Rais Samia: Rais haruhusiwi kukaa mkoa mmoja kwa zaidi ya siku tatu

Rais Samia: Rais haruhusiwi kukaa mkoa mmoja kwa zaidi ya siku tatu

ukitafakari vizuri utagundua wewe ndio umeishiwa
Wala haina haja ya kutafakari vizuri. Huyo kashaishiwa maana hajitambui. Tena hatakiwa kukaa Dodoma siku mbili ni vile tu kuna mtu alichanganyikiwa kabla yake.
 
Mabibi na mabwana mheshimiwa Rais wetu mpendwa mama Samia amepasua mbarika tena leo.

Akiongea na vijana Mwanza, mh. Rais katamka angependa kuendelea kukaa zaidi Mwanza, ila taratibu na sheria hazimruhusu kukaa zaidi ya siku 3 katika mkoa mmoja.

Bila shaka akimaanisha kukaa siku 3 mkoani nje ya ofisi rasmi za Magogoni au Chamwino.

Hizi sheria au taratibu ni mpya zilizoanza baada ya awamu ya sita kuingia ofisini au ndiyo ilivyo ila ilikuwa kupigana ma-changa ya macho?

Kumbukumbu zingali hai kwani si zamani tulipoaminishwa katika awamu ile kuwa rais anaweza kuweka kambi popote na kazi ikaendelea bila ukomo!

Kama aliyosema mama leo ndiyo ukweli wenyewe basi pongezi sana mama Samia kwa kuzingatia maadili, taratibu na sheria.

Unatudhihirishia kwa vitendo kuwa unayo nia ya dhati ya kuhakikisha kuwa wewe kama tunavyowajibika sote kwa mujibu wa sheria wewe kama rais siyo exceptional.

Hongera sana mama Samia kwa kuzingatia utawala wa sheria kazi inapoendelea!
Magufuli alikuwa anakaa hata mwezi kule kwao. Mwanaume unaenda kwenu kila siku kama umeolewa bana.
 
Wewe unasumbuliwa na ulimbukeni, ungetafuta kwanza sheria inayoipa nguvu kauli yake kuliko kushadadia kiu kisichokuwepo.

Mwulize, kwanini yeye amekaa Dar Es Salaam ambako ni mkoani kwa zaidi ya miezi miwili sasa huku akijua ofisi kuu ya Rais ni Dodoma-Chamwino?

Usipende kurukia kipande cha sentensi kisicho na ushahidi kisha unaanza kukinyambulisha kukidhi matakwa yako.

Weka hapa kifungu cha sheria ama kutoka kwenye katiba, mamlaka ya Rais, Matamko ya Rais nk ambacho kinathibitisha kilichosemwa ni kweli bila hivyo hizo ni siasa tu za kujaribu kumnanga mtu. Mbona JK alikaa miezi minne nje ya nchi huku akiendelea kutea watendaji na kutoa maagizo kama kawaida.

Jimbo la Rais ni Tanzania sio Magogoni au Chamwino hivyo popote anaweza kutekeleza majukumu yake ilimradi hakuna sheria inayovunjwa.

Lile genge pendwa linajulikana kwa wingi wa mapovu. Hakuna jipya hapo!

Tambua miye kama wengine tumesikia mama akisema. Yumkini mlisali tusiwe tumesikia 😂😂😂😂😂! Magogoni na chamwino ni rasmi hata tausi wanajua hivyo.

Kama ada tutaendelea kujifunza mengi mengine kazi inapoendelea.

Aliyosema mama yanahusu ziara za hapa nchini, za nje zinahusika vipi kama si kuweweseka kwenu?
 
Lile genge pendwa linajulikana kwa wingi wa mapovu. Hakuna jipya hapo!

Tambua miye kama wengine tumesikia mama akisema. Yumkini mlisali tusiwe tumesikia 😂😂😂😂😂! Magogoni na chamwino ni rasmi hata tausi wanajua hivyo.

Kama ada tutaendelea kujifunza mengi mengine kazi inapoendelea.

Aliyosema mama yanahusu ziara za hapa nchini, za nje zinahusika vipi kama si kuweweseka kwenu?
Taja sheria inayosema Rais haruhusiwi kukaa mkoa mmoja kwa siku tatu mfululizo hapa wala usikimbie kivuli chako
 
Taja sheria inayosema Rais haruhusiwi kukaa mkoa mmoja kwa siku tatu mfululizo hapa wala usikimbie kivuli chako

Humjui aliyetamka hayo? Huijui taasisi iliyotamka hayo?



Si mlituaminisha ile ofisi ni taasisi?

Hujui kuna mtu kayatamka hayo tena leo hii na sisi tunamnukuu tu kwa kupasua hiyo mbarika mliyokuwa mmetuaminisha vinginevyo?

Viva mama Samia Suluhu endelea kutujuza tuliyokuwa tumeingizwa cha kike!

Wewe ndiye mwenye ufahamu kuliko hao? Nenda kawaelimishe huko basi, vinginevyo ya kwako ni kelele za chura mwingine dimbwini tu 😂😂😂😂😂!
 
Kila mkoa kuna Ikulu kacha kupotosha zenye hadhi sawa. Mwanza kuna Ikulu ya Rais iko pale Capri Point barabara ya Nasser karibu na Kamanga ferry kwa hiyo anaweza kufyanya kazi kutokea hapo hata kama kwa mwaka mzima..
Hizo ni Ikulu ndogo, ziko mikoa yote na hata wilayani. Ikulu kuu ni Chamwino Dodoma na Ikulu ya Magogoni Dar es Salaam, hizi ndizo anakaa kwa muda wote siyo hizo ndogo za mikoa na wilaya.
 
ilikuwaje sasa mwendazake alikuwa anapiga kambi chato miezi bila kujali chochote,kwa maanna hiyo kumbe alikuwa mvunja taratibu na kanunni dah jamaa alikuwa anaogopwa hadi na chama chake

Hii nchi imechezewa sana! (Haya si maneno yangu.)
 
... nakubaliana na wewe. To be objective, wataalamu watuwekee sheria, kanuni, presidential decree, au chochote kile kinacho support kauli ya Mh. Rais. Otherwse, tutakuwa tunajadili kitu tusichokielewa simply Rais kasema! This is wrong!

Rais na taasisi nzima ya urais wapo.

Mama kasema walishauriana wote wakaona kuzidisha zaidi ya siku 3 ni kutoka nje ya misingi:



Jinasibu kuwasiliana naye au taasisi yake kwa ufafanuzi.

Sisi wapenzi wake anapopasua mbarika kama hivi, kwetu ni burudani tu. Kazi na iendelee!

Habari ndiyo hiyo.
 
Kiswahili kabisa tunaojua tamaduni zetu, ukiondoka sehemu kuaga lazima uwe na excuse, huwezi kuaga tu ukaondoka bila excuse.
 
Back
Top Bottom