Rais Samia: Makonda umekichemsha sana, wapo waliokuwa wamelala

Rais Samia: Makonda umekichemsha sana, wapo waliokuwa wamelala

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwaapisha Viongozi Wateule katika ukumbi wa Kikwete Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 04 Aprili, 2024.




RAIS SAMIA: MAWAZIRI MKAJIBU HOJA ZA CAG
Siku chache baada ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (#CAG), Charles Kichere kuwasilisha Ripoti ya Mwaka wa Fedha 2022/23 kwa Rais #SamiaSuluhuHassan, Machi 28, 2024, Mawaziri wametakiwa kujibu hoja mara baada ya ripoti hiyo kufikishwa Bungeni na kujadiliwa ili hatua zichukuliwe



RAIS SAMIA: BILI ZA MAJI NI KILIO KWA WANANCHI, NAAGIZA WALIPE KAMA WANAVYOLIPA UMEME
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa ameagiza mabadiliko katika mfumo wa ulipaji wa huduma za maji akielekeza mchakato ufanyike ili malipo yafanyike kadiri mtu anavyotumia kama ilivyo kwenye ununuaji wa umeme.

Soma: Napendekeza meter za maji zifungwe mifumo ya ‘LUKU’


RAIS SAMIA: MAKONDA UMEKICHEMSHA CHAMA, NINA IMANI NA WEWE
Rais Samia Suluhu Hassan ameagiza Mabadiliko katika Mfumo wa ulipaji wa Huduma za Maji akielekeza mchakato ufanyike ili malipo yafanyike kadiri Mtu anavyotumia kama ilivyo kwenye ununuaji wa Umeme.

WhatsApp Image 2024-04-04 at 16.01.58_8e8e1eb3.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Deogratius John Pancras Ndejembi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 04 Aprili, 2024.

konda.jpg

Makonda.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Paul Christian Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 04 Aprili, 2024.

WhatsApp Image 2024-04-04 at 16.06.37_c503d0a3.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akimuapisha Kanali Evans Alfred Mtambi kuwa Mkuu wa mkoa wa Mara kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 04 Aprili, 2024.

WhatsApp Image 2024-04-04 at 16.21.14_f0e90459.jpg

Viongozi mbalimbali Wakiapa Kiapo cha Maadili kwa viongozi kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 04 Aprili, 2024.
 
Makonda apewe nafasi ya kushukuru kwa Niaba..
🤗🤗🤷
 
Back
Top Bottom