Rais Samia tusaidie; DED Monduli na RC wa Arusha wametupora fidia ya ardhi Makuyuni

Rais Samia tusaidie; DED Monduli na RC wa Arusha wametupora fidia ya ardhi Makuyuni

MWIBAPORI

Member
Joined
Feb 10, 2017
Posts
60
Reaction score
35
DED wa Halmashauri ya Monduli pamoja na RC wa sasa wa Arusha Idd Kimanta wamepora fidia ya ardhi kwa taasisi za dini ya Kikristo na Kiislam pamoja na mwanamke mmoja waliopitiwa na umeme wa Kilovolt 400 kutoka Singida -Namanga katika Kijiji cha Makuyuni Wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha.

Mwaka 2016- 2017 Idd Kimanta akiwa DC wa Monduli alishirikiana na DED Monduli kuwadhulumu wananchi na taasisi za dini fidia iliyokuwa ilipwe na TANESCO kwa wananchi hao ambao walikuwa wamepewa ardhi hiyo kisheria na serikali ya kijiji cha Makuyuni kati ya miaka ya 2007- 2009.

Kijiji cha Makuyuni kiligawa ardhi hiyo kupitia vikao na mikutano halali kama inavyotakiwa katika sheria ya ardhi.

Mwaka 2016 TANESCO iliwatangazia wananchi wanaopitiwa na umeme huo katika ardhi yao wajitokeze ili kulipwa fidia na hapa ndipo DED wa Monduli na DC wa wakati huo IDD Kimanta walipoingia tamaa na kufanya kila mbinu ili wananchi na taasisi za dini ya Kikristo na kiislam wasipewe fidia bali wao wachukue kwa kigezo eti ardhi ni ya Halmashauri.

Baadhi ya wananchi walichukua uamuzi wa kupeleka shauri mahakamani lakini hata baada ya DED kushindwa vibaya katika mahakama kuu bado amewashawishi TANESCO isiwalipe fidia wananchi hao.

Mheshimiwa Rais wetu Samia Suluhu naomba utusaidie kuingilia kati ili tuweze kulipwa fidia ya ardhi yetu na kukomesha huu uonevu.
 
Kama mahakamani walishinda mnataka Samia awasaidieje, sanasana bebeni mabango mumsubiri wakati wa ziara yake vinginevyo mfateni mbunge wenu au rudini mahakamani mkakazie hukumu.
 
Hawa jamaa ni majizi sana wamewatesa sana hawa wananchi wa makuyuni wakishirikiana na kibaraka wao ambaye ni kada wa CCM aitwaye Stephano Stei.
 
Kama mahakamani walishinda mnataka Samia awasaidieje, sanasana bebeni mabango mumsubiri wakati wa ziara yake vinginevyo mfateni mbunge wenu au rudini mahakamani mkakazie hukumu.
Nafikiri hilo ndilo jambo wanalopaswa kufanya maana hawa walikuwa wanajiona miungu watu.
 
Kama mahakamani walishinda mnataka Samia awasaidieje, sanasana bebeni mabango mumsubiri wakati wa ziara yake vinginevyo mfateni mbunge wenu au rudini mahakamani mkakazie hukumu
DED wa Monduli amekuwa kama Mkurugenzi wa TANESCO kiasi kwamba hata pale sheria iko wazi anawashauri TANESCO kupindisha sheria ya fidia kwa mambo yaliyo wazi. sishangai hata hili la hukumu ya mahakama kuu ambapo yeye alikuwa mshitakiwa amewashauri vibaya TANESCO maana anataka kupiga hiyo hela na watu wa TANESCO.
 
Kama mahakamani walishinda mnataka Samia awasaidieje, sanasana bebeni mabango mumsubiri wakati wa ziara yake vinginevyo mfateni mbunge wenu au rudini mahakamani mkakazie hukumu
Ukisoma maelezo ya mtoa mada utagundua kuwa DED, RC na TANESCO wanataka kuipiga hiyo fidia.
 
TANESCO kama wameona hukumu ya mahaka kuu na bado hawataki kulipa fidia halali basi nao watatakiwa kuchukuliwa hatua zikiwemo za kuidharau mahakama.
 
Suala la fidia katika kijiji cha Makuyuni limekuwa ni kichefuchefu na aibu kubwa kwa DED wa Monduli ambaye alionyesha waziwazi ana njaa ya vijihela vya fidia na kuanza kutengeneza mazingira ya kuwadhulumu wananchi. Bahati nzuri mahakama imemuumbua lakini bado anapigana vita ambayo soon itamgharimu sana yeye pamoja na Idd Kimanta.
 
Mateso waliyopata wananchi wanaodhulumiwa fidia zao waziwazi zikiwepo taasisi za dini ya kiislamu na wakristo itakuwa hasara kubwa katika maisha yake. Navishauri vyombo vinavyohusika viwasaidie hawa watu maana TANESCO tayari imeingizwa mtegoni katika kudharau mahakama ili kujipatia mapato ya aibu.
 
In short huyu DEC wa Monduli is a big loser naiomba TANESCO ijitenge naye ili itendee wananchi haki maana likija fumuka TANESCO watakuwa katika hali mbaya zaidi.
 
ukisoma maelezo ya mtoa mada utagundua kuwa DED , RC na TANESCO wanataka kuipiga hiyo fidia
Kuna ukweli katika hili kwa sababu TANESCO walishafika Makuyuni mara kadhaa kufanya uhakiki na waliona waziwazi kuwa maeneo ni ya wananchi lakini walikubali kupanga na DED kutufanyia dhuluma ya fidia. Ninaomba rais amwondoe huyu DED wa Monduli na RC wa Arusha mana hao ndio wanaozuia sisis kupata haki yetu kwa tamaa zao.
 
Kwanza RC wa Arusha hana maadili ya uongozi maana ni muhuni na huwa anafuata makahaba hadi wilayani Karatu kujidai anakwenda kwa shughuli za kikazi. Huyu ananajisi ofisi ya umma pamoja na kutudhulumu haki yetu
 
Rais ili tupate haki yetu naomba vuruga mtandao huu unaohusisha DEC Monduli, RC Arusha na Afisa ardhi wa Monduli aitwaye Mwanga. hawa ndiyo wanaunda genge la kuwadhulumu wananchi haki zao .
 
Rais ili tupate haki yetu naomba vuruga mtandao huu unaohusisha DEC Monduli, RC Arusha na Afisa ardhi wa Monduli aitwaye Mwanga. hawa ndiyo wanaunda genge la kuwadhulumu wananchi haki zao .
Bila hawa kuondolewa tena kwa aibu tutazidi kuzungushwa maana huu ni mwaka wa 5 tunazungushwa nenda rudi nenda rudi kwa mambo yaliyo wazi kabisa
 
Naomba kama tunayooandika humu ni uongo basi tupate watu waaminifu na wasioegemea upande wowote watakaotumwa(wasitoke mkoani wala wilayani) kuongea na wale wananchi waliodhulumiwa fidia ya ardhi iliyopitiwa na umeme wa KIlovolt 400 eneo la kijiji cha Makuyuni
 
Hii ni systemic problem maana DED ni kada DC ni Kada na RC ni kada wa chama. Mkoa mzima hauongozwi professionally bali kisiasa. na ijulikane kwamba viongozi wengi wa kisiasa hawatendei haki wananchi maana wako kwa maslahi yao na siyo ya wananchi hivyo automatically hapo kuna conflicts of interest.
 
Back
Top Bottom