Rais Samia: Nitaifumua Wizara ya Mambo ya Nje

Rais Samia: Nitaifumua Wizara ya Mambo ya Nje

January hana speed yoyote best labda ya upigaji tu. Hakuna wizara yoyote kaacha alama positive labda ile ya kuzuia mifuko ya plastic tu
Watu huwa hawakisii.

Reforms and Rebuilding.
 
Rais Samia Suluhu Hassan ameweka wazi kuwa ataifumua na kuisuka upya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, ili kuirudishia hadhi baada ya kuwa na utendaji usioridhisha kwa muda mrefu.

Hatua hiyo imekuja kutokana na wizara hiyo kupoteza ushawishi kwenye medani za kidemokrasia, huku mashirika ya kimataifa yakilalamika kutoridhishwa na utendaji wa wizara hiyo nyeti.

Rais Samia amesema hayo jana, wakati akipokea ripoti ya kamati ya kutathmini ufanisi na utendaji wa wizara hiyo, kazi iliyofanyika kwa miezi sita chini ya uenyekiti wa Balozi Hassan Simba Yahaya.

Amesema muundo wa wizara hiyo unaenda kuangaliwa upya, ikiwemo namna ya kuwapata watumishi wenye sifa stahiki, kwa kuwa wengi waliopo hawana uwezo.

Amesema kwa muda mrefu wizara imekuwa ikitawaliwa na urasimu katika kuajiri, hali iliyosababisha watu wasio na sifa kuajiriwa kwa maelekezo ya vigogo ndani ya wizara.

“Ripoti imeeleza hapo katikati ajira hazikuwa katika mpangilio mzuri, zilikuwa chache na zilitolewa kwa kujuana. Sasa mengine nayafahamu mie hata kwenye ripoti hayajawekwa, pia kuna makundi, hamisha hamisha na panga pangua ya maofisa waandamizi haya yote yalichangia utendaji wa wizara kupwaya.

“Hili ni moja ya masuala yanayonisukuma kutaka kamati hii uindwe na kuifanyia tathmini wizara, ubobezi ule wa miaka ya 90 na 2000 sasa wizarani hakuna, unguli, umahiri na ushawishi wetu kwenye medani za kidemokrasia umekuwa wa kujikongoja.

Kumekuwa na malalamiko kutoka taasisi za kimataifa zilizopo nchini kuhusu utendaji usioridhisha wa wizara hii,” amesema Rais Samia.

Pia aligusia uwakilishi wa nchi kupitia balozi zake katika mataifa mbalimbali akitaka mpangilio huo kuangaliwa upya kulingana na hali ya sasa.

“Tunapaswa kuangalia upya suala la uwakilishi wetu kupitia balozi tulizonazo nje ya nchi na hadhi zake kutokana na mabadiliko yaliyopo duniani. Wakati ule tulikuwa tunaanzisha balozi kwa kuangalia wanaotusaidia pesa nyingi, lakini mambo yamebadilika, lazima tuangalie wapi tuwe na balozi za kupewa nguvu,” amesema.

Sambamba na uwakilishi wa nchi, alizungumzia pia namna teuzi za mabalozi zinavyofanyika, huku akitaka jukumu hilo sasa wapewe watu wanaostahili na sio kwa kuoneana haya.

“Tunavyofanya sasa wizara inaleta mapendekezo, yanavyoletwa na mie nina yangu mkononi naletewa nani kaharibu wapi anaweza kupelekwa. Sasa hujui mapendekezo yapi ya kisiasa, yapi ya kitaaluma.

“Sasa hivi tufumbe macho anayevurunda kazini akae pembeni, hakuna haja ya kumpoza kumpeleka kwenye ubalozi, lakini pia nafasi za kisiasa hatusemi zisiwepo, lakini tuangalie kwa asilimia gani. Ila changamoto wakati mwingine hao wenye taaluma hawapo pale wizarani kwa sababu ya undugu uliojaa,” amesema.

Kufuatia hilo, kiongozi huyo mkuu wa nchi alielekeza kuwepo vigezo vya kuajiri watumishi katika wizara hiyo na kuondokana na mfumo uliopo sasa ambao unaruhusu watu wasio na sifa kubebwa.

“Hapa mkono wa Rais unakwenda kuingia kwenye hii wizara, tutaanzisha mfumo maalumu wa ufadhili wa kutengeneza vijana ambao watakwenda kufanya kazi pale.

“Haitakuwa rahisi, ni lazima wawe vijana wenye sifa, watafanya mitihani, wakifaulu ndiyo watawekwa kwenye fellowship hii kwa miaka miwili wakipikwa kisha tuwapeleke wakafanye kazi,” amesema Rais Samia.

Awali, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Balozi Yahaya alipendekeza kubadilishwa kwa jina la wizara, akieleza jina la mambo ya nje haliakisi vizuri majukumu ya wizara husika.

“Pia tunashauri kuwa na umadhubuti wa uongozi wa mambo ya nje ili viongozi waweze kutumikia kwa muda wa kutosha kwa lengo la kutunza kumbukumbu na misimamo ya nchi na kushughulikia masuala ya kimataifa yanayohitaji ufuatiliaji,” amesema balozi Yahaya.

Pia, kamati ilipendekeza kuundwa kwa idara ya uchambuzi wa kimataifa na kupendekeza jukumu la uchambuzi wa taarifa hizo, habari na matukio mbalimbali liondolewe kutoka idara ya Sera na mipango na iundwe idara mpya.

Credit: Mwananchi
Mama anza na ripoti ya CAG. Tekeleza maoni yake kwa kuwachukulia hatua za kisheria wale waporaji walio katika balozi zetu. OVER
 
“Sasa hivi tufumbe macho anayevurunda kazini akae pembeni, hakuna haja ya kumpoza kumpeleka kwenye ubalozi.
Duh....!. Sasa leo ndio nimeelewa!. Kwa muda mrefu nimekuwa najiuliza, imekuwaje mtu mwenye level ya DGIS, anateuliwa ubalozi na kupostiwa nchi ya hovyo tuu?!. Sasa nimeanza kupata majibu!.

Tuliwahi kushauri Wito Kwa Viongozi Wetu: Unapokosea, hata kwa kujikwaa tu ulimi, tujenge utamaduni wa kuwajibika ili kumuepushia Rais wetu kubeba mzigo wa karma

Kisha tukashauri tena, Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere?

Sasa ushauri huu umepata sikio la kuusikia, sasa unakwenda kufanyiwa kazi, kiongozi anayevurunda mahali, hata awe nani, hakuna tena kupoozwa kwa kupewa ubalozi!, atupishe kazi iendelee!.

Ila Mama nae...!, ameanza kuwa mkweli wa type ya JPM, hakopeshi!. Kumbe kuna watu huwa wanavurunda, ila kwa vile post zao ni nyeti sana!, wanaondolewa hapo walipovurunda na kupoozwa kwa kutupwa ubalozini!.

Naunga mkono hoja, wanaovurunda, wasipoozwe na ubalozi, watupishe!.
P
 
[emoji23][emoji1787][emoji1485][emoji22] Vijana wenye spidi kali unawaelewa vizuri binti yangu?.

Wewe unaelewa nini maana ya ujana maji ya moto?.

Kijana aliyechelewa na mwenye njaa, katoka huko nanjirinchi mwambeo unampa kwa speed kali unategemea nini?.

Hivi pasipo kuwa na maamuzi ya kumfundisha huyo kijana wako mwenye speed 120kph unadhani atafika salama?.

Umemuona mdogo wako alipokuwa pale wizarani alichofanya?, Tena ndiyo mmoja wa hao vijana wenye speed kali.

Naendelea kujifunza tabia ya binadamu!.
wewe nanjilinji huwezi kuiandika,itajua vijana wenye spidi?
 
January hana speed yoyote best labda ya upigaji tu. Hakuna wizara yoyote kaacha alama positive labda ile ya kuzuia mifuko ya plastic tu
Hiyo ya kuzui mifuko ilibebwa na aina ya serikali iliyopo huyo januro haina influence yoyote
 
mifuko ya plastik siyo yeye aliyezuia na wala hakuwa na uwezo huo ilikuwa ni mpango wa serikali 2015/20 hivyo yoyote ambaye angekuwa hiyo wizara angezuia pia hata kama angekuwa nape …
Agreed with you
 
Mama anza na ripoti ya CAG. Tekeleza maoni yake kwa kuwachukulia hatua za kisheria wale waporaji walio katika balozi zetu. OVER
Hivi report ya CAG ya mwaka huu ipo wapi jamani ,au wameamua kumpiga spana CAG kupitia mwigulu na Nepi
 
Duh....!. Sasa leo ndio nimeelewa!. Kwa muda mrefu nimekuwa najiuliza, imekuwaje mtu mwenye level ya DGIS, anateuliwa ubalozi na kupostiwa nchi ya hovyo tuu?!. Sasa nimeanza kupata majibu!.

Tuliwahi kushauri Wito Kwa Viongozi Wetu: Unapokosea, hata kwa kujikwaa tu ulimi, tujenge utamaduni wa kuwajibika ili kumuepushia Rais wetu kubeba mzigo wa karma

Kisha tukashauri tena, Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere?

Sasa ushauri huu umepata sikio la kuusikia, sasa unakwenda kufanyiwa kazi, kiongozi anayevurunda mahali, hata awe nani, hakuna tena kupoozwa kwa kupewa ubalozi!, atupishe kazi iendelee!.

Ila Mama nae...!, ameanza kuwa mkweli wa type ya JPM, hakopeshi!. Kumbe kuna watu huwa wanavurunda, ila kwa vile post zao ni nyeti sana!, wanaondolewa hapo walipovurunda na kupoozwa kwa kutupwa ubalozini!.

Naunga mkono hoja, wanaovurunda, wasipoozwe na ubalozi, watupishe!.
P
It's too late ,kama imemchukua miaka 3 ndo anagundua hilo vipi mambo mengine
 
Dawa Kali ni kuwa na effective and realistic performance appraisal tool , watumishi wote wa hiyo wizara wanapewa tasks/targets and timeline anaeshindwa anatolewa, no other way! Hivi ndivyo Rais atafanikiwa akifanya vinginevyo atavuna mabua!

Balozi za nje hazina msaada kwa taifa hazileti wawekezaji, hazitangazi fursa zilizoko nchini na hazina msaada kwa watz wanaopata matatizo huko ughaibuni, hata passport ikiisha muda ukiwafuata wanakwambia rudi bongo ukarenew! Narudije bongo na kibarua nimwachie nani! Kazi zao hazieleweki hasa ni zipi! Binafsi siwapendi kabisa hao maofisa wa ubalozi wengi wao ni vilaza wenye ubini za Vigogo wa bongo!
 
Mabalozi wetu wa kitanzania huwa hawajitokezi kuhojiwa ktk vyombo vya habari huko wanakotuwakilisha, sababu ni nini ? Hawapo YouTube, ktk Televisheni, vyuo vikuu kutoa muhadhara wala magazetini online ! Tofauti na mabalozi wa mataifa mengine

10 October 2023
Nairobi, Kenya

GUEST: H.E Amb. Hazem Shabat- Palestinian Ambassador To Kenya


View: https://m.youtube.com/watch?v=1Y8Gr15VkAg

This Is The Situation Room, Kenya's Biggest Conversation!Hosts: Eric Latiff, Ndu Okoh & CT Muga Producer: Ednah Ombaso Executive Producer: Tom Japanni
Source: SpiceFM
 
Ni kweli mabalozi wasukwe tangu wakiwa vijana waive kwenda kuwakilisha maslahi ya nchi, badala ya kuteua wazee waliochoka wanaoendekeza siasa kuwa mabalozi ikiwa kama pensheni ya kustaafu.

Naono mengi ya wafalme waliotawala dola zao kubwa za kitaifa waliamini katika kukuza vipaji tangu vikiwa vinaonekana ndani ya vijana kisha mbali ya kuwaendeleza pia kuwapeleka shule maalum kupata elimu wawe mabalozi au viongozi watendaji wazuri wa serikali.

A monarchist will not agree that the state should be ruled by a politician, instead he will prefer a person who has been educated to rule. Black Hundreds – Nicholas II and
 
Back
Top Bottom