Rais Samia ni nani hata mvua zimtii?

Rais Samia ni nani hata mvua zimtii?

Mbingu na Nchi zinamtii Muumbaji wa waumbaji ni Yesu kristo.

Kwa neno lake anaweza kukunja Nchi na kuwa kama karatasi.

Wengine wana dosari.

Una uwakika gani kabla ya huo mkutano kuna watumishi wa Bwana yalifanya Maombi ya Mvua, Bwana akafanya kuwapa itaji lao
Unataka kuamisha sifa za watumishi wa Bwana kupeleka kwa Rais?

Imani ya Rais inafanana na imani yako ya kuokoka kumpenda Yesu. Mungu gani unayempatia sifa alijibu Maombi ya Rais?
 
John 1:1-3
[1]In the beginning was the Word, and the Word was with God, and the Word was God...
Mungu anaitwa Neno au sijakuelewa,usianze kuvuruga watu asubui hii.

Aafu bora usiendelee naona unaelekea motoni. Embu mtafute ndugu yako anaesoma dalasa la tano kisha msomee aafu muulize amefahamu kitu gani ? Ndio utajua maana ya kuburuzwa.
 
Sasa iweje sifa umpe mwanasiasa badala ya kuwapa hao viongozi wa dini walioomba?...
Hilo linawezekana ni ujanja tu,mi mbona nikiomba mvua ilikuwa inanyesha ila watoto wadogo waliniona kama nina miujiza kumbe ,nikishaona wingu zito na radi za hapa na pale zimeanza basi huwaita wasio na akili timamu na kuwambia ngojeni niombe mvua,sijamaliza mvua hio.
 
John 1:1-3
[1]In the beginning was the Word, and the Word was with God, and the Word was God.
Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu...
In the beginning was the Word, and the Word was with God, and the Word was God.

Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. (Tiyari ushaweka Mungu wawili).
jaribu kuifahamu lugha ndugu yangu mlokole, niseme tu Nyamagondo alikuwepo kwa askari,Nyamagondo nae ni askari (Askari wangapi hao?)
 
Huyuhuyu Rais ambaye anafurahia kupata urais kwa kufa mwenzake ndo mbingu na nchi zinamtii?.
 
Mungu anaitwa Neno au sijakuelewa,usianze kuvuruga watu asubui hii.

Aafu bora usiendelee naona unaelekea motoni.
Embu mtafute ndugu yako anaesoma dalasa la tano kisha msomee aafu muulize amefahamu kitu gani ? Ndio utajua maana ya kuburuzwa.
Na wewe ficha ujinga, mwenzako amequote scripture! Kama huamini ungefungua kwanza hiyo Yohana chapter 1!!
 
Andiko jingine lanena:
John 1:18 “No one has ever seen God, but the one and only Son, who is himself God and is in closest relationship with the Father, has made him known...
Usinishike,kwa maana sijapaa kwenda kwa baba,baba yangu ambae ni baba yenu,mungu wangu mungu wenu
Mungu wangu mungu wangu,mbona umeniacha!!?
 
Hili likemewe kwa nguvu zoote.Kama inawezekana Mh.Rais atoke hadharani alikemee au wasaidizi wake wafanye hivyo haraka saana.
ANGALIZO.

Tuwe nakini na mipaka yake Mwenyezimungu,tusiivuke.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Na wewe ficha ujinga, mwenzako amequote scripture! Kama huamini ungefungua kwanza hiyo Yohana chapter 1!!
Ukweli ndio utakaowaweka kuwa huru ,utafuteni.

Mungu hafi. Mungu hajiombei dua. Mungu hajibishani kimwenyewe mwenyewe. mengi tu inahitaji mjifunze ili muwe huru, Tuseme Mungu alikuwemo ndani ya yesu lakini Yesu sio Mungu ,hapo panahitaji ufahamu sio uvamizi.

hebu kasomeni Yohana kumi na inne muifahamu kwa kina.

1 Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.

2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.

3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.

4 Nami niendako mwaijua njia.

5 Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia?

6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

7 Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.

8 Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.

9 Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?

10 Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake.

11 Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe.

12 Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.

13 Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.

14 Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.

15 Mkinipenda, mtazishika amri zangu.

16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;

17 ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.

18 Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu.

19 Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.

20 Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu.

21 Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.

22 Yuda (siye Iskariote), akamwambia, Bwana, imekuwaje ya kwamba wataka kujidhihirisha kwetu, wala si kwa ulimwengu?

23 Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.

24 Mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalolisikia silo langu, ila ni lake Baba aliyenipeleka.

25 Hayo ndiyo niliyowaambia wakati nilipokuwa nikikaa kwenu.

26 Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.

27 Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.

28 Mlisikia ya kwamba mimi naliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahi kwa sababu naenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.

29 Na sasa nimewaambia kabla halijatokea, kusudi litakapotokea mpate kuamini.

30 Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu.

31 Lakini ulimwengu ujue ya kuwa nampenda Baba; na kama vile Baba alivyoniamuru; ndivyo nifanyavyo. Ondokeni, twendeni zetu.
 
Wapo watu wana makarama mengi na makubwa sana na bado hawawi mitume wala kujiona Mungu - Tunasema wamepewa uwezo wa kuyatekeleza hayo.

mambo wanayoyafanya sisi walala hoi wengine hatuwezi kuyafanya ,hivyo Jesu alitunukiwa kuwa na makarama na makarama hayo uamini kuwa Mungu yupo na sio yeyey. Mijitu haifahamu sijui ikoje ,halafu lugha very simpo.
 
Back
Top Bottom