Rais Samia Suluhu: Mkikidhi vigezo, Chato tutaifanya kuwa Mkoa

Rais Samia Suluhu: Mkikidhi vigezo, Chato tutaifanya kuwa Mkoa

Ukabila ni turufu ya mwisho ya CCM kuendelea kubaki madarakani, na Magufuli alikuwa ameandaliwa kwa hilo.

CCM waliamini kabisa, kuwa Chadema ilikuwa ni hatari sana kwa wao kuendelea kula keki peke yao.

Magufuli aliandaliwa ili kura za Wasukuma ziende CCM lakini kutokana na Magufuli na utawala wake wa mkono wa Chuma ilipofika Uchaguzi wa 2020 Wasukuma wengi walipanga kumtosa, ndipo CCM wakafanya wizi wa kutisha kupata kutokea kwenye nchi ya kidemokrasia.
 
Ikiwa mkoa,itasaidia nini?itaongeza kipato kwa wananchi?itaongeza ajira?zaidi itaongeza gharama na watumishi tu,RC,DC,RAC ambao hawazalishi kitu zaidi ya kula mishahara tu,
Bora wangesema tujenge kiwanda,Mi Afrika bwana shida sana.inataka mkoa,mie kijana wa bodaboda itanisaidia kwa lipi?
Mtu mmoja aniambie Mara ya mwisho kusikia USA,au UK imeongeza mkoa au wilaya,au jimbo,lini?
sisi ni waafrika sio wazungu,tatizo umezaliwa ukiwa na tamaa ya Mali za wenzako
 
Mkuu, ndio ulikuwa mpago wenyewe - kumega sehemu ya Mkoa wa Kagera specifically Ngara may be part ya Karagwe na Kasulu - usifikiri Burigi ilikuwa inapigiwa debe as if it belongs to Chato bila sababu. Mpango huo nilikuwa siuingi mkono hata kidogo, hasa uporaji wa Ziwa Burigi na kulibatiza Chato /Burigi wakati ukweli ni kwamba Ziwa hilo lipo Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera.
kwani chato ikiwa mkoa wewe utapongukiwa nini,acha wivu kwa mambo yasiyo kuhusu
 
"Kuhusu suala la CHATO kuwa mkoa, nimekwisha kujulishwa kuwa mchakato umekwisha kuanza, sisi kama serikali tunaomba mkamilishe mchakato huo kisha mtuletee, Tukiona umekidhi vigezo tutaupandisha HADHI na Kama utakuwa haujakidhi vigezo tutawaambia nini cha kufanya ili ukidhi vigezo vya kuwa mkoa."- Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania
View attachment 1734954
ila haijakaa vizuri kwangu binafsi yani Geita ikatwe baada ya miaka mitano ya kuinyanyapaa kujenga kila kitu Chato? Chato inaweza kuwa mji ndani ya mkoa wa Geita!
 
Mama amekubali, amesema hata kama wataona vigezo havijakidhi basi watawaelekeza ili vigezo vikidhi

Ndio nimeanza kumuona huyu mama hamna kitu

Basi Butiama, Mkuranga, Bagamoyo, Masasi nazo zingefanywa mkoa basi kwa kuwa nazo zimetoa viongozi waliofanya makubwa tu

Unaipa chato kuwa mkoa wakati kuna mikoa mikubwa kama Morogoro haijagawanywa
Maza kajibu kiutu uzima...

Ni kama uulizwe lini utajenga ukweni. Unawaacha 50 50.
 
Tatizo sio Chato kama Chato tatizo lipo wanasiasa wanapo endelea kuigawa nchi na kutengeneza mikoa,majimbo,wilaya,harafu wakituaminisha kwamba hicho kitendo kinaleta maendeleo,
Mwananchi wa kawaida anataka Maji,shule,afya,Usalama,ajira,chakula,badala ya kufikiria kuigawa nchi na kuongeza maeneo ya kiutawala,bora wangesema tutajenga mradi wa kilimo Cha umwagiliaji mkubwa kuliko yote Afrika,wa miwa,Mpunga,au kiwanda Cha nyama,maziwa,au kuweka plant ya kua assemble magari,wao wanataka kuifanya Chato iwe mkoa,tupate RC,RAC,RPC,na mavyeo meeengi yasio na tija,hapa hatuleti maendeleo,tunaongeza Wage bill kwa serikali,Mkoa sio kiwanda,hatuzalishi,ni utawala tu,hauongezi panadol Wala asprini,
Kama ni huduma za ardhi,jenga ofisi ya kanda,weka maofisa kwenye ofisi ya DC,
Badala ya kuleta RC,na kumjengea Ofisi,bora kijengwe chuo kikuu Cha sayansi na tekinolojia,silicon valley iwe Chato,au kuna ubaya gani kukawa na Kariakoo nyingine Chato,lakini sio limkoa,
Hakukuwa na Tija kuigawa Arusha,kutengeneza Manyara,hakuna tija kuwa na Katavi,simiyu,Dar ilikuwa na wilaya tatu tu,Kinondoni,Ilala,Temeke,leo zipo tano,hata kama watu wameongezeka,ukubwa wa Dar upo pale pale kijiografia,kama ni huduma huitaji watumishi wengi,ni vitendea kazi tu,ongeza mashule,hospitari,vituo vya polisi.
Madakitari.sio huu upuuzi wa kuongeza watawala.
Hili ndio jibu tosha la maada hii,nahakika samia akiliona hili jibu ndio kitakuwa kipaumbele chake
 
Mama Samia aangalie huko Kisiwani Pemba wana dhiki iliyosababishwa kisiasa ajikite zaidi katika kulijenga hili Taifa maana kujenga Nchi inakuwa rahisi iwapo Taifa liko imara
 
Ule uwanja wa ndege kwushnei.
Tuliwaambia uvccm kuwa uwanja huu haukupaswa kuwekwa Chato kwasasa wakabisha.
Haya nendeni mkaugeuze danguro
 
Wilaya tajwa hapo juu zinaunganishwa na mbuga ya Burigi-Chato. Kwa ukubwa wake, zinatosha kuwa mkoa. Mkoa huu utakuwa na kila vigezo vya kuwa mkoa kwa vile una idadi ya kutosha ya watu, eneo, na kila sababu ya kuwa mkoa hata pasina kuwa ndiko alikozaliwa Magufuli.n Rais Samia amesema ataufanya mkoa kama utakidhi vigezo. Hapo nimetaja vichache. Je, wewe unashaurije?
Naomba na sengerema isogozwe mkoa wa Chato maana imezidi ukubwa.
 
Wabongo bana. Utazani hawataki maendeleo.

Aliondoka pinda wakasema kama wewe.

Sasa hivi kule mpanda ndege zinatua.

Hapo chato airport patanoga na hautaamini macho yako
mkuu umenikumbusha kweli huyu mwamba yupo wapi ni muda sasa sijawahi kumuona wala kumsikia nilitegemea leo nitamuona msibani lakin sijafanikisha kabisa(MIZENGO PINDA) waziri mkuu mstafu,Kama unahabari zake tafadhali
 
mkuu umenikumbusha kweli huyu mwamba yupo wapi ni muda sasa sijawahi kumuona wala kumsikia nilitegemea leo nitamuona msibani lakin sijafanikisha kabisa(MIZENGO PINDA) waziri mkuu mstafu,Kama unahabari zake tafadhali
Yupo mzima. Mara ya mwisho kumuona ni tarehe 20 machi 2021 pale lumumba. Kwenye kikao Cha kamati kuu ya CCM.
 
Back
Top Bottom