Rais Samia: Majirani zetu wanazo The so called 'Tume Huru', hawana migogoro? Auliza nini kinafatwa kwenye tume huru

Rais Samia: Majirani zetu wanazo The so called 'Tume Huru', hawana migogoro? Auliza nini kinafatwa kwenye tume huru

Huenda kweli akawa na nia ya kurejesha siasa za ushindani otherwise she is manipulating the opposition parties not the citzen
Not really.

She is showing how unreliable and uninformed she is, as the head of state.
 
Tunataka Tume Huru ili wote tuwe na nafasi ya kula keki ya Taifa,kama CCM mtachukua viti miambili hivi mia vigawane vyama mbalimbali hilo tu.
 
KUASISIWA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI



Mwaka 1991 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi aliteua Tume ya kwanza chini ya Uenyekiti wa Marehemu Jaji Mkuu Mstaafu Francis Nyalali Madhumuni ya Tume hii ilikuwa kukusanya maoni ya wananchi juu ya kuendelea na mfumo wa chama kimoja au kuwa na mfumo wa vyama vingi.

Kutokana na ushauri wa Tume ya Nyalali ,Sura ya 3 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ilirekebishwa na kufanya Tanzania kuwa Taifa linalofuata mfumo wa Vyama vingi vya Siasa.

Sheria ya Vyama vya siasa, (Na. 5ya 1992) ilirekebishwa ili kuwezesha kuandikishwa kwa vyama vya siasa. Sheria ya Taifa ya Uchaguzi,(Na.1ya 1985), Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa,(Na. 4 ya 1979) na sheria zinazoendana pia zilirekebishwa ili kuondokana na matakwa ya chama kimoja na kuruhusu mchakato wa Kufanyika kwa Uchaguzi chini ya Mfumo wa vyama vingi vya siasa.

Mwaka1993 Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilianzishwa chini ya Ibara ya 74 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Wajumbe wa Tume waliteuliwa kwa mara ya kwanza tarehe 14 January 1993.

KUUNDWA KWA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ni Taasisi huru ya Serikali iliyoanzishwa mwaka 1993 chini ya Ibara ya 74(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977. Na Tume ya Taifa ya Uchaguzi inaundwa na wajumbe wafuatao:-

i. Mwenyekiti ambaye ni lazima awe amewahi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu au Mahakama ya Rufaa ya Tanzania au mwanasheria mwenye sifa za kuwa wakili na ambaye amekuwa katika wadhifa huo si chini ya miaka 15

ii. Makamu mwenyekiti ambaye ni lazima awe amewahi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu au Mahakama ya Rufaa ya Tanzania au mwanasheria mwenye sifa za kuwa wakili na ambaye amekuwa katika wadhifa huo si chini ya miaka 15.

iii. Mjumbe aliyeteuliwa kutoka kaika chama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society).

iv. Wajumbe wengine wanneni watu ambao wana uzoefu katika kuendesha na kusimamia chaguzi au sifa nyingine za ziada ambazo Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ataona zinafaa.

Kwa mujibu wa Ibara ya 74(7) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 na Kifungu cha 4(4) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi (Na. 1 ya1985), Mkurugenzi wa Uchaguzi ndiye Katibu wa Tume ambaye pia huteuliwa na Rais.

Uhuru wa Tume ya Uchaguzi unapotea kwa sababu ya Rais kuwa ndiye Mteuzi wa Mkurugenzi na baadhi ya Wajumbe wa Tume.

Mkurugenzi anakuwa sio mwamuzi huru wa Uchaguzi, hata Simba na Yanga, Simba ikileta refa nakuhakikishia Yanga hawatacheza hiyo mechi
 
Rais Samia akiwa anapokea ripoti ya kikosi kazi alichounda ameongelea Tume huru ya uchaguzi na kuhoji uwepo wa kuendelea migogoro kwenye nchi za jirani zinazotajwa kuwa na tume huru.

Rais Samia ametaka kujua 'Definition' ya tume huru na ipi kiu itakayopatikana kwenye tume huru.

======

Samia Suluhu: Tume huru hizo na nini mtatulete mapendekezo, tume huru maana yake nini!

Iweje? Lakini angalieni na mifano ya waliokuwa na tume huru, Je hawana migogoro ya kisiasa? The so called 'Tume Huru'.

Kwa mfano majirani zetu wanazo The so called 'Tume Huru' lakini zinaendeshwaje? Hawana migogoro? Hawatangazi matokeo wakakimbia nchi kabisa?

Si hutangaza matokeo kisha wakakimbia! Nendeni nchi mbalimbali zenye hizo zinazoitwa tume huru, angalieni yanaendaje lakini tunaposema tume huru tunafata nini hasa huko kwenye tume huru.

Kitu gani kinatupa kiu tunahisi tutakipata kwenye tume huru huko na definition hasa ya tume huru ni nini?

===

Kuhusu maboresho ya sheria na kanuni za Uchaguzi, Rais Samia amesema watasema vipengele gani vinavyouma kwani inawezekana maboresho yakifanyika, kelele ya katiba inaweza ikaishia kwasababu zile kiu za watu zinapotaka katiba ibadilishwe ilishafanyiwa kazi.

PIA, Soma=> Ikulu, Dar es Salaam: Rais Samia apokea taarifa ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa
Maana ya tume huru ni pale ambapo chama tawala kinatoka madarakani.
 
Namkubali Mama lakini naona kuna maeneo kama ana U-mbogamboga badala ya kukaa nyutro akaishepu nchi,dawa ya kuondoa malalamiko ni kutia kinachodaiwa,mambo mawili huwa mbogamboga hawayakubali na huenda hawatayakubali kitahisi ni TUME HURU NA KATIBA MOYA KABISA,siyo iliyokarabatiwa.
Haoa Mama atupatie vyote viwili,awe na legacy yake.
Sidhani kama kwa utashi wake anaweza kuamua kufanya jambo ambalo litavuruga maslahi ya wana-CCM wenzake hata kama lina maslahi kwa taifa.

Ukiwa ndani ya mfumo ni tofauti na kuwa single.
 
Mimi sitaki tume huru wala katiba mpya.

Nataka watu waelimishwe kwanza wajitambue kabla ya kuvipata vyote hivyo.

Hakuna tija ya kuwa na vifaa vipya kabla ya kujifunza kwanza kuvitumia.

Tuondoane ujinga kwanza ndio twende huko.
Kauli yako inajipinga
 
Mimi sitaki tume huru wala katiba mpya.

Nataka watu waelimishwe kwanza wajitambue kabla ya kuvipata vyote hivyo.

Hakuna tija ya kuwa na vifaa vipya kabla ya kujifunza kwanza kuvitumia.

Tuondoane ujinga kwanza ndio twende huko.
kama tumeshindwa kuondoka huu ujinga ndani ya miaka yetu 60 ya uhuru basi tena - cha msingi twende na matakwa ya jamii yetu kwa sasa - na takwa la kwanza kabisa ni KATIBA MPYA.

Tuwape wananchi hawa kuandika katiba yao wanayoitaka, hii tuliyonayo ilikuwa ni katiba ya CCM.
 
Samia Suluhu: Tume huru hizo na nini mtatulete mapendekezo, tume huru maana yake nini!

Iweje? Lakini angalieni na mifano ya waliokuwa na tume huru, Je hawana migogoro ya kisiasa? The so called 'Tume Huru'.

Kwa mfano majirani zetu wanazo The so called 'Tume Huru' lakini zinaendeshwaje? Hawana migogoro? Hawatangazi matokeo wakakimbia nchi kabisa?
Tanzania tuna safari ndefu mno.
 
Rais Samia akiwa anapokea ripoti ya kikosi kazi alichounda ameongelea Tume huru ya uchaguzi na kuhoji uwepo wa kuendelea migogoro kwenye nchi za jirani zinazotajwa kuwa na tume huru.

Rais Samia ametaka kujua 'Definition' ya tume huru na ipi kiu itakayopatikana kwenye tume huru.

======

Samia Suluhu: Tume huru hizo na nini mtatulete mapendekezo, tume huru maana yake nini!

Iweje? Lakini angalieni na mifano ya waliokuwa na tume huru, Je hawana migogoro ya kisiasa? The so called 'Tume Huru'.

Kwa mfano majirani zetu wanazo The so called 'Tume Huru' lakini zinaendeshwaje? Hawana migogoro? Hawatangazi matokeo wakakimbia nchi kabisa?

Si hutangaza matokeo kisha wakakimbia! Nendeni nchi mbalimbali zenye hizo zinazoitwa tume huru, angalieni yanaendaje lakini tunaposema tume huru tunafata nini hasa huko kwenye tume huru.

Kitu gani kinatupa kiu tunahisi tutakipata kwenye tume huru huko na definition hasa ya tume huru ni nini?

===

Kuhusu maboresho ya sheria na kanuni za Uchaguzi, Rais Samia amesema watasema vipengele gani vinavyouma kwani inawezekana maboresho yakifanyika, kelele ya katiba inaweza ikaishia kwasababu zile kiu za watu zinapotaka katiba ibadilishwe ilishafanyiwa kazi.

PIA, Soma=> Ikulu, Dar es Salaam: Rais Samia apokea taarifa ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa
independent commission ndiyo maana ya Tume Huru.

Usije ukauliza tena nini maana ya independent commission?
 
Kwani nini maana ya tume huru?
Kama mtu hawezi kuwa huru yeye binafsi katika fikra na maamuzi yake, kwa mstakabali wa taifa; ni vigumu sana kupata hiyo tume huru.

Lakini hata kama tume itaundwa na rais, watendaji wake wakaqa huru kutoa mawazo na maamuzi ya wananchi pasipo kuogopa aliyewateua, basi ni rahisi kwa na hiyo the so called tume huru!
 
Nashangaa mbona yeye ndie anakuwa kikwazo cha upatikanaji wa hiyo Tume Huru? anyway wengine hatutaki Tume Huru tunataka Katiba Mpya.

Halafu kama hajui maana ya Tume Huru kwanini asiulize akajibiwa kuliko kujitokeza hadharani na kuanza kutoa kauli zitakazoleta sintofahamu?

Vipi Zitto hawezi kumuelewesha rafiki yake kwenye hili?

Huyu Rais kama walivyo CCM wenzake hawana nia ya dhati ya kutupa Katiba Mpya wala Tume Huru ya uchaguzi, yote yanayoendelea kuunda timu zao za vikosi kazi vya uongo ni maigizo matupu, wananchi tusipoamua tutasubiri sana.
Pambaneni kwanza na Marehemu maana boss wenu katoka jela mmeanza kumtukana Marehemu ATI kawanyanyasa kaskazini, huku miradi ya maji ya Atown na Loliondo ikikamilika pamoja na ujenzi wa kiwanda Cha ngozi.

Hata hamueleweki kabisa nyie kudai katiba mpya is a great joke
 
Huenda kweli akawa na nia ya kurejesha siasa za ushindani otherwise she is manipulating the opposition parties not the citzen
You are right. Every decision of this president is spinning around. She is a dangerous manipulator
 
Muhimu kuwe na Uhuru ndani tume ili time iwe huru.

Watumishi wa tume wanapaswa kutoingiliwa na mamlaka yoyote katika utendaji wa kazi.

Hata hii time ni huru Ila dosali unaanza pale matokeo yanapoamuliwa nje Kura halali.

Tutatambua kuwa time ni huru endapo tutaacha maslahi binafsi na kuheshimu matokeo yatokananyo na kura na sii vinginevyo.

Mwaka 2020 wakurugenzi waliharibia picha ya Taifa letu kwa kukubali kutumika kuwadhurumu wapinzani katika mambo mawili, kuwaengua wagombea bila Sababu za msingi Tena bila soni yoyote na pia kutangazwa washindi ambao kimsingi hawakutokana na kura Bali maagizo ya mwendazake.

Tunaweza kubaki na mfumo wa tume hii endapo ndani ya tume Uhuru utakuwepo na wakurugenzi wa tume watatangaza matokeo yatokananyo na wapiga kura na Wala sio vinginevyo.

Pili, inapotekeo malalamiko dhidi ya tume ya uchaguzi kuwe na chombo chenye watu huru wa kuweza kuyafanyia kazi malalamiko hayo kwa muda sahihi katika mfumo sahihi.

Chombo hicho kiwe na wanasiasa toka vyama vyote na washikadau wengine ili kuwe na uwaxi katika ktenda haki.

Tatu, wakurugenzi wanaweza kutangazwa matokeo ambayo yatatokana na kura zilizopigwa na sii zile wanazoletewa na mamlaka zingine.

Nne, Maslahi ya Taifa yawekwe mbele Bali si wanasiasa, tuangalie kuwa siasa no ajira Bali owe ni njia ya kutuondolea matatizo na sio kutuletea matatizo.

Time iwe no chombo Cha kuweka mizania katika uwanja wa siasa na sio upendeleo, watu wapige kampaini kwa Uhuru ambao umewekwa kicheria bila kuvuka mipaka.

Mwisho, kila taifa Lina maagano yake,
Moja ni siasa safi
Mbili, watu wenye afya safi na ujuzi wa kuleta maendeleo,
Tatu , Ardhi safi ili itume kupunguza umasikini.

Tume hii inahitaji Uhuru Wala hatuhitaji tume mpya Bali twahitaji utashi kwa watumishi wa tume kujua kuwa tumewapa mamlaka ya kutangazwa matokeo yaliyotokana na kura na Wala sio vinginevyo.
Siku njema
 
Pambaneni kwanza na Marehemu maana boss wenu katoka jela mmeanza kumtukana Marehemu ATI kawanyanyasa kaskazini, huku miradi ya maji ya Atown na Loliondo ikikamilika pamoja na ujenzi wa kiwanda Cha ngozi.Hata hamueleweki kabisa nyie kudai katiba mpya is a great joke
Mtu yeyote atakayemtaja Mareham lazima nimtusi bahati yako hujataja jina la lile jini lililolala chattle
 
Yanabana lakini yataachia.Katiba mpya ni lazima,huwezi kuzuia hitaji la wenye nchi yao.
 
Kwa nini kila mara unapenda kurudia huu uongo na upotoshaji wako kwamba hakuna demokrasia ya kweli duniani??

Demokrasia iliyopo Canada sio ya kweli?
Huenda hao wana So called Tume Huru ila hawa Tume Huru

In short hata iliyopo duniani ni so called demokrasia lakini sio demokrasia ya kweli...

LAKINI..., faida ya hivi vitu ni kama wenzetu wanasheria wanavyosema -
Justice should not only be done but should manifestly and undoubtedly be seen to be done”.

Kwahio watu wakiona kwamba TUME ni huru hata malalamiko / sababu / excuses zitapungua hence huenda tukahamia kwenye malalamiko na Kero nyingine..., ila sababu ya kwamba fulani ingawa anacho hiki ila analalamika sio mtaji wa kutokufanya hilo jambo...

KAMA Tume sio Huru kwanini tuendelee kuwanayo ? Si bora isiwepo kabisa hili hivyo vijisenti vikafanye mengine ?
 
Waelimishwe na nani?
Mimi sitaki tume huru wala katiba mpya.

Nataka watu waelimishwe kwanza wajitambue kabla ya kuvipata vyote hivyo.

Hakuna tija ya kuwa na vifaa vipya kabla ya kujifunza kwanza kuvitumia.

Tuondoane ujinga kwanza ndio twende huko.
 
Back
Top Bottom