Rais Samia Suluhu Hassan ampa onyo Waziri wa OR-TAMISEMI, Selemani Jafo

Rais Samia Suluhu Hassan ampa onyo Waziri wa OR-TAMISEMI, Selemani Jafo

Pesa za miradi ya EP4R zinapigwa hadi huruma. Wahandisi wa halmashauri kwa kushirikiana na maafisa elimu pamoja na wakuu wa shule wanaandika calculations za kufoji kuhalalisha upigaji

Just imagine tofali moja la block unaambiwa limenunuliwa 5000, sink la choo haya yanayouzwa kati ya 15000-20000 unaambiwa limenunuliwa kwa 87000 mara mfuko wa cement umenunuliwa kwa 45000. Si upuuzi huuu?

Jaffo resign kwa hiari yako usingoje kutumbuliwa
 
Mhurumieni jafo Ana wizara 5, maana wake wanne ni wizara nne na tamisemi ya tano.
Kama cheo ndio kilimfanya aoe wake wanne ajiandae na maisha ya useja tuu sasa
Cheo ni dhamana.... cheo ni koti la kuazima
 
Wewe unadhani waziri atawachukulia hatua gani maDED? Yeye sio mamlaka ya uteuzi au utenguzi wao, hiyo mamlaka anayo Rais. Jafo hawezi hata kuwaweka ndani siku moja mbili. Hiyo mamlaka wamepewa wakuu wa mikoa. Rejea alivyokuwa analalamika akiwa geita juu ya wale maafisa ardhi na mkurugenzi waliofanya madudu. Ni Mongela RC wa mwanza ndio alikuja kusema hiyo mamlaka yeye anayo na akawaweka ndani.yeye Jafo sana sana atakachoweza kufanya ni kuwabwekea tu na kuwashitaki kwa mamlaka iliyowateua, si zaidi ya hapo. lazima wamvimbie na kumpuuza.
Ana wakati mgumu sana!
Najua hana cha kuwafanya lakini hata kumwambia Boss aliyewateua napo alishindwa? Jaffo mna mkingia kifua tuu lakn niwambie hata kama atapewa miaka 100 kwenye hiyo wizara hakuna mabadiliko yoyote atakayofanya maana uwezo wake wa kufikiri na kutenda ndio umeishia hapo.
 
Nashauri kuwe na zone officer ambae atamonitor kila mradi akishirikiana na pccb na cag .Jafo acheze na hao mabosi kuliko wakurugenzi wezi.
Je wakuu wa mikoa wanafanya nini kwa upigaji huu?
 
Hakupandishwa kwa sababu ya utendaji kazi bali ni kwa sababu ya ushikaji ili waendelee kufichiana siri.
Kumbuka Jafo alikuwa naibu waziri baadae Magu akampandisha. Hiyo inaonesha Jafo ni muwajibikaji ila hawa wa chini ake ndo wanamwangusha.
 
Nimeshtushwa na tuhuma za rushwa za TAMISEMI, niliwahi kushauri na Sasa nashauri Mhe. Rais ajitenge na TAMISEMI amwachie Waziri Mkuu ili iwe raisi kwake kuimulika. Ikiwa chini yake ikatuhumiwa ametuhumiwa na nivigumu kumwajibisha maana baadhi ya nyaraka zao anakuwa kazipitisha yeye.

Wizi wizi wizi umekuwa mwiba kwa taasisi zetu, hakuna usafi inategemeana Nani yupo
Umeongea kitu kizuri sana TAMISEMI irud kwa waziri mkuu ikuli ina mambo mengi sana ilijirundikia wakati wa bwana yule na yote hii ilikuwa sababu ya ubinafsi
 
Upo sahihi kiongozi, Waziri Jafo sio mteuaji wala mwajibishaji wa watendaji wakuu wa Halmashauri (Wakurugenzi) na pia yawezekana mifumo ya uendeshaji wa halmashauri sio rafiki sana katika kudhibiti mambo yasiyoendana na matakwa ya serikali
Nakuona mdau hongera kwa utetez
 
Nikweli. ,hata uchaguzi serikali za mitaa 2019_ akiwa kwenye dhamana alitumia pesanyingi akijua uchaguzi haupo..akaandaa uchafunzi kwapesa nyingi mama alishauri hakisikilizwa
 
Punguza speed ili uandike kitu chenye "CONTENT" Makosa ya kiuandishi yanaweza kuondoa credibility yako!!

"Anahonywa" sijui kiswahili gani hiki, huwa nakereka sana na watu msioweza kujua matumizi ya herufi"h"


Anyway, kujiuzuru ni rahisi kuizungumza, hata hivyo watajiuzuru wangapi? Kwakuwa amepewa nafasi nyingine ya yeye kufuatilia agizo hilo, tusubiri utekelezaji wake kisha tutahoji nafasi yake ya uwaziri!!

Ahsante!
Kujiuzuru [emoji777][emoji777][emoji777]

Kujiuzulu[emoji818][emoji819][emoji736]
 
Jafo wanamuonea tu,wakurugenzi wengi wameingia kwa kiki za uanachama wa kijani pia ni vilaza mno hawawezi kusimamia pesa za serikali.Aanzia kwa hao DED ndo shida zipo
Nayo inachangia pia,..mtu ajira ya kwanza kwenye utumishi wa umma anaanzia kwenye ukurugenz direct..mfano Yule Kamoga alikuwaga clouds, aliteuliwa direct kuwa mkurugenz mbulu huko na wapo wengi wa hivyo ...shida ni cheo cha utendaji kwa mtu aliyetoka nje ya system moja kwa moja lazima apate tabu kwa muda kufit,tofauti ya miaka ya nyuma walikuwa wanawapindisha wakuu wa idara waliofanya vizur
 
Hii ni mara ya pili huyu waziri wa TAMISEMI anahonywa mbele ya hadhara kwamba abadilike katika utendaji wake

Kwa kauli ya leo kutoka kwa Rais Samia Suluhu, Jaffo anatakiwa kujizuru nyazifa zake

Kakini pia huyu Jaffo ana nini cha mno mpaka aendelee kupewa maonyo kila siku juu ya utendaji wake na usimamizi wa mali za umma?
Katika hili Jaffo unatakiwa utumie hekima na busara kuiacha TAMISEMI, kiuhalisia wizara hii kubwa imekushinda

Kama anaonewa si nae pia aachie Ngazi!
 
Yaani juzi tu wala maboga walibwatuka kuwa jiwe ni Rais pekee aliyeweza kuikoa Tz na genge la wezi.

Hata kabla hajaoza kaburini anaonekana ni mwizi. Tulisema mapema tukaonekana wasaliti kiko wapi sasa.

Cha ajabu wala maboga wanajinadi mtaani kuwa kimetoka chuma kimeingia chuma.

Acha kwanza nitafakari hizi kauli labda uwezo wangu wa kuwaza unaanza kuchoka.
Kama umejitambua sawa ni kweli uwezo wako wa kufikiri ni mdogo yani IQ yako ni ndogo inawezekana ni 0.00000001

Watu walikuwa wanasema JPM anapambana na wala rushuwa pamoja na mafisadi na alionyesha vitendo katika hili

Si dhani kama kuna mtanzania aliyewahi kusema kuwa JPM amemaliza wala rushuwa wote na mafisadi wote nchini

Sasa kama wewe hukuwahi kuziona juhudi za JPM katika kupambana na mafisadi pamoja na wala rushuwa hilo linatokana na uwezo wako wa kufikiri

Ila sisi wenye IQ kubwa tuliliona hilo na tunataka mama Samia aendeleze pale alipoishia
 
Hatujui mengi yaliyokua yanaendelea ndani combination (hayati na mama) ila kwa tafsir ya haraka haraka hiki kinachofanyika ni kua kipndi Cha hayati maamuzi yalikua yanatolewa na mtu mmoja tu na mawazo ya mama hayapewi nafasi,ila kwa jicho lingine hotuba ya mama leo inatoa kengele kwa watu wafuatao wajiandae kisaikolojia jafo,waziri mkuu, na Yule wa azina waliochota mapesa kipind cha hayati akiwa mgonjwa

Kama uko ushahidi huo si fedha zipigwe pini na zirudishwe na awatumbue na atoe sababu hii kama kitumbulio.

Ila hii ya leo haiko vizuri jinsi inavyotumika. Mfano ATCL imepata hasara miaka mitano accumulative. Je wakati JPM anaishi, CAG alishatoa ripoti ikionesha ATCL walikuwa wanatengeneza faida? Je mashirika mengine ya ndege ya kaliba ya ATCL na makubwa yalitengeneza faida gani kipindi hicho? Tulinganishe.

Lakini mfano Suala la Mh Jaffo, JPM aliuliza kuhusu bei ya Stendi ya Mbezi ya Kimara hii inayoitwa Magufuli. Na alisema alijishauri kumchagua na kumrudidha tena lakini alifikiria anavyojituma usiku na mchana akaona haidhuru ampe another chance. Sasa kwa nini tena litake kutumika kutaka kumchafua JPM marehemu mbele ya macho ya Watanzania na kumpa Mh Rais SSH sifa eti hakujua yanayo endelea.!!

Propoganda za aina hii hazimsaidii wala hazita msaidia huyu Rais wetu zaidi ya kuwaudhi Watanzania na kumharibia asubuhi na mapema katika Urais wake. Yeye ajikite kutenda kazi na matokeo ya kazi yake yataonekana tu, utandawazi uko wa kutosha hasa. Hii ya kutaka kucheza na legacy ya JPM itamgharimu vilivyo. Ndio maana twajiuliza kwa nini kaanza na Riport ya CAG? Kwa nini jimapili huku wapambe nuksi mitandaoni wakikashifu marehemu JPM siku tatu tu baada ya kuzikwa kuwa angalikuwa kwenye mimbari Kanisani. Mara ngapi JPM kateu na baada ye akafanya kazi ya uapishaji jumapili?
 
Back
Top Bottom