Rais Samia Suluhu ateua Wabunge wapya watatu na kuteua Baraza la Mawaziri

Rais Samia Suluhu ateua Wabunge wapya watatu na kuteua Baraza la Mawaziri

Alisikika mlevi mmoja hapa bar
bigest mistake ni kumludisha mwigulu wizara ya fedha mara mia angemleta sada mkuya mwigulu anatafuta urais na ndoto zake zinaenda kutimia atamsumbua sana mama
 
Ina maana bashiru atakuwa raia wa kawaida? Baada ya kutolewa chamani, sasa hata serekalini katolewa!??
Nilisikia jamaa ni muizi sanaaa!!
Ameteuliwa kuwa mbunge...lakin kwa sasa ana inshu...yaan yuko reserve tuu[emoji41]
 
Na timu Veronica France mpoo! Mbeba maono wenu kaambulia ubunge wa viti maalum kama akina Mzee Mdee vile,masikini kala mshahara mmoja tu wa u KMK.
Kama mama angekua hamtaki angemuacha tu hata viti maalum asingepewa,kwani nani wa kumzuia.
Ubunge inamaana akihitaji kumtumia hatokua nae mbali iwe wizara ama nafasi nyingine yeyote ile.
Kwani kuna mtu alitarajia Mwigulu atateuliwa wizara ya fedha?
Kwa macho ya kawaida legacy ya Magufuli bado ipo.
 
^Umuhimu uliobaki wa makabila sasa hivi ni kutambika tu, hamna kingine. Mnaongelea habari za makabila kwani mnataka kutambika!??? ~ JK Nyerere
Baada ya ukabila utauliza mbona hakuna wa dini yetu,kwani akiwa mchaga ndio atakulishia watoto wako?
 
CCM ni ile ile ! Unafiki kwa kwenda mbele Jiwe aliikanyaga katiba awezavyo hadi kumuweka Kakurwa kuidhinisha mipango yake leo hii katolewa kapoozwa kwa kiubunge cha kinafki pia!
 
Wabunge wapya walioteuliwa kuwa wabunge ni pamoja na Aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Bashiru Kakurwa Ali, Mbarouk Nassor Mbarouk na Liberata Mulamula.

Rais Samia Suluhu akitangaza Baraza la Mawaziri amesema...

''Kuondoka kwa Mpango kumefanya nifanye mabadiliko kidogo kwenye Baraza la Mawaziri na nitatangaza hapahapa zege halilali''

Baadhi ya Wizara zimefanyiwa Mabadiliko na nyingine zimebaki kama zilivyokuwa.

MAJINA YA MAWAZIRI WANAOUNDA BARAZA LA MAWAZIRI

Ummy Mwalimu - Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI

Mohammed Mchengelwa - Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Selemani Jafo - Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais

Geoffrey Mwambe - Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji

Dkt. Mwigulu Nchemba - Waziri wa Fedha na Mipango

Profesa Palamagamba Kabudi - Waziri Wizara ya Katiba na Sheria

Balozi Liberata Mulamula - Waziri wa Mambo ya Nje

Prof Kitila Mkumbo - Waziri wa Viwanda na Biashara
Rais ana haki kumuondoa Jaffo TAMISEMI,alishindwa kabisa kukomesha upigaji kwenye Halimashauri.Ila Umi naye sijui kama ataweza,TAMISEMI ilihitaji mtu very strong,sioni quality hii kwa Umi.Nchemba ni wazi viatu vya Mpango havimtoshi,nadhani tulihitaji a better person,hii ni Wizara nyeti sana.
 
Huu mziki wa Umy Mwalimu na Dr Dorothy Gwajima huko afya.... Maana Dr Gwajima alijisikia sana akiwa naibu KM -TAMISEMI, Afya...alijiona mkubwa kuliko waziri wa Afya...Umy Mwalimu.
 
Rais ana haki kumuondoa Jaffo TAMISEMI,alishindwa kabisa kukomesha upigaji kwenye Halimashauri.Ila Umi naye sijui kama ataweza.Nchemba ni wazi viatu vya Mpango havimtoshi,nadhani tulihitaji a better person,hii ni Wizara nyeti sana.
Wizara ya Fedha imetupwa jalalani.

Huwezi ukateua mwehu awe msimamizi wa sera za uchumi.
 
Huyu Mama Ana Kusudi Sana Nadhani Hataki Kufanya Kazi Na Mwalimu Wangu Bashiru, Kamteua Kuwa Mbunge Halafu Kamwacha Domant Tu.. Daaaah Dharau Hizi.
Dharau vipi alizaliwa ikulu?aache mambo yake arudi kufundisha na vp kuhusu nafasi yake ya katibu mkuu CCM kama una uelewa tujuzane tafadhali
 
Mama kaniharibia Sana ule utamu wa kuniletea Katanga! Mwigulu, Jaffo na Kabudi wa kazi gani Tena? Na kule afya mbona umewaacha wale comedians? Mama hebu funga macho utafakari kwa kina juu ya hao pamoja na pm na ikikupendeza piga chini hao uanze upya na timu mpya yenye ueledi na adabu ya kazi wasioiwazia nafasi yako ya urais mwaka 2025!
 
Back
Top Bottom