Rais Samia Suluhu anakwenda kuzoa kura zote uchaguzi ujao

Rais Samia Suluhu anakwenda kuzoa kura zote uchaguzi ujao

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu wahenga walishasema "nyota njema huonekana asubuhi", kwa kazi nzuri na ya kutukuka anayoifanya Mh. Rais katika kuijenga Tanzania mpya, ni dhahiri uchaguzi ujao utakuwa mwepesi Sana kwake kuweza kupita. Kwa Sasa hakuna mpinzani yeyote mwenye mwelekeo wala nguvu ya kuweza kuja kumtikisa Mh. Rais uchaguzi ujao.

Hii inatokana na ukweli kwamba upinzani ulikuwa unategemea makosa ya serikali ili upate ajenda na kujijenga, lakini Mama Samia Suluhu Hassani, punde tu baada ya kuapishwa ni Kama alikuwa analijua hilo. Kwa sasa ndani ya mwaka mmoja na miez kadhaa ameziba mianya yote na kuunyima upinzani ajenda na sera kwa serikali yake, kwa hiyo sasa hivi wapinzani wanashindwa wawaeleze nini wananchi, maana kila kitu kimeguswa na kufanyiwa kazi na Mh. Rais.

Ndio maana unaona wapinzani wengi sana wanamuunga mkono Mh. Rais kwa kazi kubwa anazofanya katika kuijenga nchi yetu. Hakika siasa ni sayansi na mama ameumaliza upinzani kisayansi kwa kufanya kazi wanayohitaji wananchi. Maana wananchi walichokuwa wanahitaji ni mtumishi wao, na kwa sasa Mama Samia Suluhu Hassani amepatikana, hivyo hawana muda tena na habari za vurugu, maandamano, makelele wala matusi kwa serikali.

Mama anaupiga mwingi, ni Mama hadi 2030 hapo ndiyo tutaanza mazungumzo baada ya kufika kituo hicho. Kikubwa ni maombi yetu kwa Mwenyezi Mungu ili amlinde na kumpigania Mh. Rais wetu, ampatie na kumjalia uzima na afya njema.
 
Hata Magufuli ilisemwa ameleta maendeleo sana hivyo atachukua kura nyingi, matokeo yake ndio tukashuhudia uchaguzi wa kihayawani kuliko wakati mwingine wowote.

Kwa bahati mbaya uchaguzi wa 2025 utakuwa na wapiga kura wachache sana, kwani kwa sasa box la kura limepuuzwa rasmi.

Hivyo mwambie mama wala asipoteze muda wake kupanga wizi wa kura uweje, kwani watu wengi hawatakuwa na muda na huo ushenzi uitwao uchaguzi. Machafuko tu ndio yatafanya tupate katiba bora.
 
Umeishia darasa la ngapi kijana
Ningependaa wewe ndio unieleze Elimu yako ili nijuwe Nani alikufundisha kuwa ukishindwa na kuishiwa hoja Basi uwe unatukana matusi tu, hata hivyo nimekusamehe na siwezi nikakutukana maana kwangu Namheshimu kila mtu hata ninayetofautiaana Naye bado nitamjibu kwa hekima na busara tu

Kwanguu Mimi utu wa mtu Ni Jambo la msingi na ndicho nimefundishwa hivyo

Hata Rais wetu Ndio maana unaona akikaa hata na wapinzani wake wa kisiasa ili kuzungumza na kukubaliana yanayokubalika na Kuendelea na mazungumzo kwa Yale yanayohitaji mjadala mrefu na maridhiano ya pamoja,

Hata wewe nakushauri kufuata mkondo huu wa kuvumiliana na kukosoana kwa hekima na busara,
 
Nyie ndio mnafanya watanzania wote tunaonekane wajinga...
Ukweli ndio huo Wala hutaonekana Ni mjinga popote pale kwa Sasa ukisikika unamuunga mkono mh Rais, maana watanzania wanaridhishwa na utendaji kazi wa mh Rais wetu unaogusa maisha ya kila mmoja wetu, niambie Ni wapi unapohisi mh Rais anafanya kazi kwa manufaa yake mwenyewe
 
Acha ujinga.
Waweke washindani kama.ilivyokuwa Kenya tuwaone.Tatizo lanwaTanzania wengi hasa viongozi ni waganga njaa ndio maana imebakia kusifia. What the H..l.!!
Hapana ndugu yangu, Naomba uelewe kuwa siyo tume inayokupigia kura, Bali wananchi ndio wanaokupigia kura, utapigiwa kura endapo una Sera na ajenda zinazo gusa maisha ya watu,

Kwa Sasa wapinzani na upinzani umepokwa hoja zote kwa mh Rais kufanyia kazi Kero mbalimbali zinazokuwa zinawatesa wananchi, watu wanaona juhudi za mh Rais katika kuboresha maisha yao, watu wanaona Rais anavyokosa hata muda wa kupumzika ili watanzania wapate maji Safi na salama, Elimu Bora, umeme wa uhakika na Bei nafuu, huduma za Afya zilizo Bora

Sasa utawaambia Nini watanzania juu ya mama Samia wakakuelewa kwa Sasa, utaanzaje kuwakusanya watanzania wamzomee Rais wao ambao kwao Ni mkombozi katika maisha yao

Watanzania wanaona namna mh Rais alivyo msikivu, Namna alivyo na Roho ya huruma Jambo linalomnyima usingizi akiona Kuna watu wanahitaji maji au kituo Cha Afya eneo fulani, Ndio maana unaona anavyopambana kuhakikisha kila Senti inayopatikana inakwenda kupunguza kero kwa wananchi
 
Ndugu zangu wahenga walishasema Nyota njema huonekana asubuhi, kwa kazi nzuri na ya kutukuka anayoifanya mh Rais katika kuijenga Tanzania mpya, Ni dhahiri uchaguzi ujao utakuwa mwepesi Sana kwake kuweza kupita.

Kwa Sasa hakuna mpinzani yeyote mwenye mwelekeo Wala nguvu ya kuweza kuja kumtikisa mh Rais uchaguzi ujao.

Hii inatokana na ukweli kwamba upinzani ulikuwa unategemea makosa ya serikali ili upate ajenda na kujijenga, lakini Mama Samia suluhu Hassani, punde tu baada ya kuapishwa Ni Kama alikuwa analijuwa Hilo.

Kwa sasa ndani ya mwaka mmoja na miez kadhaa ameziba mianya yote na kuunyima upinzani ajenda na Sera kwa serikali yake, kwa hiyo saiz wapinzani wanashindwa wawaeleze Nini wananchi maana kila kitu kimeguswa na kufanyiwa kazi na mh Rais.

Ndio maana unaona wapinzani wengi Sana wanamuunga mkono mh Rais kwa kazi kubwa anazofanya katika kuijenga nchi yetu.

Hakika siasa Ni sayansi na mama ameumaliza upinzani kisayansi kwa kufanya kazi wanayohitaji wananchi, maana wananchi walichokuwa wanahitaji Ni mtumishi wao na kwa Sasa mama Samia suluhu Hassani amepatikana, hivyo hawana habari tena na habari za vurugu Wala maandamano Wala makelele Wala matusi kwa serikali.

Mama anaupiga mwingi, Ni mama Hadi 2030 Ndio tutaanza mazungumzo baada ya kufika kituo hicho.

Kikubwa ni maombi yetu kwa Mwenyezi Mungu ili amlinde na kumpigania mh Rais wetu, ampatie na kumjalia uzima na Afya njema.
Kwa Takwimu hizi hapa unategemea atashindana na nani akamshinda?

Someni wenyewe,hi ni afya tuu bado maji,kilimo,barabara,elimu, biashara nk nk👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220816-203211.png
    Screenshot_20220816-203211.png
    87.3 KB · Views: 8
Eti "atapata kura zote", kauli za namna hii hutolewa na watu wenye low IQ, walamba miguu, was wasubiri teuzi

Tuna safari ndefu kama tunataka tufike nchi tenye demokrasia walau kama hapo Kenya tu.

Wapi uliona mchezaji anateua refa, kamisaa, uwanja wa kuchezea, mpira halafu anapambanishwa na mwenzake, only in tz..nchi ya hovyo hii.
 
Kwa Takwimu hizi hapa unategemea atashindana na nani akamshinda?

Someni wenyewe,hi ni afya tuu bado maji,kilimo,barabara,elimu, biashara nk nk👇
Hakuna wa kushindana na mh Rais Samia suluhu Hassani kwa Sasa, kaudhoofisha Upinzani kwa kuchapa kazi bila kupumzika, kwa Sasa uungwaji mkono wa watanzania kwa mh Rais wetu Ni mkubwa Sanaa
 
Hakuna wa kushindana na mh Rais Samia suluhu Hassani kwa Sasa, kaudhoofisha Upinzani kwa kuchapa kazi bila kupumzika, kwa Sasa uungwaji mkono wa watanzania kwa mh Rais wetu Ni mkubwa Sanaa
Hata wale haters saizi wanayetemeka..

Mbarawa alisema mwezi wa Tisa magari yataanza kupita Wami itakuwa hivyo ujenzi uko hatua za mwisho 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220816-201819.png
    Screenshot_20220816-201819.png
    149.7 KB · Views: 9
  • Screenshot_20220816-201912.png
    Screenshot_20220816-201912.png
    216.4 KB · Views: 7
Eti "atapata kura zote", kauli za namna hii hutolewa na watu wenye low IQ, walamba miguu, was wasubiri teuzi

Tuna safari ndefu kama tunataka tufike nchi tenye demokrasia walau kama hapo Kenya tu.

Wapi uliona mchezaji anateua refa, kamisaa, uwanja wa kuchezea, mpira halafu anapambanishwa na mwenzake, only in tz..nchi ya hovyo hii.
Hapo Kenya unapopasifia kwani hujasikia Raila Odinga anailalamikia Tume au hujasikia akijitangaza kuwa Ni mshindi hata kabla ya matokeo, Sasa unataka kusema Nini tuelewe vizuri
 
Mama hana shida ila akamate majizi wanaokula hela za umma na kuweka katiba nzuri tuu
 
Back
Top Bottom