Rais Samia: Tutafuta baadhi ya Mashirika yasiyoleta tija, yakifa wafe nayo

Rais Samia: Tutafuta baadhi ya Mashirika yasiyoleta tija, yakifa wafe nayo

Tatizo la Serikali ni ugumu wa kuelewa, wangeona Faida wanayopata NMB, CRDB, NBC wakaamua fanya hivyo kwa Mashirika yake hakika tungekuwa Mbali
Wanatangaza gawio NMB na Crdb wanalopokea halafu badala ya kupunguza Tu hisa zao huko kwingineko wanawaza kuuza outright
 
Kuna sandakalawe ya mashirika inakuja, I expect na baadhi ya Viwanda vitauzwa, kwa hio ndugu zangu tuanze kuwa karibu na maafisa mikopo, pia tujitahidi kusave, unaweza nunua kiwanda cha Urafiki hata kwa elfu kumi tu 😂😂😂😂
 
Private sector? Hakuna Mwekezaji atataka kuwekeza Sehemu kama tanesco, Imagine mteja anahudumiwa Bure akipata changamoto, Application fee bure halafu Connection fee anakuja kulipa 27K ni mwekezaji gani anaweza kuwekeza apo? Unless ije reform kubwa ambapo ikitokea hio Umeme haitakuwa huduma tena itakuwa Anasa
Kwa nini mteja nisihudumiwe bure wakati nanunua umeme wako? Wewe unauza umeme lazima ufanye uwezalo umeme unifikie nilipe...tatizo tanesco ni mikataba ya kipuuzi ambayo inawafanya walipe madeni kibao.
 
Kati mashirika umma 500 tuone yatabakia mangapi......wapungUe share as serikali.....tupime miaka 5 ijayo tuone ufanisi kama utabadilika
 
Ndio nachomaanisha, kwa rate zao za bei ya umeme,, hakuna investor ataona faida... Mi naona private sector waendeleo kuzalisha na kuuza umeme Tanesco kisha Tanesco watuuzie wananchi kwa bei affordable
Kwani bei zao ni ndogo sana? Kwa wenzetu mbona umeme mpaka wanapikia maharage ina maana hawapati faida?
 
Kuna kila dalili kuwa TANESCO wanakwenda kutolewa kwa Wajomba kama ilivyokuwa Bandari.
Kama TANESCO hawana tija bora nao wakabidhiwe kwa Wajomba tu ili wananchi wa kawaida na sisi tufaidike na huduma nzuri kutoka ugenini!! Maana tumechoka na Mambo ya kutumbuwana!!
 
Rais Samia amesema anasubiria ripoti ya Timu aliyoiunda Kupitia mashirika ya Umma yanayoripoti Kwa Msajili wa Hazina Ili juyafutilia mbali Yale ambayo hayana Tija Wala faida. Amesema Mashirika Yatakayokufa basi wahusika wajiandae kufa nayo.

“Serikali tumeamua kufanya tathmini ya utendaji wa mashirika yote ya umma na yale ambayo Serikali ina hisa kubwa. Lengo la tathmini hiyo ni kubaini mashirika yasiyo na faida ambayo yameshindwa kujiendesha na yanaitia Serikali hasara.”

"Nasubiri taarifa ya mwisho, ya mashirika gani yanabaki, gani yanaondoka, na gani yasaidiwe vipi kufanya biashara, na siku tutakayoyatangaza...haya mashirika yakifa, wafe nayo, sitaki kusikia shirika linazorota,meneja anapiga suti nzuri anatamba mitaani, hatutaenda pamoja".


---
My Take
Safi sana mh.Rais hakuna kulea ujinga ujinga wa miaka Mingi ambako watu waligeuza Mali ya Umma ni mashamba ya Bibi..

Kwa heri titisiielo na eitisii
 
Private sector? Hakuna Mwekezaji atataka kuwekeza Sehemu kama tanesco, Imagine mteja anahudumiwa Bure akipata changamoto, Application fee bure halafu Connection fee anakuja kulipa 27K ni mwekezaji gani anaweza kuwekeza apo? Unless ije reform kubwa ambapo ikitokea hio Umeme haitakuwa huduma tena itakuwa Anasa
Hiwa nawashangaa sana wanaotaka wawekezaji kwenye umeme hawajui kuwa bei ya umeme haitakuwa hii tena si ajabu unit 1 wakanunua kwa 1000 au zaidi
 
Tanesco ana supply tu. Yeye umeme anauziwa na mashirika mengine alafu anausambaza .changamoto ni kwamba ni monopoly ndo mana shirika halija changamka.
Mkuu sio kweli 90% ya umeme nchini uko produced na Tanesco, Inshu ya tanesco kutokuwa monopoly ni nzuri sana ila tujiulize je tanesco akianza kwenda kibiashara wananchi mtaweza kumudu izo cost?
 
Back
Top Bottom