Rais Samia Suluhu ana emotional intelligence, utulivu wa hali ya juu

Rais Samia Suluhu ana emotional intelligence, utulivu wa hali ya juu

Halafu mama ajue huko CCM kuna watu walikuwa wanamsubiri ateleze!! Muda huu wanachekea tumboni tu wakiwa mbele yake, lakini wakiwa wenyewe wanafanya sherehe!! Wakiwa mbele yake "wanaunga" mkono mkataba wa bandari kinafiki!! Kama mama anadhani ana watu huko labda ni ile aina ya kina Nape, tu lakini wale vigogo wenyewe hawako pamoja naye!! Atalazimika kunyoosha mikono mwenyewe!!
 
Kumsifia baba mwenye nyumba kwa kukaa kimya wakati watu wa nyumbani kwake wanampigia kelele mwizi aliyekwapua ng'ombe wa familia nao ni uchizi wa aina yake!!
 
Niliamuwa kunyamaza kimya, na naendelea kunyamaza kimya. - Mama Samia.
 
Wacha nikuambie kitu kuwa huo sio utulivu bali kiburi kwa anao waongoza kiongozi wa umma kwa nafasi yake huwezi kuwa kimya katika ajenda kubwa ya kitaifa bila kuijibia kwa maelezo ya kutosha na ya kueleweka kwa watu wote unao ongoza.

Taifa hili lingekuwa linatumia parliamentary democracy mpaka sasa maza angekuwa amekwisha wajibishwa na bunge haraka sana.

Hii presidential system ndio inampa kiburi ambacho wewe unaiita utulivu kwa sababu nafasi yake ipo safe katika kuwajibishwa ni ngumu sana hilo kutokea.

Maza hana utulivu bali ana kiburi kwa anao waongoza ila hana kiburi kwa walio mpa hayo madaraka( ukiielewa hii sentensi ya mwisho utakuwa umekua kimwili na kiakili usipo ielewa wewe bado dogo)
Pascal Mayalla una maoni yoyote hapa brother?

Mimi Kwa maoni yangu, huyu ndugu So special ndiye katoa jibu sahihi la hoja zote za mleta mada ndugu Robert Heriel Mtibeli.

Na nakubaliana kabisa na So special. Huu sio utulivu wa kawaida. Huu ni utulivu wa kupigwa na bumbuwazi ili ibilisi afanye kazi yake. Ni kiburi cha hovyo...

Kuna mambo ya kukaa kimya kama jibu na shida ikaisha. Lakini kuna mambo ambayo ni lazima kiongozi awe very pro - active, firm and intelligently aggressive bila kusahau kutumia hekima na busara katika kila hatua ya maamuzi ili kuleta usawazisho wa haraka ktk jamii iliyo ktk mgongano wa mawazo kabla ya uharibifu kutokea.

Kwa hili, bila shaka Kuna watakaosema, ooh mbona Hayati Magufuli alikuwa very aggressive na mkamsema sana..

Ni kweli, Magufuli alikuwa very aggressive lakini bila busara wala hekima. Hii ndiyo ilikuwa shida yake kubwa yule Mzee...
 
Waarabu wamemshika pabaya!! Hawana adabu wale!! Lazima watamwaibisha!!
Halafu hawana huruma. Jana BBC imetoa habari kuwa maaskari wa Saudi Arabia wakiwakuta wahamiaji haramu mpakani kutoka Afrika wanaokwenda kutafuta maisha hawana salia mtume, bali huwapiga risasi hapo hapo na kuwaua. Wameuawa wengi sana na wanawazika kwa kificho. Mijitu mikatili kweli kweli hii.
FaizaFoxy

 
Naunga mkono hoja yako kwani ile kauli yake ya kuwa amechagua kukaa kimya na akamalizia kwa kusema hakuna mwenye ubavu ....... anamaanisha kuwa semeni yote mmalize lakini hamna cha kunifanya niliyoamua nimeamua na mkataba upo na utakuwepo kama ulivyo,hizo ni kelele za mlango tu hazimnyimi usingizi mwenye nyumba. Hicho ni kiburi cha kiwango cha juu sana.
Mtu amedakwa kuweupe hana pa kutokea uliktaka ajibu nini ,mkataba amesain youe hana wa kumsingizia
 
Mengine unamsingizia hasa hayo ya kushindwa makesi.

Wapi Watu wanafanya watakavyo Mkuu?
Mnataka Ile ya kila kitu Rais akitolee ufafanuzi kama Hana Wasaidizi wake?
Au unataka Ile ya Rais kudhalilisha Wasaidizi wake hadharani ili aonekane mchapakazi ilhali hafuati sheria kuwawajibisha hao anaowadhalilisha hadharani?

Hutaki kila mmoja abaki kwenye nafasi yake?

Kama ishu ni kusainishana mikataba ya kimangungo, hizi kesi tunazoshindwa sasa hivi Huyo Samia alikuwa Rais?

Simtetei Rais Ila najaribu kuonyesha kuwa kama taifa tunatatizo la kimfumo, kisheria na kimaadili
Tumefika hapa kwa kuonea aibu kama unavyosema ,kutowajibishana mtu anaiba hapa anapelekwa Pele, lazima wizi utaongezekaz tu
 
Unamuonea....

Hivi unaifurahiyaje "OVER INVOICES"?!!

Mathalani manunuzi yale ya ndege kutoka dola milioni 37 mpaka dola milioni 87?!!

Hili halikuumi?!!

Haya ni maji ya mvua kutoka mawinguni ama fedha zetu tunazokatwa tunaponunua SIGARA na SMART GIN?!!! [emoji15][emoji1787][emoji1787]

Mh.Samia anastahili pongezi.....

#SiempreJMT[emoji120]
Sawa Samia anastahili pongezi. Je nani hastahili pongezi na kwa sababu zipi ? Hapo nd msingi wa hoja yangu ilipoanzia na nilikuwa namjibu mtoa mada kwa rejea kuntu.
 
Akili kubwa iliyo barikiwa utulivu mkubwa.
Ni binaadamu wachache walio barikiwa hivyo.
Mungu azidi kumlinda Rais wetu.
 
Tumefika hapa kwa kuonea aibu kama unavyosema ,kutowajibishana mtu anaiba hapa anapelekwa Pele, lazima wizi utaongezekaz tu

Wizi lazima uwepo ikiwa kuna Watu hawashtakiwi.
Katiba iwekwe Sawa. Yeyote ashtakiwe hapo ndio tutapata PA kuanzia
 
Utulivu wa kuagiza wanaopingwa washikiliwe bila kwenda mahakaman .utulivu ni kutoendana na mood ya mjadala ili kujipa muda kuamua vizuri.ukimya ni kukosa cha kujibu juu ya hoja 7 za TEC .MAMA Samia ni mkimya sio mtulivu
 
Utulivu wa kuagiza wanaopingwa washikiliwe bila kwenda mahakaman .utulivu ni kutoendana na mood ya mjadala ili kujipa muda kuamua vizuri.ukimya ni kukosa cha kujibu juu ya hoja 7 za TEC .MAMA Samia ni mkimya sio mtulivu

Ukimya ni sehemu ya utulivu Mkuu.
Ila ukimya sio utulivu
 
Naunga mkono hoja yako kwani ile kauli yake ya kuwa amechagua kukaa kimya na akamalizia kwa kusema hakuna mwenye ubavu ....... anamaanisha kuwa semeni yote mmalize lakini hamna cha kunifanya niliyoamua nimeamua na mkataba upo na utakuwepo kama ulivyo,hizo ni kelele za mlango tu hazimnyimi usingizi mwenye nyumba. Hicho ni kiburi cha kiwango cha juu sana.
This should be laminated then thread closed.

Mleta mada anachanganya emotional intelligence na arrogance. Kwa circumstance ya hili sakata, na hiyo statement yake ni wazi ni mjivuni mwingi wa kiburi.
 
Ukimya ni sehemu ya utulivu Mkuu.
Ila ukimya sio utulivu
Sawa mama ni mkimya kwa kuwa hajibu hoja (hana majibu) ila sio mtulivu kwa kuwa kashatumia mabavu kuvunja katiba na quran kwa kulaza watoto wa wenzie wenye mama zao kama Rashid ndani kihuni
 
Kumbe watu tunatofautiana sana katika kupima uongozi wa Rais!

Mimi naona Rais hajakaa kimya hata kidogo katika suala hili la Bandari, anaongea sana, tena kila siku kupitia wapambe wake pamoja na walamba viatu ama machawa.

Kitendo cha kukamatwa watu wanaopinga mkataba mbovu na kupewa kesi za mchongo, Mawaziri kutoka hadharani na kutoa vitisho kwa mambo yanayoruhusiwa kisheria na kikatiba, kina Wasira kuacha shughuli zao na kupanda majukwaani na kuanza kumwaga fitina, Kikwete kupanda mimbari za kidini na kupiga ngebe zake, kauli zote hizo ndiye yeye Samia kaziongea, ni zake na ndiyo msimamo wake huo.

Hakuna mtu anayeweza kukurupuka kutoa mambo kichwani bila ya kuwasiliana na boss wake kwanza, hayupo.

Ninachoweza kumtetea Rais ni kwenye jambo la ubambikiwaji wa kesi za kina Slaa, hilo laweza kuwa limeasisiwa na Ndumbaro pamoja na Wambura kwa minajiri ya kumfurahisha Rais kujionesha kuwa ni wachapa kazi, ndiyo maana kalikemea.

Lingekuwa limetoka kwake, kina Slaa wangelikuwa bado wanasota Ndani

Lakini hata hivyo, kina Ndumbaro hao si wanaamka na kupeana "hi" na Rais kila siku, wanaweza kutoka nje ya mstari wake kweli?

Nilichokuwa nakitegemea sasa Rais afanye conclusion ya jambo hili ambao ndiyo utakuwa ni msimamo wa Serikali.

Hakuna wazo jipya ama ushauri mpya utakaotolewa zaidi ya haya yaliyokwishatolewa na wananchi kamchanganyikeni kwa sasa.

Ujue nini, kuendelea kulikalia kimya jambo hili kwa sifa za ukimya ni sawa na kubet!
Isee hii tafakuri ni kama ume copy na paste toka mawazoni mwangu.
Nilijadili hili jana kijiwe cha soga. Wakapiga kimya watetezi wake wakabaki ku suffocate.
 
Sawa mama ni mkimya kwa kuwa hajibu hoja (hana majibu) ila sio mtulivu kwa kuwa kashatumia mabavu kuvunja katiba na quran kwa kulaza watoto wa wenzie wenye mama zao kama Rashid ndani kihuni

Unaweza kuwa Sawa kuwa Hana utulivu Kwa 100% ambalo ni Jambo la kawaida.
Ila hakosi 60%

Ukilinganisha na waliomtangulia.
Ngoja tusubiri amalize miaka yake tutakuja kuhitimisha.
 
Kukaa kimya wakati unatakiwa kuzungumza siyo hekima hata kidogo!! Kukaa kimya wakati ni wewe peke yako unayetakiwa kutoa suluhisho siyo hekima hata kidogo! Ni woga! ni kukwepa jukumu ambalo ni wewe peke yako unasubiriwa ulitoe!! Kukaa kimya wakati suluhisho la haraka linatakiwa ni kutokujiamini!! Tukubali kuusema ukweli hata kama tunataka nafasi za uteuzi!!! Mama tunampenda lakini hapa amefeli!! Ameamua kuyaacha mambo yaende hivyo hivyo liwalo na liwe!! Historia itamhukumu!!
Nakumbuka mwanzoni mwa mwaka 1990+ Zanzibar ilikuwa inataka kujiunga OIC binafsi, pamoja na kuwa yenyewe ni sehemu ya TANZANIA. Wakati huo, Rais wetu alikuwa ni M- Zanzibari, Ali Hassan Mwinyi.
Huku Bara, Watu wengi walipinga mpango huo. Wabunge Bungeni, nako wakaja juu. Rais Mwinyi, akaonyesha BUSARA yake, ya KUKAA KIMYA tu! Asasi mbali mbali zikapiga kelele, na hasa ukizingatia kuwa hiyo OIC ikitafsiriwa kuwa ni ya kidini dini, Kiislamu! Rais Mwinyi, akawa anapiga kimya tu!
Wakaibuka akina Njelu Kasaka na G55 yao, wakadai, kama ni hivyo, basi nasi tuifufue Tanganyika yetu, kwani wenzao Zenji wameshajionyesha ni NCHI, na wanaweza wakajiamulia mambo yao hata ya KIMATAIFA bila kuihusisha TANGANYIKA. Rais Mwinyi, kimya!
Mchakato wa KUIFUFUA TANGANYIKA ukaanza! Ukapelekwa Bungeni, Spika Pius Msekwa, Waziri Mkuu Malecela, Katibu Mkuu CCM Horace Kolimba. Rais Mwinyi, KIMYAA!
Watu wote tukajua, sasa Tanganyika inafufuka! Wakati wote huo, Mwalimu Nyerere yupo, anaangalia tu! Alivyoona hali imekuwa mbaya, na kutambua kuwa ule UKIMYA wa Mwinyi, si BUSARA, bali ni kushindwa kuliendesha gari. Akaingilia kati. Akamshauri aizime ile hali. Lakini Mwinyi, hakujua aanzie wapi! (Kwa wanao kumbuka, Nyerere alidai Mwinyi alikuwa DHAIFU, akamtungia na kitabu). Rais Mwinyi, akaomba Mwalimu, amsaidie, kwani pamoja na kuwa yeye alikuwa ndiye Rais, lakini alikuwa hajui atalimalizaje!
Mwalimu akamwambia, kwanza FUKUZA Malecela kama Waziri Mkuu, pia, FURUSHA Horace Kolimba kama Katibu Mkuu wa CCM. Kwani hawa hawakukushauri vizuri, mpaka hali kufikia hapo ilipokuwa. Pia, ZANZIBAR, IACHANE NA MPANGO WA KUJIUNGA NA OIC!
Yakafanyika hayo! Pia, tukaahidiwa kuwa, TANZANIA itaangalia KUJIUNGA kama Nchi, sio upande fulani. IKAWA IMETOKA HIYOOO! Mliokuwepo, mnakumbuka!
Lile suala la G55 na kuitaka TANGANYIKA, Mwalimu alilimaliza, kama KUMCHINJA NG'OMBE BILA KUTOKA DAMU! Alienda Bungeni, na kuhutubia Wabunge. Na wakati ule, Wabunge wote walikuwa ni wa CCM. Akawaambia akina Njelu Kasaka kuwa, sera ya CCM, Tanzania ni ya serikali mbili. Kama kuna mtu hataki hivyo, ahame chama, kwani vipo vyama vyenye kuamini Serikali tatu, nne nk. Nendeni huko, tunaoamini serikali mbili mtuachie CCM yetu!
Huo ndiyo ukawa mwisho wa G55.
Sasa, hili la BANDARI, naona linafanana! Rais, ni Mzenji! Pia, upande mmoja wa Muungano hauhusiki! Kelele zimekuwa nyingi kama wakati ule. Rais, yupo kimyaaaa! Na tunamsifu! Sidhani kama kukaa kimya ni vizuri! Kwa sasa, tumeona kila kukicha, watu wanaibuka wapya, tena wengine wanaongea maneno ya hatari, chuki, kutugawa!
Leo hii, Mwalimu hayupo. Inawezekana washauri waliopo karibu na Rais, sio wazuri. Wao, wapo kwa ajili ya masirahi yao. Wapo wanaotaka AHARIBIKIWE! Yupo kwenye boti ziwani. Ziwa limechafuka. Mizigo mingi botini. Usalama wa abiria na boti lenyewe, ni kupunguza uzito. Kama anaamini atafika nchi kavu salama bila kupunguza uzito kwa kutupa majini baadhi ya mizigo, sawa! Kinyume cha hivyo, asione aibu. Wala haitakuwa ni kushindwa. TUACHANE NALO!
Ila, inabidi, ZA KIKWETE, ZETU HUKU MITANDAONI,ZA WARAKA NK ACHANGANYE NA ZAKE!
 
Back
Top Bottom