Rais Samia tafuta fedha au ingia mkataba na sekta binafsi wajenge uwanja wa Mpira wa kisasa Dodoma

hivi mpuuzi wewe si ndio mlikuwa mnasema mnataka maendeleo ya watu na sio vitu???

na vitu unavyotaka ni uwanja wa mpira

mbegu za mbowe zimekuharibu ubongo
Tuliza hasira. Wakati wa utawala uliopita, wengi tulilalamikia maendeleo ya vitu yaende sambamba na maendeleo ya watu!

Hatukusema tunataka maendeleo ya watu tu.
 
NHC wameamua kutumia UCHAWI ili miji ING'ARE..... Zaidi ya magorofa 500 yameota maeneo ya Nzuguni DODOMA leo... Kwa sasa HALMASHAURI YA JIJI INAANGAIKA KUMILIKISHA WATU MAGOROFA HAYO... HAKIKA UCHAWI UNALIPA BADALA YA KUJENGA UNAKUTA MAJENGO YAMEOTA KAMA UYOGA, MAHARAGE.... yanavutia.... UWANJA UTAOTA HAKUNA HAJA YA KUJENGA

 
Thread safi
 
Uwanja wa mpira wa Dom si karibu utaanza bila hata na kushirikiana na sekta binafsi mkuu.
 
mfalme wa morocco alikuwa tapeli..tujenge billion 100ntujenge uwanja wa kiasas dodoma,mbeya,,mwanza na arusha
hata mimi nilishangaa, yaani Morocco masikini kama sisi tu hao watupatie msaada? kwa manufaa gani kwao?...Mh Samia chukua hata hizo hela za tozo, jenga uwanja. pia wananchi wameshaanza kukusema ati wewe una mpango kurudisha serikali Dsm, hata wafanyakazi wengi tu wanarudi. ile move ya kuhamia Dodoma ilienda vizuri sana tunaomba iendelee. vilevile, wanasema ati hujengi dodoma (barabara, viwanja nk) kama Magu alivyokuwa anataka kufanya. mji wa mtumba n.k. wasije kuja kukusema sana wakati wa kampeni 2025. Ubarikiwe.
 
Ukiwasikiliza vijana wa CHADEMA, unajua wazi kwanini Div 0 ya Form 6 ya Mbowe ndio inawaongoza, low thinkers sana, it can't be,
kuna mambo ya aibu huko CDM badala ya kuhoji wao wanalala usiku kulalamikia Mh. Rais, hata ofisi tu hawana. Aibu tupu. CHADEMA ni Saccos ya Mbowe, ila misukule hawaelewi tu.

Imagine mtu anashauri uwanja wa mpira mkubwa wakati huu, wakati sio priority kabisa hata kidogo, watu wanataka maendeleo plz plz, maji, huduma za afya bora, elimu bora, barabara, umeme wa uhakika, kilimo cha kisasa, masoko ya mazao yao, kuwezeshwa kiuchumi kwa kupata mikopo ya riba nafuu hasa single digit 9%, 8%, 7%, ajira mpya, usalama wa raia na mali zao, wastaafu kupata haki zao mapema, kudhibiti rushwa, kudhibiti matumizi ya serikali, etc etc

Sasa ww unashauri uwanja mkubwa wa mpira wakati huu?
 
Hawa wajingai na wenye uwezo mdogo wa kufiiri nao wana-enjoy uhuru wa kutoa maoni.
 
Kumbe unazikubaki kazi na maono ya JPM na mrithi wake Rais Samia. Safi sana kamanda. Uzalendo na utanzania kwanza πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™
 
Halafu baada ya kujengwa tuvimilikishe kwa ccm
Kama kawaida, unaongeza neno CCM kabla ya jina la uwanja na tayari unakuwa wa CCM!
Siku akija mwingine akaondoa hiyo ccm kabla ya jina la uwanja sijui itakuwaje. (rais anaweza maana ana mamlaka ya kufuta umiliki wowote ule wa ardhi)
 
Hii nchi Maskini sana, mpaka uwanja wa mpira tunaomba tujingewe na kwa ufadhili wa nchi nyingine?

Hii nchi Misaada kila kona
Inasikitisha na kuhuzunisha, bila kusahau kuaibisha.

Tumekuwa na tabia mbaya sana kama nchi.

Hadi hapo tutakapoamua kwamba tunaweza kufanya mambo mengi kwa ajili ya maendeleo yetu hapo ndipo tutakapoanza hatua za kwenda mbele.
Moyo huo wa "tunaweza" ulikuwepo wakati wa Mwalimu Nyerere, baada ya hapo, siku hizi ni lazima tujengewe hata matundu ya chooo!!?? Ni aibu gani hii!!!!
 
Hapangiwi kipi cha kuanza na kipi cha kumaliza nacho...
 
Hakuna haja ya kujenga uwanja Dodoma kwa pesa zote hizo. Ukitoka kilometer 15 kutoka Dodoma Mjini (Mkonze, Matumbulu) watu wanachota maji kwenye madimbwi. Hizo fedha bora zitumike kuleta maji ya uhakika Dodoma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…