Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Rais Samia ametoa hotuba yenye hisia kali sana ,iliyowagusa watu wengi sana. Ni hotuba ya kihistoria yenye kuonyesha namna Tanzania tulivyo bahatika kuwa na kiongozi mwenye Maono, akili kubwa, upeo, maarifa na kipaji cha uongozi. Imeonyesha namna Rais wetu alivyomtanguliza Mungu katika uongozi wake.
Pengine hii ndio sababu ya kuona mambo yakienda vyema na baraka na neema zikitawala na kutamalaki hapa Nchini pasipo kupatwa na Majanga makubwa au misukosuko au migawanyiko katika Taifa letu.
Rais wetu Mpendwa kipenzi cha mamilioni ya watanzania akiwa mkoani Morogoro hii leo. Amesema ya kuwa Mapito ya kiuongozi aliyopitia pamoja na kushika nyadhifa mbalimbali imekuwa nguzo ya kumuongezea maarifa katika kuwaongoza watu.
Jemedari wetu kipenzi Daktari Mama Samia akaendelea kusema kuwa anamshukuru sana Mungu kwa kuendelea kuonyesha njia ya kuongoza Taifa letu. Hii maana yake nini ndugu zangu Watanzania?
Hii maana yake ni kuwa Rais wetu Mpendwa amekuwa mtu mwenye kumtegemea na kumtumainia Mungu katika uongozi wake na hata katika kufanya maamuzi. Ikumbukwe na kufahamika ya kuwa Mungu ndiye mtoa maarifa na njia kwa Mwanadamu na yeyote amchaye hawezi kupotea Njia.
Hawezi kujikwaa ,hawezi kuyumba wala kuyumbishwa ,hawezi kuwapoteza watu wake,hawezi kuliingiza Taifa shimoni ,hawezi kulipeleka Taifa gizani kwa sababu mbele yake upo Mkono wa Mungu umuongozao njia na Uso wake u pamoja naye na yeye Mungu Yupo ndani yake Rais wetu.
Ndio Maana siku zote huwaambieni kuwa huyu Mama ni chaguo la Mungu na aliyeinuliwa kwa mkono wa Mungu Mwenyewe.Ndio Maana ya kuja na 4R ili kuwaleta pamoja watanzania na kuishi pamoja kama Taifa. Kwa hakika huyu Mama ni Mpango wa Mungu Mwenyewe na hawezi kushushwa na mwanadamu mwenye chuki binafsi.
Embu angalia tu hata namna anavyozungumza kwa upole, upendo,ukarimu, unyenyekevu na heshima kubwa sana.tofauti na mwingine angekuwa na madaraka ya Urais ungeona akifokea na kuwatukana watu bila sababu, kuwadhalilisha,kuwatweza utu wao,kuwaumiza kwa maneno machafu mbele ya familia zao na watoto wao, kujiona yeye ndiye mwenye akili kuliko wengine na asiyetakiwa kushauriwa au kupokea ushauri wa mtu.
Lakini huyu Mama Mwenye hofu ya Mungu kifuani pake na aliyelelewa akaleleka ,aliyefundwa akafundika,mwenye heshima zake,busara zake na staha zake unaona akiwa mwenye ulimi wa haki kwa wote pasipo ubaguzi. Kwa hakika itatuchukua miaka mingi sana kumpata Mama Samia mwingine katika Taifa letu baada ya kumaliza muhula wake hapo 2030
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Rais Samia ametoa hotuba yenye hisia kali sana ,iliyowagusa watu wengi sana. Ni hotuba ya kihistoria yenye kuonyesha namna Tanzania tulivyo bahatika kuwa na kiongozi mwenye Maono, akili kubwa, upeo, maarifa na kipaji cha uongozi. Imeonyesha namna Rais wetu alivyomtanguliza Mungu katika uongozi wake.
Pengine hii ndio sababu ya kuona mambo yakienda vyema na baraka na neema zikitawala na kutamalaki hapa Nchini pasipo kupatwa na Majanga makubwa au misukosuko au migawanyiko katika Taifa letu.
Rais wetu Mpendwa kipenzi cha mamilioni ya watanzania akiwa mkoani Morogoro hii leo. Amesema ya kuwa Mapito ya kiuongozi aliyopitia pamoja na kushika nyadhifa mbalimbali imekuwa nguzo ya kumuongezea maarifa katika kuwaongoza watu.
Jemedari wetu kipenzi Daktari Mama Samia akaendelea kusema kuwa anamshukuru sana Mungu kwa kuendelea kuonyesha njia ya kuongoza Taifa letu. Hii maana yake nini ndugu zangu Watanzania?
Hii maana yake ni kuwa Rais wetu Mpendwa amekuwa mtu mwenye kumtegemea na kumtumainia Mungu katika uongozi wake na hata katika kufanya maamuzi. Ikumbukwe na kufahamika ya kuwa Mungu ndiye mtoa maarifa na njia kwa Mwanadamu na yeyote amchaye hawezi kupotea Njia.
Hawezi kujikwaa ,hawezi kuyumba wala kuyumbishwa ,hawezi kuwapoteza watu wake,hawezi kuliingiza Taifa shimoni ,hawezi kulipeleka Taifa gizani kwa sababu mbele yake upo Mkono wa Mungu umuongozao njia na Uso wake u pamoja naye na yeye Mungu Yupo ndani yake Rais wetu.
Ndio Maana siku zote huwaambieni kuwa huyu Mama ni chaguo la Mungu na aliyeinuliwa kwa mkono wa Mungu Mwenyewe.Ndio Maana ya kuja na 4R ili kuwaleta pamoja watanzania na kuishi pamoja kama Taifa. Kwa hakika huyu Mama ni Mpango wa Mungu Mwenyewe na hawezi kushushwa na mwanadamu mwenye chuki binafsi.
Embu angalia tu hata namna anavyozungumza kwa upole, upendo,ukarimu, unyenyekevu na heshima kubwa sana.tofauti na mwingine angekuwa na madaraka ya Urais ungeona akifokea na kuwatukana watu bila sababu, kuwadhalilisha,kuwatweza utu wao,kuwaumiza kwa maneno machafu mbele ya familia zao na watoto wao, kujiona yeye ndiye mwenye akili kuliko wengine na asiyetakiwa kushauriwa au kupokea ushauri wa mtu.
Lakini huyu Mama Mwenye hofu ya Mungu kifuani pake na aliyelelewa akaleleka ,aliyefundwa akafundika,mwenye heshima zake,busara zake na staha zake unaona akiwa mwenye ulimi wa haki kwa wote pasipo ubaguzi. Kwa hakika itatuchukua miaka mingi sana kumpata Mama Samia mwingine katika Taifa letu baada ya kumaliza muhula wake hapo 2030
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.