Rais Samia: Mauaji ya Kibao hayakubaliki. Uchunguzi umeanzishwa

Rais Samia: Mauaji ya Kibao hayakubaliki. Uchunguzi umeanzishwa

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameungana na Watanzania katika kulaani mauaji ya aliyekuwa kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Ali Kibao yaliyosababisha mshtuko na hisia kali nchini.

Akizungumza Septemba 17, 2024, kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya Jeshi la Polisi yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Polisi Moshi, Rais Samia amesisitiza kwamba mauaji hayo hayakubaliki kwa sababu yoyote ile. Rais Samia alisema:

"Siku kadhaa zilizopita ndugu zangu nchi yetu imepata msiba wa kuuawa kwa mmoja wa viongozi wa CHADEMA, kifo kilichosisimua miili na akili za sisi wananchi na kuibua hisia kali hasa kwa wafuasi wa chama hicho.
Kifo hicho kimeleta majonzi sio tu kwa Watanzania bali pia kwa wawakilishi wa baadhi ya mataifa ya nje wanaoziwakilisha nchi zao nchini Tanzania"

Rais Samia aliendelea kusema kwamba mauaji hayo hayakubaliki na serikali imechukua hatua za haraka kuhakikisha uchunguzi unafanyika.

Nataka niungane nao niseme kwamba kwa sababu yoyote ile mauaji haya hayakubaliki," amesema Rais Samia.

Soma Pia: Freeman Mbowe: Tutaandamana kudai watu waliopotea
 
Anajifanya hajui wakati yeye ndiyo aliwaambie wafanye huo unyama.kama ameumizwa Kwa Nini Hadi Sasa hatujapewa majibu ya uchunguzi?.uchunguzi Hadi lini wakati wauwaji wanajulikana.
 
Nataka niungane nao niseme kwamba kwa sababu yoyote ile mauaji haya hayakubaliki," amesema Rais Samia.
Tunamsubiria kwenye maandamano, shukrani sana Samia kwa kukubali kulaani mauwaji haya! Hatujui next ni Nani......
 
Hii kauli inaleta huzuni kubwa na kushangaza sana!! Anaongelea tu mauaji ya Ally Kibao. Je, utekaji unakubalika? Kama Kibao angetekwa halafu asingeuawa, kwake ingekuwa ni sawa?Au bado anaendelea na msimamo wake kuwa utekaji ni drama?
 
Yaani wameshindwa kuwatambua wauwaji? Nawezaje kupata vichekesho vingine kama hivi?? Kama kumkamata muuwaji kati Kati ya mji inashindikana Hadi leo, je usalama wetu ukoje?

Nani anamiliki acid? Watu wangapi waliwekwa kwenye acid wakayeyuka? Mmmmmgh haya
 
Huu ndiyo ulio ukweli:

"Nataka niungane nao niseme kwamba kwa sababu yoyote ile mauaji haya hayakubaliki,"
 
Alifanya makosa kuongea na wananchi kwa twitter

Jambo zito hutolewa kwa hotuba hata kama upo nje ya nchi teknolojia ya video onaweza kuitumia TEHAMA angeonekana live akiongea .


Ni muda umepita kiasi tamko la leo huko Moshi Kilimanjaro live halina mguso tena.

Kosa kubwa la kiufundi kwa rais kutotoa tamko mapema kupitia televisheni, tehama ipo mahali pote watu waione sura ya rais kama inamaanisha kweli au vipi.

Twitter inafaa kwa kutuma pongezi kwa mambo ya magoli ya Timu za taifa na vilabu vya Kariakoo.
 
Alifanya makosa kuongea na wananchi kwa twitter

Jambo zito hutolewa kwa hotuba hata kama upo nje ya nchi teknolojia ya video onaweza kuitumia TEHAMA angeonekana live akiongea .


Ni muda umepita kiasi tamko la leo huko Moshi Kilimanjaro live halina mguso tena.

Kosa kubwa la kiufundi kwa rais kutotoa tamko mapema kupitia televisheni, tehama ipo mahali pote watu waione sura ya rais kama inamaanisha kweli au vipi.

Twitter inafaa kwa kutuma pongezi kwa mambo ya magoli ya Timu za taifa na vilabu vya Kariakoo.
Hakika
 
Cku zimeenda Sasa mama na wanatajwa mpk wauwaji na picha zao zinataambaa mitandao ,mbona hawakamatwi ...
Mnyika kaitwa na mkuu wa upelelezi kinondoni kesho saa nne asubuhi,kuhusiana na kifo cha kibao
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameungana na Watanzania katika kulaani mauaji ya aliyekuwa kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Ali Kibao yaliyosababisha mshtuko na hisia kali nchini.

Akizungumza Septemba 17, 2024, kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya Jeshi la Polisi yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Polisi Moshi, Rais Samia amesisitiza kwamba mauaji hayo hayakubaliki kwa sababu yoyote ile. Rais Samia alisema:

"Siku kadhaa zilizopita ndugu zangu nchi yetu imepata msiba wa kuuawa kwa mmoja wa viongozi wa CHADEMA, kifo kilichosisimua miili na akili za sisi wananchi na kuibua hisia kali hasa kwa wafuasi wa chama hicho.
Kifo hicho kimeleta majonzi sio tu kwa Watanzania bali pia kwa wawakilishi wa baadhi ya mataifa ya nje wanaoziwakilisha nchi zao nchini Tanzania"

Rais Samia aliendelea kusema kwamba mauaji hayo hayakubaliki na serikali imechukua hatua za haraka kuhakikisha uchunguzi unafanyika.

Nataka niungane nao niseme kwamba kwa sababu yoyote ile mauaji haya hayakubaliki," amesema Rais Samia.

Soma Pia: Freeman Mbowe: Tutaandamana kudai watu waliopotea
20240916_052739.jpg
 
Ushauri kwa watao andamana, ni bora waachane na hilo swala lao

..Mama akaandamane na Chadema kuonyesha kwamba anapinga mauaji.

..Mzee Joe Biden aliungana na waandamanaji waliokuwa wakipinga mishahara midogo ya kampuni ya General Motors.
 
Rais Samia aliendelea kusema kwamba mauaji hayo hayakubaliki na serikali imechukua hatua za haraka kuhakikisha uchunguzi unafanyika.

Nataka niungane nao niseme kwamba kwa sababu yoyote ile mauaji haya hayakubaliki," amesema Rais Samia.

Nilitarajia angetupa mrejesho wa uchunguzi ulipofikia ,haiwezekani week inakaribia ya pili hajui nani alyetekeleza mauaji.
 
Back
Top Bottom