Rais Samia Suluhu amsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko

Rais Samia Suluhu amsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko

Ngoja sasa Watobolewe, hapo TPA kuna wajuaji wengi sana ila wapigaji watupu, kuna mzee alikuwa mzungumzaji sanaaa akapewa kitengo hapo TPA.....ghafla akawa bubu!!!
dawa ya hapo ni kusafisha wote.
Yule Mzee Mkinga alikuwa anapenda Sana kuhojiwa na vipindi vya mabishano ya hoja alikuwa anapambana shirika la meli Nasaco lilejeshwe.

Kuna sehemu alikuwa anagusa wazee, kuna muda alikuwa anatoa hoja hazipo kabisa technical ila akapewa shavu bodi ya wakurungezi saizi shavu dodo kelele hakuna tena mwezi uliopita nilikutana nae live.
 
Nashauri Kigogo ajengewe sanamu
Hii hapa
download%20(11).jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na Ripoti ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, ametoa agizo la kusimamishwa Mkurugenzi Mkuu wa Bandari(TPA) kutokana ubadhirifu mkubwa unaoikumba mamlaka hiyo.

Rais Samia Suluhu Hassan amesema haya

“Ripoti nimeona, nimeipitia na nimebaini ubadhirifu mkubwa uliofanywa pale bandari, hili suala mnatakiwa kushirikiana, nakuomba Takukuru jishughulishe pale, alipita Waziri Mkuu alilishughulikia.

“Waziri Mkuu aliunda kamati na wakafanya uchunguzi kidogo ambao yaliyotoka, hatua chache zilichukuliwa lakini imani yangu ni kwamba kama kuna ubadhirifu pale waliosimamishwa ni hawa wa chini huku, ninaomba mara moja nitoe agizo la kumsimamisha Mkurugenzi Mkuu wa Bandari halafu hatua zaidi ziendelee,”



Wanataka kumpima mama mara tatu kuu, kama Rais, kama mwanamke na kama mzanzibar. Lakini hawatafua dafu kwa huyu mama japo anaonekana mpole.
 
Pia miradi mingi ya maji kuna ubadhirifu wachunguze sana hasa hii miradi mikubwa kwa mfano Mradi wa Maji Arusha wa Billioni takribani 500

Value of money hakuna.

Kazi tu!...
Sio huo tu bali yote ifanyiwe uhakiki maana mingi haikupita bungeni.
 
Mama kachachamaa wapigaji wote na majizi yote awamu hii ya mama watakoma, big up Mheshimiwa.
Avunje baraza ateue upya na awaapishe upya yeye nwenyewe watakaomtii na kufuata maagizo yake. Kuna makabila ambayo yanadharau wanawake yatamsumbua sana kwenye serikali yake kama watakuwa wengi kwenye cabinet
 
Kuna makabila ambayo yanadharau wanawake yatamsumbua sana kwenye serikali yake kama watakuwa wengi kwenye cabinet
Yana vimelea kama vya yule Naibu wa TAMISEMI aliyetoka ng'ambo ileeeee!!!
 
PM alifanya lilikokuwa kwenye uwezo wake na alisema ambao wako juu ya uwezo wake anamwachia rais...PM asingeweza kumtumbua DG wa TPA wakati hajamteua yeye.
 
Kabla ya kumpa mtu wizara tuangalie na uwezo wake/ uzoefu. TAMISEMI ni wizara kubwa sana na ina wajanja wengi na wasomi pia. Lakini vilevile ni wizara yenye njaa hats deal la 5,000/= mtu haachi. Hii wizara inahitaji waziri mwenye uzoefu mkubwa na ufuatiliaji wa hali ya juu sio kurukaruka.
Yaani ukiona clip ya Jofu wakati JPM ametembelea soko la Kisutu hauwezi kudhani huyu ni waziri
 
Kama siyo kujuana, mkurugenzi wa Bandari Deusdedit Kakoko alikuwa atumbuliwe mwaka 2015 baada ya kuibuka kashfa za mita za mafuta na baadaye magari polisi. Ila kwa vile alikuwa mshikaji wa jiwe, alisepa kama alivyosepa Lugumi.
 
Back
Top Bottom