Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 13,417
- 23,310
Hatuwezi kubadili jina la Mkoa wa Geita kwa ajili ya kuwafurahisha watu wenye akili fupi eti kumuenzi Mwendazake!! Why so much propaganda?? Ni nini cha ziada alichofanya zaidi ya UDIKTETA, kutumia raslimali za nchi vibaya kwa kujenga miundombinu ya kitaifa kijijini kwake??Hivi katika yote uliyo orodhesha kuna kigezo hata kimoja kinacho kidhi uundwaji wa MKOA wa sijui Chato/Robondo - hakipo kabisa.
Sijui kwa nini watu wanaendelea kupoteza Mega Calories kuzungumzia mambo ya kulazimishana uundwaji wa Mkoa ambao hauna kigezo wala ulazima wa kuanzishwa in the first place - kama kigezo ni kutaka kumkumbuka/muenzi Magufuli, basi Mkoa wa Geita upewe jina la Magufuli au Chato nk. Mbona Mkoa wa Ziwa magharibi ulibadirishwa jina na kujulikana kama Mkoa wa Kagera.
Kosa amefanya yeye kuweka vitu Chato badala ya Geita au Kagera, halafu eti sisi tunajadili kubariki kosa la Mwendazake kwa kuanza kumega ardhi za hiyo mikoa jirani?? Kweli TUTADHARAURIWA sana na vizazi vijavyo tukifanya hivyo