Rais Samia Suluhu akiendelea kumkumbatia Majaliwa na Baraza lake Serikali yake haitofanikiwa, Hawana jipya

Keshawapuuza sasa mmeanza ramli na matusi.Asante Rais Samia kwa kupuuza hiki kikundi cha wahalufu kazi iendelee
Awamu ya 5 ndiyo awamu pekee iliyoshuhudia ufisadi wa kihistoria tangu Tanzania ipate uhuru
 
Mkuu kuhusu ilani umemaliza,

CCM huwa wanadanganywa kuwa ilani ndiyo itaongoza nchi hawajui ilani ni maneno ya hadaa ya kutafutia kura mtu mmoja, Baada ya Kikwete kuchaguliwa alisema urais wake hauna ubia, baada ya Magufuli kuchaguliwa hatukusikia akisema Tanzania ya CCM bali Tanzania ya Magufuli, wajinga ndio waliwao.
 
Wewe vipi, kwani mimi nimesema ni Rais nusu... Mbona huna heshima, huyo ni Rais wa kurithi, huo muda wa kutengeneza wafuasi ndani ya chama hana, hata huo ushawishi hana ndani ya chama, kufanya anachotaka huo uwezo hana kwa sasa, akifanya hivyo labda awe anataka kuua chama, maana 2025 kitakuwa kibarua sana, sasa huo upumbavu mnaotaka afanye kuna adhabu yake
 
Ila watanzania tu wanafiki sana na ni HERI MCHAWI KULIKO MNAFIKI. Tuache unafiki ukiona jambo ulitakalo haliendi mfuate yule unayejua anahusika mwambie rekebisha hapa habari za kutakamwenzio ashushwe pale alipo na unajua kabisa wewe uwezi kwenda kukaa hapo unafaidi nini
 
hoja hapa mnataka Majaliwa atemwe au asiwe na hizo sifa ulizotaja?
ni kama mmechanganyikiwa kila kitu mnataka nyie,wakati mna mbunge mmoja tu
Tatizo lenu nyinyi sukuma gang mnataka mama aendeleze tabia zenu mlizo zoeshwa jambo ambalo mama hataki .

Mnajitahidi kulazimisha lkn wapi mnaagukia pua.
 
Anafanya kile alichokubaliana na wananchi kupitia ilani ya chama full stop!
Endelea kusubiri ilani ya chama ikukomboe, soma katiba once anakuwa rais halazimishwi kufuata mawazo ya mtu yeyote yule ikiwemo ilani, ndio maana Magufuli alikuwa akifanya hata ambayo hayamo kwenye ilani.
 
Kwa taarifa yako mama hawezi kamwe kusikiliza huo ujinga wenu maana tayari anawajua vema nyinyi wapiga zumari wa ccm.

Anataarifa zenu zote hivyo msijidanganye kumtisha mara hana ushawishi, mara hana umaarufu na kama ingekuwa umaarufu kwenye chama ndiyo kupata urais basi leo hii rais angekuwa Wasira.
 
Wabunge wote wanaitegemea ilani ya ccm iwasaidie kutekeleza miradi kwenye majimbo yao, wataangukia pua .na mwakà 2025 hawaitarudi tena bungeni na hakuna tena ubabe wa kuiba kura
 
Yaani kuwa na PM muongo ni uhujumu mkubwa sana wa taifa, ni sawa na kuwa na taifa lenye mafisadi tupu
 
Kwahiyo unashauri pia aendeleze na ufisadi mlioufanya kwenye awamu ya 5?
Bora ufisadi wa awamu ya tano lakin mambo yalionekana
Kwenu Moshi treni ilisismama kwa miaka 30,ndani ya miaka mitatu Magufuli karudisha treni,sasa hivi mnaenda kula x-mas kwa 13,000
Mnyonge mnyongeni,haki yake mpeni chuki zenu haziwezi kufuta legacy ya Magufuli kwa sababu inaonekana kwa macho
 
Kwani samia ametokana na serikali gani? Alikuwa anayahubiri ya nani? Amekabidhiwa ilani ipi? Amenadi sera zipi? MAJIBU YA HAYA MASWALI YATAKUFANYA UFIKIRI UPYA.
Hili ndilo jibu sahihi na uzi imeishia hapa.
 
Huyo PM ni bumunda tu na jiwe alimchukua kwakuwa hana akili wala hana uwezo wa kuuliza kitu ni kama jibwa koko linabweka pale linapokanyagwa mkia tu , kiufupi ni crap kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…