Rais Samia Suluhu afanya uteuzi wa viongozi mbalimbali

Duu...luteni jenerali ndo ameshachomolewa jeshini hapo

..nina ndugu yangu amesoma na Lt.Gen.Yakubu Mohamed amestaafu tangu mwaka juzi.

..kwa hiyo bila shaka CoS Yakubu Mohamed amefikia umri wa kustaafu.

..CoS Mwakalindile aliteuliwa balozi Msumbiji. Cos Kiwelu aliteuliwa balozi Ufaransa. CoS Abdulrahman Shimbo aliteuliwa balozi China.
 
🤣🤣🤣🤣
Hapo Samia inabidi atembee kwa uangalifu sana. Hakuna kitu kitamtoa haraka Ikulu kama watu wa bara kuanza kuwa na hisia kama hizo.
Nani au nini nje ya force majeure chenye ubavu wa kumtoa Ikulu Rais wa JMT kabla ya muda wake kuisha?
 
Hayo majina ya kiislamu hapo ataambiwa mdini.
Tumuache mama jamani afanye kazi yake,ni kama enzi za mwendazake wa upande wa pili walivyokuwa wanapendelewa basi nao hao ni zamu yao
 
Huyo Lt Gen kapelekwa Uturuki kule waliko stage mapinduzi fake kuwa hadaa wazungu! Mwanajeshi muasi yuko ndani ya kifaru anashambuliwa na bomu la machozi la polisi mtii. Dunia hii inayo mambo na majambozi.
 
Hii Ya Prof. Elsante Ole Gabriel Naona Kama Ni Silent Demotion, Kutoka Kuwa KM Wa Wizara Mpaka Kuwa Mtendaji Mkuu Wa Mahakama.

Wajivu Wa Mambo Tuwekane Sawa
 
Kwenye nchi za kiislamu anapeleka waislamu, nchi za kikristo nako anapeleka Wapemba! Hii imekaaje
Asilimia kubwa ya wawekezaji katika sekta ya utalii Zanzibar ni Waitaliano, na Z'bar ni mbia katika Muungano, kwahiyo wakati anafanya kazi za Jamhuri atakuwa analink na visiwani, na bahati nzuri aliyepelekwa ameshakuwa Waziri wa mambo ya utalii Zanzibar, mawazo yangu🙏
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…