Rais Samia nae ameanza vitisho kwa waandishi kama Magufuli, inasikitisha

Rais Samia nae ameanza vitisho kwa waandishi kama Magufuli, inasikitisha

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Nimesikiliza hotuba ya Rais wetu leo kwenye maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani

Kwenye hotuba hiyo ambayo rais alikuwa katika mood ya kitofauti alisikika akiwaambia waandishi wa habari kuwa, 'ukinikuna nami nitakukuna, ila ukinikwaruza nitakuparura'

Kwa tafsiri rahisi ni kuwa anawaambia waandishi kuwa wakimuandika vizuri yeye pia atawapa favor, ila walimuandika vibaya watakiona cha mtema kuni

Hiki ni kitisho kwa waandishi kuandika habari zao kwa uhuru bila hofu ya kumkwaza Rais

Nadhani angewaasa kuandika habari kwa weledi zisizoegemea upande fulani, sio kumfurahisha
 
Rais Samia ana umagufuli na ana ukikwete pia

hana falsafa yake binafsi

mie nimemsikiliza sijaridhishwa nae

anakosema Waandishi wakiwa wanaandika watafakari kama hili litamkera Mama au laa sio sawa …hilo alipaswa amueleze Gerson Msigwa na Zuhura Yinus

Waandishi kwmy kazi yao kuna misingi ya kuzingatia ikiwemo sheria, maslahi ya Nchi na ushahidi wa wanachokiandika sio kutathmini kama Rais atafurahi au laa

Anasema ana ngozi ngumu hapo hapo anasema Waandishi wajitathnini kama habari zao zitaikera Serikali sasa hapo 'ugumu wa ngozi ' unapimwaje?

Jakaya na Mzee Ally Hassan ndio ma Rais wana Demokrasia zaid kuwahi kutokea hapa nchini na itachukua muda sana kupata wa mfanano nao
 
mie ni mpenzi sana wa kusoma Magazeti …siku hizi magazeti yote yanafanana tofauti ipo kwny jina la gazeti na mbinu za kuweka headings tu lakini contents zote zinafanana
Yale magazeti yaliyofunguliwa yataanza kufungiwa tena, kwani mara zote kosa lao huwa sio kuvunja sheria, bali kutowafurahisha watawala kwenye magazeti yao, mpaka sheria kandamizi zitakapobadilishwa ndio watakuwa huru.
 
anakosema Waandishi wakiwa wanaandika watafakari kama hili litamkera Mama au laa sio sawa …hilo alipaswa amueleze Gerson Msigwa na Zuhura Yinus

Waandishi kwmy kazi yao kuna misingi ya kuzingatia ikiwemo sheria, maslahi ya Nchi na ushahidi wa wanachokiandika sio kutathmini kama Rais atafurahi au laa
Tutegemee kupata habari za kupongeza na kusifia tuu.

Sijajua hawa watawala wanaogopa/ wanaficha nini.
 
Huyo aliyepiga picha sijui ya wapi huko ajiatathmini maana kamfanya Mh Rais hadi kaongea kwa kujishika kiuno.
 
mie ni mpenzi sana wa kusoma Magazeti …siku hizi magazeti yote yanafanana tofauti ipo kwny jina la gazeti na mbinu za kuweka headings tu lakini contents zote zinafanana
Hii biashara kichaa ndio iliyonifanya nisihangaike na magazeti, nikishaona heading asubuhi kwenye simu yangu inatosha.
 
Ila kwakweli awamu hii ya kwake.

Naona Magazeti yakimsifia mno

Kuliko awamu nyingine yeyote ile.

Unakuta magazeti karibia matano yanaandika almost the same title.

Sasa kama anataka waongeze kusifu itakua balaa.
 
Kashalewa madaraka,anabehua mvinyo!!!

Nape nae tayari ameshajisahau,labda kama siku ile pale kitaa wangekua wamemtwanga risasi moko na kumjeruhi,huenda leo nae asingetoa vitisho!!
 
Rais Samia ana umagufuli na ana ukikwete pia

hana falsafa yake binafsi

mie nimemsikiliza sijaridhishwa nae

anakosema Waandishi wakiwa wanaandika watafakari kama hili litamkera Mama au laa sio sawa …hilo alipaswa amueleze Gerson Msigwa na Zuhura Yinus

Waandishi kwmy kazi yao kuna misingi ya kuzingatia ikiwemo sheria, maslahi ya Nchi na ushahidi wa wanachokiandika sio kutathmini kama Rais atafurahi au laa

Anasema ana ngozi ngumu hapo hapo anasema Waandishi wajitathnini kama habari zao zitaikera Serikali sasa hapo 'ugumu wa ngozi ' unapimwaje?

Jakaya na Mzee Ally Hassan ndio ma Rais wana Demokrasia zaid kuwahi kutokea hapa nchini na itachukua muda sana kupata wa mfanano nao
Huyu mama bado hajajua kuwa anaamini kitu gani na anasimamia kitu gani.
Kwa kifupi anapuyanga tu.
 
Rais Samia ana umagufuli na ana ukikwete pia

hana falsafa yake binafsi

mie nimemsikiliza sijaridhishwa nae

anakosema Waandishi wakiwa wanaandika watafakari kama hili litamkera Mama au laa sio sawa …hilo alipaswa amueleze Gerson Msigwa na Zuhura Yinus

Waandishi kwmy kazi yao kuna misingi ya kuzingatia ikiwemo sheria, maslahi ya Nchi na ushahidi wa wanachokiandika sio kutathmini kama Rais atafurahi au laa

Anasema ana ngozi ngumu hapo hapo anasema Waandishi wajitathnini kama habari zao zitaikera Serikali sasa hapo 'ugumu wa ngozi ' unapimwaje?

Jakaya na Mzee Ally Hassan ndio ma Rais wana Demokrasia zaid kuwahi kutokea hapa nchini na itachukua muda sana kupata wa mfanano nao
Rais anayeongoza kwa vitisho si dalili ya kujiamini.
 
Nimesikiliza hotuba ya Rais wetu leo kwenye maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani

Kwenye hotuba hiyo ambayo rais alikuwa katika mood ya kitofauti alisikika akiwaambia waandishi wa habari kuwa, 'ukinikuna nami nitakukuna, ila ukinikwaruza nitakuparura'

Kwa tafsiri rahisi ni kuwa anawaambia waandishi kuwa wakimuandika vizuri yeye pia atawapa favor, ila walimuandika vibaya watakiona cha mtema kuni

Hiki ni kitisho kwa waandishi kuandika habari zao kwa uhuru bila hofu ya kumkwaza Rais

Nadhani angewaasa kuandika habari kwa weledi zisizoegemea upande fulani, sio kumfurahisha
Mbona waandishi wenyewe walishangilia kwa kudemka
 
Nimesikiliza hotuba ya Rais wetu leo kwenye maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani

Kwenye hotuba hiyo ambayo rais alikuwa katika mood ya kitofauti alisikika akiwaambia waandishi wa habari kuwa, 'ukinikuna nami nitakukuna, ila ukinikwaruza nitakuparura'

Kwa tafsiri rahisi ni kuwa anawaambia waandishi kuwa wakimuandika vizuri yeye pia atawapa favor, ila walimuandika vibaya watakiona cha mtema kuni

Hiki ni kitisho kwa waandishi kuandika habari zao kwa uhuru bila hofu ya kumkwaza Rais

Nadhani angewaasa kuandika habari kwa weledi zisizoegemea upande fulani, sio kumfurahisha
Rais yuko sahihi kwa asilimia 100. Tena kafanya vema kuwagonga waandishi kutoka nchi zote za Afrika. Waandishi (baadhi) wa Afrika ndiyo wanaolibagaza bara hili. Wanajua tu wanezaliwa Afrika lakini hawajui THAMANI YA AFRIKA. Hawana tofauti na baadhi ya wanasiasa wasiojua THAMANI YA AFRIKA. WAJISAHIHISHE.
 
Ukimsimiliza SSH vizuri unagundua ni mtu anaji-contradict mwenyewe kwenye maelezo yake. Atakwambia ana ngozi ngumu lakini hapo hapo atakupa vitisho.
Mtu kama huyu inabidi asome hotuba kama alivyoandaliwa... vinginevyo haeleweki vizuri kwa wananchi na watendaji wake!
 
Nimesikiliza hotuba ya Rais wetu leo kwenye maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani

Kwenye hotuba hiyo ambayo rais alikuwa katika mood ya kitofauti alisikika akiwaambia waandishi wa habari kuwa, 'ukinikuna nami nitakukuna, ila ukinikwaruza nitakuparura'

Kwa tafsiri rahisi ni kuwa anawaambia waandishi kuwa wakimuandika vizuri yeye pia atawapa favor, ila walimuandika vibaya watakiona cha mtema kuni

Hiki ni kitisho kwa waandishi kuandika habari zao kwa uhuru bila hofu ya kumkwaza Rais

Nadhani angewaasa kuandika habari kwa weledi zisizoegemea upande fulani, sio kumfurahisha
Ungemsikiliza vizuri acha kudandia maneno
 
Rais yuko sahihi kwa asilimia 100. Tena kafanya vema kuwagonga waandishi kutoka nchi zote za Afrika. Waandishi (baadhi) wa Afrika ndiyo wanaolibagaza bara hili. Wanajua tu wanezaliwa Afrika lakini hawajui THAMANI YA AFRIKA. Hawana tofauti na baadhi ya wanasiasa wasiojua THAMANI YA AFRIKA. WAJISAHIHISHE.
Kwa hiyo kujua thamani ya Afrika ni kuandika habari za kumfurahisha rais?
 
Back
Top Bottom