kufaulu inategemea pande tatu, wazazi, walimu na serikali. Rais amesema. Amesisitiza watu wote tushiriki kulea ili tung'ae bila kulea vizuri tutazalisha panya road wa kike na wa kiume.
Baada ya Walimu aje na Polisi , maana nako wanachukua waliofeli
 
Tutegemee kuona ufaulu ukipanda hata kuongoza kitaifa kwa shule za kusini unguja kama ilikuwa kwa chato

Sasa hapa umezungumza nini?
Hoja ni ipi hapa? Hili swala la kuchukua waliofeli na kuwafanya walimu lianza kukemewa na mwendazake na akatukanwa sana na Sasa Samia!
Lakini sasa hivi kuna mabadiliko maana ni kweli division 4 hapati chuo cha ualimu serikali!

Ukweli ni kwamba mwanafunzi anapofeli hatuwezi kuacha kimtazama mwalimu kama kweli hachangii na hata mwanafunzi akifaulu mwalimu husifiwa pia!

Ukweli ni kwamba huchukuaji wa Walimu vilaxa waliofeli ndio wawe walimu kunachangia sana wanafunzi kufeli ukiacha sababu nyingine!

Rais kaongea ukweli japo wengi watapinga!
 
Sasa hapa umezungumza nini?
Hoja ni ipi hapa? Hili swala la kuchukua waliofeli na kuwafanya walimu lianza kukemewa na mwendazake na akatukanwa sana na Sasa Samia!
Lakini sasa hivi kuna mabadiliko maana ni kweli division 4 hapati chuo cha ualimu serikali!

Ukweli ni kwamba mwanafunzi anapofeli hatuwezi kuacha kimtazama mwalimu kama kweli hachangii na hata mwanafunzi akifaulu mwalimu husifiwa pia!

Ukweli ni kwamba huchukuaji wa Walimu vilaxa waliofeli ndio wawe walimu kunachangia sana wanafunzi kufeli ukiacha sababu nyingine!

Rais kaongea ukweli japo wengi watapinga!
Soma habari nzima,kuna mahali amesema ni aibu jimbo la Rais kufeli
 
Walimu wenye three na four wameghushi utumishi, wafukuzwe tuajiri degree za first class kuanzia msingi
 
Hakuna Mwalimu aliyefeli halafu anafundisha ngazi aliyo feli.

Mtu akipata ufaulu hafifu form 4 HAFUNDISHI form 4,.anakuwa trained na kurudi kufundisha LA SABA ambako ALIFAULU.

Hivyo, hivyo kwa FORM 6 wanafundishwa kuja kufundisha O-level ambako walifaulu.

Ni Nani anafundisha ngazi aliyo feli?
 
Rais Samia Suluhu Hassan akishiriki Uzinduzi wa Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation - Zanzibar

Rais ahuzunika kwa kufeli sana kwa mkoa anaotokea, Kusini Unguja.

Rais Samia azungumzia ubovu wa matokeo Zanzibar ambapo alitoa maelekezo na sasa ufaulu kwa wanafunzi umeongezeka. Amezungumzia kufeli kwa wanafunzi Zanzibar na amepongeza juhudi za asasi za kiraia na serikali katika kuongeza ufaulu akitolea mfano wa matokeo ya 2020.

Rais amesema ni aibu kwa mkoa ambao anatoka Rais wa JMT(Kusini Unguja) kuwa na ufaulu duni ukilindanisha na mikoa mingine.

Rais ametoa wito wa kuwa na performance appraisal na vipimo tofauti na sasa ambapo walimu wamepewa ajira za maisha hivyo hubweteka na kusababisha elimu kuwa duni kwa kuwa hawajitumi kazini.

Rais amekosoa suala la kuchukua wanafunzi waliofanya vibaya darasani, badala yake walimu wazuri wawe ni wale ambao wamefaulu vizuri ili kuboresha elimu nchini.

Bila kulea watoto vizuri tutazalisha Panya Road

Rais atoa wito kwa wazazi kuhusu mkakati wa kutokomeza zero Zanzibar kwa kuwataka wazazi washiriki kutambua maendeleo ya elimu ya watoto wao, badala ya kuwaachia walimu peke yao.

Ili mwanafunzi aweze kufaulu inategemea pande tatu, wazazi, walimu na serikali. Rais amesema. Amesisitiza watu wote tushiriki kulea ili tung'ae bila kulea vizuri tutazalisha panya road wa kike na wa kiume.

Na ndiko tunaelekea,waajiriwe wenye ufaulu wa juu darasani na waajiriwe kwa mikataba ambayo ni renewable kila baada ya miaka 3.
 
Back
Top Bottom