Rais Samia Suluhu akiendelea kumkumbatia Majaliwa na Baraza lake Serikali yake haitofanikiwa, Hawana jipya

Inasikitisha sana na haya ni matokeo ya watu kupumbazwa kuwa mwendazake alikuwa ni malaika.
Nyie ndiye ambao mpo kama fisi mkisubiri mkono udondoke. Kwani yeye hajui anachotakiwa kufanya? Huko ni kumkosea heshima napia ni kumweka Rais kwenye mazingira mabovu ya kushindwa kuwa huru kuamua kwaajili ya mustakabali wa taifa letu
 
Kuna sukuma gang ikiongozwa na PM inataka kumnyaua maza nini!!?

Ila hawa jamaa wapo chini chini lkn ni kama wana kanguvu flani hv aise sio wa kuwapuuza hata kidogo ni kuwala vichwa tuu
 

Na nikusaidie tu hakuna Watu Marafiki na ambao walikuwa 'Wakifarijiana' kwa Kutukanwa na hata Kudharauliwa na 'Jamaa' yenu kama Mama Samia na Kaka Kassim.

Kama mnategemea Rais Mama Samia 'atamtema' Waziri Mkuu Majaliwa mnapoteza bure muda wenu na mtaendelea Kununa tu.

Halafu kuupima 'ubaya' wa Waziri Mkuu Majaliwa kwa Kauli zake 'tata' tu dhidi ya Hayati alipokuwa Mgonjwa ni Upumbavu mkubwa.

Kiutendaji na hapa nisiwe Mnafiki bado sijayaona 'Mapungufu' hasa ya Waziri Mkuu Majaliwa hadi mseme aondolewe hapo alipo.

Kwa aina ya 'Upole' wa Mama ( Mheshimiwa Rais ) Samia tunahitaji Waziri Mkuu 'Mkali' na 'Mtendajj' hasa kama Kassim Majaliwa.

Mnalazimisha tu Waziri Mkuu 'ang'olewe' hivi mnajua Gharama zake hasa za Kuwatunza hawa Mawaziri Wakuu Wastaafu nchini?

Acheni Kukurupuka na tumieni Akili pia.
 
Reactions: Ame
fiki kaka sio unaongea tu
fikilia mzee
 
Nyie ndiye ambao mpo kama fisi mkisubiri mkono udondoke. Kwani yeye hajui anachotakiwa kufanya? Huko ni kumkosea heshima napia ni kumweka Rais kwenye mazingira mabovu ya kushindwa kuwa huru kuamua kwaajili ya mustakabali wa taifa letu
Tulisha waambia kuwa hilo kundi lenu lililo kuwa limeanza kumbeza mama yetu na kumtishia kuwa anabidi awabakishe watu wenu serikalini au ikulu kwa manufaa yenu hamtoweza.

Hilo kundi lenu halina tena meno kwa sasa ni kibogoyo tu na mama Samia sasa hivi ndiye amiri jeshi mkuu wa majeshi yetu hapa nchini.

Nadhani ulimsikia vema cdf pale chato siku ya mazishi ya mwendazake alivyo mhakikishia rais wetu.

Sasa kama nyie ni wanaume endeleeni na huo ushenzi wenu mmtajua kuwa hamjui.
 
Kwa bahati mbaya sana hatuna makundi tunayoyajua zaidi ya CCM na Rais wetu ndiye msimamizi wa ilani yao, hayo yako uliyonayo utaendelea kubaki nayo sisi tukisonga mbele...Bado kidogo utagundua Mh. Rais hana huo upumbavu wenu mnaotaka kuwaaminisha watanzania kuwa kuna kundi hili na lile...Sisi ni watanzania wenye chama chao CCM ambachokimeunda serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwakushinda uchaguzi wa kikatiba hapo 2020 na kwa sasa pamoja na Kamanda wetu JPM kulala kwa amani mkono wake wa Kuume Mama Samia Suluhu Hassan anaendeleza kazi yake...Ndiyo maana ya ile salamu mpya, upo?

Pole sana kwakuwa na wishful thinking, time will heal your ignorance and arrogance!
 
2025 ni patamu, wapinzani wakijipanfa vizuri watachukua nchi, endapo mama atatelekeza miradi ya JPM
 
Endelea ila jua kuwa hilo kundi lenu linajulikana na muda ndiyo utaamua hatima yenu
 
Unakuta watu wanajiongelesha na kujifanya wana maono sana wakati hawajui lolote kuhusu uongozi hata shuleni hawakuwahi kua viranja, halafu wanabetua mabega juu kumshauri rais eti atakwamishwa na waziri mkuu,

Pathetic.
 
Hahaha..mmeanza kuugua naona..yaan mtapasuka awamu hii..na bado..mnataka kumpangia mama nani wa kukaa nani wakutoka...
 
Mh. Rais anahitaji reshuffle kubwa sana, vinginevyo asije akatafuta mchawi ikifika 2025
 
Sawa, kila Rais huwa na maono yake, utawala wa Kikwete na Magufuli ulikuwa tofauti kabisa pamoja na kutumia ilani ileile ya CCM.
Mbona huelewi wa mwanamke! Ilani ya magufuli na ya kikwete ni tofaut..ndio mana kila uchanguzi mkuu baada ya 10yrs kunakuwa na ilani mpya..kwa case ya samia ni tofauti..ilani aliokuwa nayo magu ndio hiyo hiyo anaeitekeleza samia mana bado miaka 10 haijatimia..hivyo maono magu ndiyo hayo hayo ya samia mana walikuwa wanatekeleza ilani hiyo hiyo..
Watz wengi ni vilaza hawaelewi jinsi serikali inavyoendeshwaa..
Wewe pia ni kilaza tena sana.
Pole yakk
 
Rubish!
 
Daah aisee......najiuliza huyu Samia amekuja na chama Kipya au nayeye ni mmojawapo wa waliokuwepo Serikali iliyopita? Kuna jambo gani limebadilika kwenye Utawala zaidi ya kifo cha JPM? Sisiemu ni ile ile, Mpango ni yule yule ambaye yale yalikuwa yanafanyika na Tra nina imani zile task force alizijua vizuri kama Waziri....
Kumlaumu Majaliwa ni chuki binafsi kwake maana hata Samia wakati yuko Tanga alituambia kitu kilekile tu.......hata atakayemchagua kama unavyodhani ni sisiemu ileile tu.
 
Ilani ya chama siyo vision ya rais.
 
Nyie ndiye ambao mpo kama fisi mkisubiri mkono udondoke. Kwani yeye hajui anachotakiwa kufanya? Huko ni kumkosea heshima napia ni kumweka Rais kwenye mazingira mabovu ya kushindwa kuwa huru kuamua kwaajili ya mustakabali wa taifa letu
Wanaomuwekea rais mazingira magumu ni CCM wenyewe wakiwemo wabunge wanaomlazimisha afuate ya marehemu hata kama yalikuwa hayafai.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…