Rais Samia Mgeni Rasmi Maadhimisho ya Miaka 60 ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Agosti 21, 2023

 
Tumsikilize yupi hapa!!🙆‍♂️🙆‍♂️🙆‍♂️🙆‍♂️
 
Juha ni wale wanaoshindwa kujibu hoja za TEC, na kukimbilia kujificha kwenye uchambuzi wa mchongo TV Imaan!.
Ni mjinga tu asiye na kazi za kufanya km wewe ndo atahangaika na kijitamko chenu. Serikali ishapanga yake na mchakato waendelea
 
Tukumbushe kama walitoa Lissu alipopigwa risasi, tukumbushe ya Mbowe na kesi ya ugaidi, tukumbushe ya zuio haramu la mikutano ya Siasa, tukumbushe ya kubambikia watu kesi enzi zile, ukikumbuka tukumbushe ya maiti kwenye viroba, tukumbushe ya Kibiti.
 
Wana kelele utadhani wana historia ya kuishinda serikali
 
Huyo atatapigwa spana shoo huko huko na
 
Amen jina la Bwana libarikiwe
 
Your browser is not able to display this video.
 
KKKT watoe waraka wao siku hiyo. 😎😎
Thubutu... Hawatakiwi kuchanganya siasa na dini.
Ila kumwaalika SSH ambaye ni kiongozi wa kisiasa kwenye shughuli ya kidini ni rukhsa!
Hivi mbona huku mtaani wenye dini ndo sisi na wenye vyama ndo hao hao akina sisi?
Mbona moto ukiungua na maji yakikorogeka na wanasiasa wakivurunda ndo tunasikia hiki kisichanganywe na kile??

#Mchanga
#Mchanganuo
#Mchanganyo
#Mchanganyiko
#Mchanganyikano
 
JAKAYA UMECHELEWA SANA .DINI NA SIASA

Wassalamu Aliukhum Mabibi na Mabwana.

Kwanza nianze kwa kumshukuru Mola wetu kwa yote mema, aliotujaalia.

Naitwa Abubakari Mtanzania toka hapa tanganyika

Kubwa lililonisukuma kuandika majibu ya hoja ya dini kwa Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete,

(1)ni kauli yake ya udini & siasa kuchanganywa
(2)Kwanini Leo jumapili
(3)anajua kilichotufikisha hapa au hakijui?

Mzee kikwete Kwanza heshima yako Baba yangu na nikupongeze Sana kwa hotuba nzuri ulipotoka Leo hii jumapili siku maalumi kwa ndugu zetu wakristo wanayokutana na kufanya Ibada kwa Mola .

~FIKRA ZANGU HURU~

Nilijiuliza Sana kwanini Mzee wangu aka wa msoga ameamua kuleta taharuki kwa kauli yake ya dini na siasa?

Na ikifuatana na Ile ya ndugu Camilius wambura inayohusu kupinduliwa kwa serikali

Naomba NImkumbushe ndugu Jakaya haya yafuatayo

(1)anafahamu taasisi za dini kuwa zinatambulika kisheria ?

(2)katika tawala zetu zote kila zinapoanza kazi pale ikulu sio lazima ila mara nyingi wamekuwa wakiwaita viongozi wa dini na kutambua uwepo wao na hiii ni kutokana na majukumu ynayofanya na dini zetu katika jamii zetu hasa kimwili na kiroho pia

Lakini pia serikali inapotaka kufanya kampeni za Amani,ama maendeleo hutumia majukwaa haya ya kidini kutimiza malengo Yao na kutaka kuungwa mkono na waamini

Sasa dini na siasa ni mambo ya ayokwenda pamoja maana hata mzungu na mwarabu walikuwa na malengo nyuma ya dini hizi walizotuletea

Ambayo kimsingi hayana tofauti na siasa na ajenda hiyo ni moja tu kukuwekea mfumo wezeshi wa kukutawala wewe kikwete na Mimi Abubakar,Peter na John

Wakishindwa kuwagawa katika siasa watawagawa kupitia dini zenu

Mzee kikwete unakumbuka kuwaona DPW wakipita misikitini na kutoa misaada hapa tanzania

Na nikajiuliza kwanini hawajaenda makanisani

Lakini kwanini wapite kutoa misaada nyakati hizi ambazo sio rafiki kwao wala kwetu tena tukiwa tunajadili mikataba ilioletwa na wao na serikali yetu?

Na walipomaliza Hilo tuliona waislam wenzetu wakitoka na kupambana na watanzania wengi wanaojitokeza kupinga issue ya mkataba wa bandari

Mzee kikwete hukusema neno ulikaa kimya Mzee wangu, watanzania pia walipiga kelele kwa serikali iwazuie DP world kupitia misikitini na kuwanunua viongozi wa dini hizi kwa hongo ndogo ndogo huku wakiwa na lengo la viongozi hao wa dini watetee Jambo ambalo ni kharam kwa mujibu wa quran tukufu..

Sasa Mzee kikwete nini kimekusibu Leo ikiwa siku ya ndugu zetu wakiristu kuabudu ndio ukaja na tamko hili kwanini usingoje?

Lakini swala la kuichanganya dini na siasa Sisi raia tumejifunza toka kwenu ninyi watawala hasa serikali yetu hii sasa kama kuanza dhambi hii basi serikali ndio imeanza na Sisi tunamalizia

Mzee kikwete nadhani kingine umeshau ni kujiuliza nini kimetufikisha hapa . Naamini unakifahamu na kama ukifahamu nikumbushe

Mzee kikwete shida ni mkataba wa hovyo ulioingiwa na serikali ya tanzania na Dubai port would (DPW) tuliousoma mkataba huu tumegindua Una shida nyingi Sana ambazo kama taifa hatupaswi kufikiria hata kidogo kuingia mkataba wa aina hii

Huku majukwaani genge lako la wanasiasa wanakuja kutudanganya na wanatulazimisha tukubaliane na uongo wao

Mzee kikwete si wewe uliondoa dubwasha la Richmond?Mzee lowasa alipokuandikia anataka kujiuzuru ukabariki sio

Sasa ni sawia na hili watanzania huku mtaani tumeusoma mkataba na HATUUTAKI

Matarajio yetu mengi yalikuwa ni kukuona wewe kikwete uje hapa na ueleze msimamo wako kwenye Hilo Sakata la bandari na sio kukaa kimya ama kujificha kwenye mgongo wa dini la hasha haitotusaidia

Tumewaona baadhi ya wataafute wenye heshima kubwa katika taifa hili wakitoa maoni Yao juu ya hili la bandari ila wewe umekaa kimya

Sasa Baba yangu kikwete nikumbushe tatua tatizo lililotufanya tujikwae na usije ukatatua tatizo la hapa tulipoangukia

Lakini mwisho nikutoe hofu Mzee wangu wa msoga NI,huku mtaani sote tunaongea lugha moja tu nayo ni KATAA MKATABA WA DUBAI PORT WORLD (DPW)

kwa swala la udini hatuna shida kabisa na Moshi uliomwaga na hawa wakiristu Leo ni Sisi pamoja na Mimi Abubakar ndio hasa tunachokitaka kifanyike na sio vinginevyo

Hawa viongozi wetu wa dini hizi tunawajua baadhi Yao wakipewa makobazi, tende ,na mafuta ya Kula huku wakinogeshwa na nyama ya ngamia basi wanatusaliti

Tunawajua vyema sauti yeti Sisi watanzania hatutaki uwekezaji kharam usio na manufaa na taifa hili

Sasa Mzee kikwete njoo tusikie maoni yako ili tuokoe lasilimali za wajukuu wa Ridhiwani,na Mimi Abubakar wakati ninyi mkiwa mmeshatuacha katika dunia hii

Asante Baba wako mwananchi
Abubakar zuberi Mlangumbulu
Tanzania
 
Dr Fredrick Shoo the man who fears nobody but GOD! nenda mazeri hili jabali si mchezo lakini usije ukabwata kama Kikwete aliyejifanya kurekebisha mtumbwi uliozama kule SDA.
 
This time ni tofauti kwa yaliyoko huko ni kumuomba Mungu

Narudia this time ni tofauti ni DOA( Die or Alive)

Sent from my CPH2217 using JamiiForums mobile app
 
Mmeuza mali zenu kishenzi kwa bei ya kutupa mnataka kugawa bandari kwa wajomba? Pelekeni ushenzi wenu huko!
 
Hakika hamna atakayepona kudugwa Sindano kali na nzito ya Bandari Tulia Mwansasu jana amedugwa Sindano hii kali zaidi ya Power Safe kanisani leo tutarajie Tamko la K.K.K.T mambo ni mazito mwambieni yule mkwere atulie adugwe sindano hii kali ya Bandari
 
KKKT hawana msimamo hao
Hujawajua wewe, inapotokea jambo lenye maslahi mapana kwa Nchi kama ilivyo bandari sasahivi, Kanisa huungana na kuwa wamoja.

Jaribu kufatilia kilichotokea wakati ule wa JK na sakata lake la Mahakama ya Kadhi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…