Rais Samia katika Uzinduzi Zanzibar akosoa kuchukua waliofeli kuwa walimu asema ndio wanadumisha elimu nchini

Rais Samia katika Uzinduzi Zanzibar akosoa kuchukua waliofeli kuwa walimu asema ndio wanadumisha elimu nchini

Rais Samia Suluhu Hassan akishiriki Uzinduzi wa Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation - Zanzibar

Rais ahuzunika kwa kufeli sana kwa mkoa anaotokea, Kusini Unguja.

Rais Samia azungumzia ubovu wa matokeo Zanzibar ambapo alitoa maelekezo na sasa ufaulu kwa wanafunzi umeongezeka. Amezungumzia kufeli kwa wanafunzi Zanzibar na amepongeza juhudi za asasi za kiraia na serikali katika kuongeza ufaulu akitolea mfano wa matokeo ya 2020.

Rais amesema ni aibu kwa mkoa ambao anatoka Rais wa JMT(Kusini Unguja) kuwa na ufaulu duni ukilindanisha na mikoa mingine.

Rais ametoa wito wa kuwa na performance appraisal na vipimo tofauti na sasa ambapo walimu wamepewa ajira za maisha hivyo hubweteka na kusababisha elimu kuwa duni kwa kuwa hawajitumi kazini.

Rais amekosoa suala la kuchukua wanafunzi waliofanya vibaya darasani, badala yake walimu wazuri wawe ni wale ambao wamefaulu vizuri ili kuboresha elimu nchini.

Bila kulea watoto vizuri tutazalisha Panya Road

Rais atoa wito kwa wazazi kuhusu mkakati wa kutokomeza zero Zanzibar kwa kuwataka wazazi washiriki kutambua maendeleo ya elimu ya watoto wao, badala ya kuwaachia walimu peke yao.

Ili mwanafunzi aweze kufaulu inategemea pande tatu, wazazi, walimu na serikali. Rais amesema. Amesisitiza watu wote tushiriki kulea ili tung'ae bila kulea vizuri tutazalisha panya road wa kike na wa kiume.
Mnawalipa mshahara wa Mama Ntilie halafu mnataka waliofaulu?
 

Rais Samia anafanana na Vasco dagama.​


Vasco Dagama unamfahua au unasoma tu kwenye historia. Kwa kuingia kwa rais Samia mm mwenyewe nimepiga hatua 20 mail. Ukilinganisha na Magufuli. Kwanza mkopo wangu wa Chuo Kikuu umeisha mapema. Namshukuru Mungu sana kwa Rais Samia kuwa Rais.
 
Nipo kusini mwa Tanzania huku kwakweli wananchi hawaridhishwi na awamu hii ya sita.
 
Sasa hapa umezungumza nini?
Hoja ni ipi hapa? Hili swala la kuchukua waliofeli na kuwafanya walimu lianza kukemewa na mwendazake na akatukanwa sana na Sasa Samia!
Lakini sasa hivi kuna mabadiliko maana ni kweli division 4 hapati chuo cha ualimu serikali!

Ukweli ni kwamba mwanafunzi anapofeli hatuwezi kuacha kimtazama mwalimu kama kweli hachangii na hata mwanafunzi akifaulu mwalimu husifiwa pia!

Ukweli ni kwamba huchukuaji wa Walimu vilaxa waliofeli ndio wawe walimu kunachangia sana wanafunzi kufeli ukiacha sababu nyingine!

Rais kaongea ukweli japo wengi watapinga!
Walimu wa St Francis, Feza, Canossa, Marian wote wana division I point 3 ?
 
Sasa hapa umezungumza nini?
Hoja ni ipi hapa? Hili swala la kuchukua waliofeli na kuwafanya walimu lianza kukemewa na mwendazake na akatukanwa sana na Sasa Samia!
Lakini sasa hivi kuna mabadiliko maana ni kweli division 4 hapati chuo cha ualimu serikali!

Ukweli ni kwamba mwanafunzi anapofeli hatuwezi kuacha kimtazama mwalimu kama kweli hachangii na hata mwanafunzi akifaulu mwalimu husifiwa pia!

Ukweli ni kwamba huchukuaji wa Walimu vilaxa waliofeli ndio wawe walimu kunachangia sana wanafunzi kufeli ukiacha sababu nyingine!

Rais kaongea ukweli japo wengi watapinga!
Kada ipi ichukue waliofeli?
 
Yaani nipate div one pcm au cbg then nikawe mwalimu serious kwa mshahara upi wkt engineer wa tanrod anakula milioon 6 kwa mwezi hapa

Itabakia hvyo hvyo kuwa waliofelinndio wawe waaLimu wetu na pia waanzishe performance appraisal kwa walimu wasiopaerfomu vzr
 
Nipo kusini mwa Tanzania huku kwakweli wananchi hawaridhishwi na awamu hii ya sita.
Hawana elimu huko ata huku kanda ya ziwa raia wanasema amesanabisha vitu kupanda bei yaan nawaangalia nabaki kuwaacha na ujinga wao
 
[emoji625]GOLDEN TULIP, Zanzibar. Juni 19, 2022.

RAIS SAMIA AZINDUA TAASISI YA MWANAMKE INITIATIVE FOUNDATION

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea Tuzo yenye saini 50 za Wanafunzi Wanawake waliofaidika na Taasisi ya Mwanamke Initiatives Foundation (MIF) katika hafla iliyofanyika kwenye hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar tarehe 19 Juni, 2022.

#KaziIendelee
#AlipoMamaVijanaTupo
#JiandaeKuhesabiwa2022
IMG-20220619-WA0282.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan akishiriki Uzinduzi wa Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation - Zanzibar

Rais ahuzunika kwa kufeli sana kwa mkoa anaotokea, Kusini Unguja.

Rais Samia azungumzia ubovu wa matokeo Zanzibar ambapo alitoa maelekezo na sasa ufaulu kwa wanafunzi umeongezeka. Amezungumzia kufeli kwa wanafunzi Zanzibar na amepongeza juhudi za asasi za kiraia na serikali katika kuongeza ufaulu akitolea mfano wa matokeo ya 2020.

Rais amesema ni aibu kwa mkoa ambao anatoka Rais wa JMT(Kusini Unguja) kuwa na ufaulu duni ukilinganisha na mikoa mingine.

Rais ametoa wito wa kuwa na performance appraisal na vipimo tofauti na sasa ambapo walimu wamepewa ajira za maisha hivyo hubweteka na kusababisha elimu kuwa duni kwa kuwa hawajitumi kazini.

Rais amekosoa suala la kuchukua wanafunzi waliofanya vibaya darasani, badala yake walimu wazuri wawe ni wale ambao wamefaulu vizuri ili kuboresha elimu nchini.

Bila kulea watoto vizuri tutazalisha Panya Road

Rais atoa wito kwa wazazi kuhusu mkakati wa kutokomeza zero Zanzibar kwa kuwataka wazazi washiriki kutambua maendeleo ya elimu ya watoto wao, badala ya kuwaachia walimu peke yao.

Ili mwanafunzi aweze kufaulu inategemea pande tatu, wazazi, walimu na serikali. Rais amesema. Amesisitiza watu wote tushiriki kulea ili tung'ae bila kulea vizuri tutazalisha panya road wa kike na wa kiume.

Kwa hiyo Rais, ameona sababu ni kuajiriwa tu kwa walimu waliofeli! Na anaposema walimu waliofeli, anafahamu anacho kizungumza? Maana NECTA inamtambua mtahiniwa aliyepata daraja 0 pekee au yule aliyepata F kwenye somo; ndiye aliyefeli!
Kuanzia daraja la 1-IV, hawa wote ni watahiniwa walio faulu! Sasa atuambie kama kina mwalimu aliye ajiriwa huku akiwa amepata division 0!!

Siku nyingine aseme labda 'walimu wenye ufaulu hafifu'!!! Na siyo walimu waliofeli.

By the way, anatambua pia changamoto nyingine zinazo wakabili walimu wake wa huko Zanzibar? Au ameamua tu na yeye kuongea ili aonekane? Mfano mazingira duni ya kufanyia kazi, mishahara midogo na isiyokidhi mahitaji, kutokupandishwa madaraja kwa wakati, jamii kutokuwa na muamko wa kusoma; na hasa elimu dunia! nk!
 
Walimu wenye three na four wameghushi utumishi, wafukuzwe tuajiri degree za first class kuanzia msingi
Mna hela za kuwalipa hao walimu mishahara inayo endana na elimu yao? Au na wewe una akili kama za Rais wako? Unataka ng'ombe atoe maziwa, huku ukiwa humpi chakula kinacho stahili?
 
Yaani nipate div one pcm au cbg then nikawe mwalimu serious kwa mshahara upi wkt engineer wa tanrod anakula milioon 6 kwa mwezi hapa

Itabakia hvyo hvyo kuwa waliofelinndio wawe waaLimu wetu na pia waanzishe performance appraisal kwa walimu wasiopaerfomu vzr
mshahara wa wapi huo.kwani tannroad wana special scheme au.ninachojua ni kwamba tanroad wanapokea sana rushwa kutoka kwa wakandarasi lkn si kuwa na mishahara minono.
 
Yaani nipate div one pcm au cbg then nikawe mwalimu serious kwa mshahara upi wkt engineer wa tanrod anakula milioon 6 kwa mwezi hapa

Itabakia hvyo hvyo kuwa waliofelinndio wawe waaLimu wetu na pia waanzishe performance appraisal kwa walimu wasiopaerfomu vzr
Eng tanroad anakula mil 6?? [emoji23][emoji23]
Story za vijiweni hizo
 
Yaani nipate div one pcm au cbg then nikawe mwalimu serious kwa mshahara upi wkt engineer wa tanrod anakula milioon 6 kwa mwezi hapa

Itabakia hvyo hvyo kuwa waliofelinndio wawe waaLimu wetu na pia waanzishe performance appraisal kwa walimu wasiopaerfomu vzr
Engineer wa halmshauri anapokea TGS E, 940000 kabla ya makato. Huko TANROAD unakosema sio rahisi kupata nafasi kizembe
 
Back
Top Bottom