#COVID19 Rais Samia: Miji mikubwa ya Tanzania tayari imekumbwa na wimbi la tatu la Covid-19

Sasa sisi tufanyeje? Tujikunyatie ndani? Kama ni kuvaa mask vaa hakuna aliyekukataza. Hata chanjo nimesikia mtaletewa, ikifika chanja.
 
Mkuu hivi anaweza ongea bila kuwa na data?
 
Nyie ndio kila kitu unachokisoma kwenye elimu ya kikoloni kuhusu Afrika unakibeba hook, line and sinker? Eti Ulaya na Marekani wamekufa wazee wengi na Afrika hatujafa kivile kwa sababu tuna idadi kubwa ya vijana? Muwe mnajiongeza walau hata kidogo na kujithamini wewe na uafrika wako. Ukweli ni kwamba hata Afrika wazee tunao tena wa kutosha tu na kimsingi predictions za awali ziliiweka Afrika kwenye danger zone kwenye inshu za corona. Hata leo hii pamoja na Afrika kuwa less vulnerable kwenye corona bado mainstream narrative kutoka vyombo vya habari vya magharibi vinalazimishia Afrika ionekane tatizo la corona ni kubwa.

Ubaguzi wa rangi wa mzungu dhidi ya mtu mweusi umejikita mizizi kiasi kwamba kila jambo baya duniani mzungu anatamani limkumbe mtu mweusi. Kule US ambako kuna weusi wa kutosha tulikuwa tukisoma kwenye vyombo vyao vya habari jinsi corona ilivyowaathiri "disproportionately" watu weusi kuliko watu weupe! Seriously? Hata UK nako stori ikawa hivyo hivyo. Ni ubaguzi tu wa rangi, si lolote si chochote.

Kwa ufupi ni kwamba corona ni ugonjwa wa lifestyle. Wazyngu wengi wameathirika na huu ugonjwa kwa sababu lifestyle yao (vyakula wanavyokula, mazingira wanamoishi, artificial supplements kibao wanazobugia) inawafanya wawe na upungufu mkubwa sana wa kinga ya asili. Waafrika tulio wengi bado tunaishi organic lifestyle pamoja na mazingira yetu haya tunayoyaishi. Japo kwenye advanced medical care tupo chini, ila mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Corona haijatutesa kivile kama ilivyowatesa wazungu na msitake kuifanya corona kuwa kubwa kuliko ilivyo.
 
Nyie ndio kila kitu unachokisoma kwenye elimu ya kikoloni kuhusu Afrika unakibeba hook, line and sinker? Eti Ulaya na Marekani wamekufa wazee wengi na Afrika hatujafa kivile kwa sababu tuna idadi kubwa ya vijana? ...
Kaka nilikuomba utumie mantiki ya wastani.
*Nilieleza kwa sababu gani watu wa Afrika hawaathiriki vibaya kama watu wa Ulaya, unajibu ni "elimu ya kikoloni"
* unaeleza "mainstream media" wanasema Afrika ni tatizo kubwa la Corona.

Ipi sasa??? Ama propaganda ya kaskazini inasema Afrika ina faida kwa sababu ina vijana wengi sana kuliko Ulaya (ambayo huwezi kupinga) AU propaganda ya kaskazini inasema Afrika ni tatizo kubwa ya Corona?

Kuhusu lifestyle nakubali kiasi. Kama Wamarekani weusi, pia Malatino wanakufa wengi kuliko Wamarekani weupe ina uhusiano na lifestyle yaani makazi, kazi na chakula (ingawa hapa hujalenga). Maana si swali la rangi lakini swali la umaskini, na pamoja na matajiri kama Obama n.k. asilimia ya weusi kati ya maskini wa Marekani ni kubwa kuliko asilimia yao kati ya wananchi wote.

Watu maskini wanaishi kwenye nafasi ndogo wanapobanana zaidi, tena huko katika nyumba zilizofungwa kabisa (tofauti na hapa Dar, wengi hatuna madirisha ya kioo) ambako virusi vina nafasi nzuri kubaki hewani, tena wanafanya kazi ya moja-kwa -moja kama wauzaji madukani, kupeleka barua an vifurushi kwenye nyumba za watu, ilhali idadi ya hao wanaoweza kufanya home-office kupitia kompyuta ni ndogo kuliko wastani. Yote nafasi ya kuambukizwa zaidi.

Pamoja na chakula cha maskini (lifestyle!) maana huko watu maskini wanakula zaidi fast-food kuliko watu wenye pesa, kwa hiyo watu maskini wako wanene kuliko watu wa wastani (tofauti hapa TZ), hivyo wanaathiriwa zaidi na usukari (soma: Factors contributing to higher incidence of diabetes for black Americans), hivyo wakiambukizwa na Covid wako hatarini zaidi.
 
Sasa sisi tufanyeje? Tujikunyatie ndani? Kama ni kuvaa mask vaa hakuna aliyekukataza. Hata chanjo nimesikia mtaletewa, ikifika chanja.
Unaonekana nyie ndio wake mnakunya pembeni na utu uzima huo na hata hauchambi inaondokq na mavi kwenye suruali maana hata boxer hujui kuvaa.

Mtu anaongelea kuumwa seriously we unaleta ucng wako mcng mkubwa wewe.
 
Kaka nilikuomba utumie mantiki ya wastani.
*Nilieleza kwa sababu gani watu wa Afrika hawaathiriki vibaya kama watu wa Ulaya, unajibu ni "elimu ya kikoloni"
* unaeleza "mainstream media" wanasema Afrika ni tatizo kubwa la Corona...
Huyo ni mjinga kabisa unaweza kukuta ni limtu limetoka maporini huko juzijuzi mjomba kamleta mjini amejua kununua techno ya laki na nusu halafu unabishana nae amezoea kushinda na ng'ombe tu.

Amenikwaza sana
 
Kuhusu lifestyle nakubali kiasi. Kama Wamarekani weusi, pia Malatino wanakufa wengi kuliko Wamarekani weupe ina uhusiano na lifestyle yaani makazi, kazi na chakula (ingawa hapa hujalenga)....
Usipende kuamini kila unachosoma kwenye vyombo vya habari vya kimagharibi. Tumia common sense. Huo ndio msisitizo wangu na nitaurudia tena hapa.

Kwa kuwa Marekani na Uingereza kuna weusi wengi hao wenye ajenda zao wameendelea kuionyesha superiority complex ya mzungu dhidi ya mtu mweusi kwa kuutangazia ulimwengu kwamba watu weusi wanaathirika zaidi na corona kuliko wazungu. Lengo lao ni nini? Lengo lao ni lile lile la ukoloni mamboleo katika kumtawala mtu mweusi kuanzia kwenye saikolojia yake.

Si kweli kwamba watu weusi wa marekani wameathirika zaidi ya wazungu kwenye inshu ya corona. Ni typical ya wazungu kuhusianisha kila jambo baya (magonjwa ya aina yote yakiwemo ya kuambukiza na kutoakuambukiza) na umaskini, na ndio maana walitutabiria mapema kwamba tungeokota maiti barabarani huku Afrika kutokana umaskini wetu.

Utabiri wao haukufanikiwa, lakini bado wameendelea kutusakama kana kwamba ni lazima tufe na corona. Huko Spain na Italy walikokufa kama inzi nako ni weusi maskini?
 
Inashangaza sana kusema kweli. Anatoa tahadhari watu wajikinge kwa kuepuka misongamano na kuvaa masks 😷 pia kunawa mikono halafu yeye ndiyo anasababisha misongamano!
Ukurupukaji unawaponza
Angalia swala la moto Kariakoo
Kila mtu msemaji
Huwa nawazaaaaaa
Siku hawa watawala waandikiwe barua kibarua kimeota nyasi yaani wooote wapewe barua
Tuanze upya

Wajinga wengi sana
Nchi haieleweki inaenda kulia au kushoto
Wateule hawajui kusoma wala kuandika barua ofisi kuu utafikiri mtoto wa darasa lapili kaandika....
 
Inasikitisha sana kuhusu huu mwelekeo wa nchi yetu.

 
Kama unaweza kufanyia kazi zako tokea nyumbani na haitakuathiri utendaji wako tafadhali sana bakia tu nyumbani, third wave #COVID19 its very LETHAL🙆🏾‍♂️, wimbi la 3 la korona ni HATARI mno linaua kweli kweli na haina cha sijui huyu mzee ndio yuko vulnerable,inaangusha yeyote yule.
 
Mtaani kote hakuna aliyeumwa hayo mawimbi yenu mind you sio uswahili . Btw endeleeni kutimiza wajibu wa kupandikiza hofu kwa watu maana mshachukua mgao
 
Mtaani kote hakuna aliyeumwa hayo mawimbi yenu mind you sio uswahili . Btw endeleeni kutimiza wajibu wa kupandikiza hofu kwa watu maana mshachukua mgao
I trusted you to be a great thinker! What is happening?
 
Nmeshuhudia mmoja ninaemjua ndo akili yangu imekaa sawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…