#COVID19 Rais Samia: Tanzania haitakubali chanjo ya Corona kabla ya kujiridhisha

#COVID19 Rais Samia: Tanzania haitakubali chanjo ya Corona kabla ya kujiridhisha

Hivi watajihakikishiaje kuwa iko salama? Si inabidi wafanye clinical trials ambazo zitawachukua sio chini ya miezi sita kwa kikundi kikubwa cha kutosha? Hizo dawa za kufanya hizo trials watazitoa wapi? Na wakati wanangoja hayo matokeo watu wanaendelea kufa.

Amandla...
 
Uzuri wake hata ikija inakuwa option, kama huitaki unakaa mbali tu...wanaoitaka watachanja.

Corona mwaka jana ilipiga ikatembea na watu Tanzania na kwingineko, vumbi likatulia ilipokuja tena kuanzia Nov to April imepita na wengi pia na wengine waliumwa, binafsi nawajua walioumwa serious na ambao hawakuwa serious....decembere to April misiba ilikuwa mingi sana uraiani na wale jamaa zetu wa Moshi barabara ilikuwa busy kweli....ghafla April mpaka sasa imetoweka tena....tumuombe Mungu atunusuru na pia tuchukue tahadhari...wanaoteseka na Corona hawakuomba iwapige ni mipango tu ya Mungu..
Hiyo sio corona mazee, corona haiwezi kutimba watu wa tano ikaenda, corona ikija inatimba timba zaidi ya watu 100 na kuendelea, in facts corona huwezi kuificha , corona haifichiki, kwani huoni India?
 
Hii ni kauli ya Mh Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania Madam President Samia Suluhu Hassan. leo.

"Nataka kuwahakikishia kwamba tahadhari zote mlizotoa hapa juu ya chanjo na mengine zitafuatwa, kikamilifu na Serikali yenu, hata hivyo hii haina maana kwamba tutapokea kila kitu tutakacholetewa au kuambiwa la hasha lazima na sisi tukiridhishe.

Hata suala la chanjo tutajiridhisha kwanza kabla ya kuamua kutumia au kuacha kutumia.hivyo nawaasa watanzania kutokuwa na hofu yoyote Serikali iko makini sana katika kushughulikia suala hilo"......Rais Samia Suluhu Hassan 14/mei /2021.

MY TAKE ON COVID 19 VACCINE
Tanzania haina historia ya kugomea wala kukimbilia chanjo.
nikitolea mfano wa chanjo dhidi ya kansa ya shingo ya kizazi ambayo duniani ilianza kutumika mwaka 2006 ilichukua miaka 12 kuanza kutumika rasmi nchini Tanzania.Mwaka 2018 Serikali ilianza kueneza matumizi ya chanjo hii kwa awamu katika mikoa ya Tanzania.baada ya majaribio kadhaa miaka michache kabla.

Kenya walianza kuitumia mwaka mmoja au miwili kabla.

Ikumbukwe kansa ya shingo ya kizazi imeumiza na kuua kina mama wengi pengine kuliko covid 19.do we have clear reasons why should the nation fast track and accept covid 19 vaccines?

Wazo la kufanya uchambuzi wa kina juu ya chanjo za corona ni wazo la kisayansi.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
View attachment 1784954

Uzuri wake mama na JPM ni mtu mmoja lakini katika mambo ya msingi. Kujiridhisha kwake ni kusikia msimamo wa tume yake ya wataalamu. Kama hivi:

IMG_20210514_192000_156.jpg


Nyie siyo wasemaji wa mama Samia rais wa JMT.

Huyo msimchanganye na mufti.

IMG_20210514_210624_218.jpg


Ambaye naye aghalabu hata yale ya nyungu nayo ndiyo basi tena.

Heko Mufti na Heko Samia kwa kuweka wazi misimamo yenu dhidi ya mabush dokta na mamburula wote.
 
Ni

Ushauri tu maana unapigika sana na awamu sita 🤣🤣, na ndo kwanza ni miez miwil tu. Shubaaamiiit!!
Mimi niko vizuri sana aje nani mimi nimwendo wakula bata tu mpaka Mungu anichukue. Usifikiri mimi ni kama hao kula kulala wenzako. Hata akija Rais wa Mashoga Lissu mimi nitakuwa nakula bata tu mkuu!!
 
Jamaa yangu mmoja kaburu aliipata hapo zanzibar tukamshauri tiba za magu zile za vitunguu n.k na nini baada ya siku 3 akawa poa, alirudi SA baada ya kama miezi mitatu, akakutana na second wave, bado kidogo aage dunia, baada ya kupona akarudi tz na hataki kabisa kurudi tena SA, huku weekend ni Zenji ama bara na hapo ni bata tuu

Huu ugonjwa wa kuathiri mfumo wa upumuaji una mengi nyuma ya pazia
 
Hiyo sio corona mazee, corona haiwezi kutimba watu wa tano ikaenda, corona ikija inatimba timba zaidi ya watu 100 na kuendelea, in facts corona huwezi kuificha , corona haifichiki, kwani huoni India?

hukuwa unaona wingi wa misiba huku mtaani, hukuwa ukiona barabara kuelekea Moshi tokea dar ilivyokuwa busy....vipi mbona siku hizi Barabara to Moshi is no longer busy?
 
Kauli hiyo ni pigo kwa mpiga debe wa chanjo Mbowe
Mh Rais Samia haya yaliyowakuta wahindi India yanatokana na misemo hii hii ya wataalam wanaangalia,wanaangalia.Waziri mkuu alinukuliwa akisema miezi michache iloyopita kuwa nchi yake bado inaliangalia suala hilo.Sasa yamemkuta Mamia kwa Mamia ya wahindi wanateketea.Jamani Mh Rais ugonjwa huu haukupi taarifa.TUSIJE KUATHIRIKA KAMA WENZETU.DUNIA YA LEO KIJIJI.MH RAIS AMUA TU.
 
Hizi drama za corona zinasisimua na kuchekesha sana.

Miezi michache nyuma, kulizuka wimbi kubwa la vifo vya viongozi wakubwa na watu mashuhuri — Tukaambiwa wamefariki kwa corona.

Muendelezo wa vifo ulichachamaa mpaka ukamkumba Rais John Magufuli. Naye "tukaaminishwa" amefariki kwa corona kinyume na taarifa rasmi ya daktari.

Tangu alipofariki Rais Magufuli, hatusikia tena kuhusu vifo vya vigogo wa serikali.

Tukaambiwa corona imeenda likizo (annual leave) na kwamba itarejea kwa makali hapo baadaye.

Pamoja na drama zote hizi za kuigiza, sisi wakazi wa Kariakoo siku zote tunasongamana na hakuna hata mmoja aliyeugua japo mafua ya bahati mbaya.

Hata yale mabarakoa sijayaona. Watu wanadunda tu.

Hakuna cha wimbi wala mawimbi. Kila siku watu wapo tu na wanaendelea na maisha yao wakiwa na afya zile zile.

Tukaambiwa linakuja wimbi sijui la pili. Wenyewe wanaita ati "second wave".

Hilo wimbi nalo likaja likatukuta vile vile na likaondoka likatuacha vile vile.

Hivi sasa tunaambiwa kuwa hilo wimbi limekimbilia India. Likipiga "rivasi" linarudi tena Tanganyika likiwa na maguvu mengi.

Bibi samia anatueleza habari za chanjo. Bila shaka ziko mbioni kuja.

Najiuliza, hizo chanjo anamdunga nani?

Sisi wakazi wa Kariakoo na kwingineko, wala hatuna ugonjwa wowote ule.

Tunapoelezwa kuhusu chanjo, tunahamaki!

Wale wajuzi wa corona hebu mtueleze, hizo chanjo mnamdunga nani?

Mnawadunga hawa hawa watu ninawaona wakiwa na afya tele kila siku?

Ama kuna wagonjwa mahali ambao hatujaambiwa kuhusu taarifa zao?
Mama hana uwezo wa kugomea chanzo,watu wajiandae tu chanjo inakuja.watapigwa chanjo ingawaje hawaumwi.
 
hukuwa unaona wingi wa misiba huku mtaani, hukuwa ukiona barabara kuelekea Moshi tokea dar ilivyokuwa busy....vipi mbona siku hizi Barabara to Moshi is no longer busy?
Mtu akifa na corona unaweza kumsafirisha kwenda kumzika wewe kwenye hayo mabasi yenu bila tahadhari? sio nyie, nurse na madaktari wote waliokuwa wana watibu tayari wangekuwa affected va virus, mlifikiri mna uelewa mkubwa wa corona kwa kutangaza uelewa wenu ulivyo chini, watu walikuwa wana wachora tu.
 
Kiongozi badala ya kuinstill confidence unainstill fear kwa wananchi in the name of diplomacy.
Kwa hizo kauli,Mjiandae chanjo inakuja.
Magufuli alikomaa ila alitukanwa sana.
 
Hii ni kauli ya Mh Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania Madam President Samia Suluhu Hassan. leo.

"Nataka kuwahakikishia kwamba tahadhari zote mlizotoa hapa juu ya chanjo na mengine zitafuatwa, kikamilifu na Serikali yenu, hata hivyo hii haina maana kwamba tutapokea kila kitu tutakacholetewa au kuambiwa la hasha lazima na sisi tukiridhishe.

Hata suala la chanjo tutajiridhisha kwanza kabla ya kuamua kutumia au kuacha kutumia.hivyo nawaasa watanzania kutokuwa na hofu yoyote Serikali iko makini sana katika kushughulikia suala hilo"......Rais Samia Suluhu Hassan 14/mei /2021.

MY TAKE ON COVID 19 VACCINE
Tanzania haina historia ya kugomea wala kukimbilia chanjo.
nikitolea mfano wa chanjo dhidi ya kansa ya shingo ya kizazi ambayo duniani ilianza kutumika mwaka 2006 ilichukua miaka 12 kuanza kutumika rasmi nchini Tanzania.Mwaka 2018 Serikali ilianza kueneza matumizi ya chanjo hii kwa awamu katika mikoa ya Tanzania.baada ya majaribio kadhaa miaka michache kabla.

Kenya walianza kuitumia mwaka mmoja au miwili kabla.

Ikumbukwe kansa ya shingo ya kizazi imeumiza na kuua kina mama wengi pengine kuliko covid 19.do we have clear reasons why should the nation fast track and accept covid 19 vaccines?

Wazo la kufanya uchambuzi wa kina juu ya chanjo za corona ni wazo la kisayansi.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
View attachment 1784954
Tofauti na JPM, huyu mama anaonekana anaitumia vizuri elimu yake aliyoipata hata kama si kubwa kivile!
 
Sizungumzii conspiracies hapa mkuu,I am talking about hard science,acheni ujinga.Conspiracy iko wapi hapo.This is pure science.

Hao hao wanataka kuwaua kwa the so called C-19 ambayo Infact ni bio weapon na OS, ndio wame wawekea concept ya conspiracies kwenye akiki zenu,na ninyi bila kujua mmeishupalia, acheni ujinga.Wauaji wetu ndio wenye conspiracies kama hii ya C-19!Change your mindset.
Kweli kabisa ila upinzani wanasapoti mama akosee kwenye janga hili watu watakapoanza kufa baada ya kuchanjwa na mlipoko kuongezeka wapate ajenda 2025.
maana sasa wamepoteana hawajui wanafanya nini.
 
Na mtashangaa wenye nafasi zao wote watakuwa wamechanja. Unadhani wote wanasubiri kibali cha serikali? Ikija itawakumba walala hoi ambao wanashabikia humu. Msimlaumu mtu.

Amandla...
 
We kama hutaki chanjo, tulia tu kila mtu na maisha yake isiwe tabu... na kila mtu na chaguo na maisha yake...kazi iendelee.
Mpotosheni tu kwani waliochanjwa wameizuia ?lockdown zaidi ya mwaka sasa,unayatamani hayo maisha? Kisa kushobokea uwe kama wanavyofanya wazungu.Umepungukiwa na nini unavyoishi sasa?
Baadaye mnataka kuja kumsimanga rais kaliangamiza taifa.
 
Naona unasema ikatuacha vilevile !! unaweka ushabiki kwasababu hujafiwa kaongee na wale Watanzania waliopeteza ndugu zao kuanzia mwezi wa kwanza 2020!. Chanjo ni kwa wale wanauhitaji kama hauko kwenye wahitaji basi usifanye lakini huna haki za kuweka siasa zako kwa wananchi wote kwasababu ya fikra binafsi. Hakuna mtu analazimishwa kufanya chanjo wanacho omba wengi ni upatikanaji tu maana hizi chanjo haziuzwi kwa watu binafsi kwa sasa. Chanjo zingekuwa zinapatikana wala watu wasingeongelea serikali. Mimi nimepoteza marafiki wawili Tanzania kwa Corona najua uchungu wake
Kwa hiyo unaona hao ndugu zako wawili watu wachanjwe? Watu wamepoteza makumi elfu ya Malaria na maisha yanasonga.
kwa hiyo mkichanjwa na ndugu zako mtaishi milele? Je Ulaya walikochanjwa au India waliochanjwa hawafi?.
 
Wewe kama hutaki chanjo tulia ... wengine wanahitaji sababu either wanamagonjwa sugu ama ni wazeee....

Huu ugonjwa sio wa kubezwa especially kama una tatizo la kiafya ama una umri mkubwa .

Kaa kimya mzee
ama wanataka kusafiri nje ya nchi!
 
Hata chanjo tunazotumia zilikuwa ni mpya sana ulimwenguni muda zinaanza kutumika.Tanzania ilitumia wataalamu wake na washirika wa chanjo ulimwenguni hadi maamuzi ya kuanza kuzitumia yalivyofikiwa.

Sawa Mkuu Tuzidi Kumuomba MUNGU
Nimeandika Meeengi nimefuta sababu Pressure ya Hili jambo ni Kubwa sana!toka Nje au ndani?Sijui?
Mwisho Nimemuweka Tuu MUNGU atusaidie mimi sijui chochote
Ila Tuanze na Viongozi itakuwa Vema sanaa Umri Kuanzia 50yrs kuendelea.Kama Nchi za Wenzetu wanavyofanya
 
Back
Top Bottom