Rais Samia kupokea ndege mpya ya ATCL Julai 30, 2021

Rais Samia Suluhu Hassan kesho Julai 30, 2021 atapokea ndege mpya ya Tanzania (Bombadier DASH 8-Q400) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Ndege hiyo ni miongoni mwa ndege 11 Serikali ilizoahidi kununua (tayari ndege nane zimepokelewa nchini).

Kazi na iendelee!
 
Hii nchi ipo kwenye auto-pilot mode 🤣 🤣 ,pengine rubani halisi yupo kuzimu.
 
Kwakuwa yeye anazunguka na ile kubwa huku ile nyingine akizunguka nayo waziri mkuu, Napendekeza hii atakayopokea kesho apewe Niki wa pili nae apate toyo yake ya angani.

Ikiagizwa nyingine tena apewe Jokate, nyingine tena apewe Philip mpango na ikija nyingine apewe Kikwete kwaajili ya kufanyia ziara na kuzindulia miradi.

Baada ya hapo bunge lipitishe kodi ya kichwa kwaajili ya kumnunulia kila mbunge helikopta yake ili kuwaepusha na misukosuko ya barabarani
 
Hivi hawa watu hua wanatuonaje?
CAG anaongea hadi koo linakauka anagonga glass ya maji ya baridi mbele ya kamera akisisitiza shirika letu la ndege ni hasara mwanzo mwisho...tukiwa bado tunaugulia maumivu ya tozo, unapigwa kanzu na mapokezi ya dege jingine.
 
Safi sana mamaa.. Tanzania tunazidi kusonge mbele, huku yule mkwamishaji wetu akinyea debe.
 
Hizi zilishawekewa order kwenye awamu ya JPM kwahiyo hatuna ujanja lazima zije tu zote.
 
Mzigo mwingine wa madeni kwa mtanzania unapokelewa kesho uwanjani.
 
Hizi zilishawekewa order kwenye awamu ya JPM kwahiyo hatuna ujanja lazima zije tu zote.
Athari za mitano ya Mwendazake zitadumu kwa muda mrefu ndio maana mama anaamua kufuata humo humo.
 
Duu nilijua yashaisha ununuzi wa midege inayotuingiza hasara kumbe yanaendelea?? Inasikitisha sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…