Rais Samia Suluhu Hassan afanya uteuzi wa mabalozi; wamo Hoyce Temu na Togolani Mavura

Huyu mama Liberatha ni mtu mmoja smart sana. Niliposikia tu amekuwa waziri nikaanza kusoma mahojiano yake huko Google na taasisi za kimataifa. She's very smart upstairs.
Naam, kwenye siasa za Maziwa Makuu na Utatuzi wa Migogoro nadhani kwasasa yeye ni moja kati ya wataalamu ambao wana uzoefu na uelewa mkubwa hapa nchini. Kibarua kikubwa ambacho anacho kwasasa ni kuhakikisha anatengeneza kizazi kipya cha wataalamu, maana kile cha zamani ndiyo kinaondoka hivyo.

Hili la kuwateua vijana wengi kutoka Foreign Affairs limenigusa mno, they all have institutional memory. Naamini kabisa wakiendelea hivi tutafika sehemu nzuri,.....
 
Kweli!

Manake hata humu ukimsifia kiongozi wa nchi unaambiwa eti unatafuta uteuzi!

Mimi niliambiwa mara kadhaa eti natafuta teuzi toka kwa Magufuli!

Hakunijua na sikumjua! Aje tu aniteue β€˜Nyani Ngabu’ toka JF kisa nimemsifia au nimemuunga mkono kwenye jambo?

Akili za watu wengine bana!!
 
Mkuu watu walitoa mapovu Bashiru alipoteuliwa kuwa balozi na hadi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi haya sasa huyu Hoyce Temu nae kawa balozi nasubiri mapovu na sheria zinavyosema kama walivyomnanga mwendazake kwa Bashiru
Bashiru alinangwa kwa kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi. Uteuzi wa kuwa Balozi hauna shida. Mtu yeyote anaweza kuwa Balozi.

Amandla...
 
Kuna wanaoweka mpaka namba zao za simu.

Amandla..
 
Hadi Hoyce Temu!
Wengi kwenye hiyo list ni wahaya mmmmm au sababu waziri Wa mambo ya nje ni muhaya?

Anyway kanza yuko vizuri mno ila Ee Mungu mrehemu mtoto alikuwa vizuri kiakili kiafya na kila eneo yeyote aliyehusika kumharibia afya yake mtoto Wa watu Mungu anamuona .Na alaaniwe yeye na kizazi chake mbwa mkubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…