Rais Samia: Uanaharakati, vikundi vya kigaidi na maandamano ni mfumo wa vurugu kuwasilisha sauti ya watu

Rais Samia: Uanaharakati, vikundi vya kigaidi na maandamano ni mfumo wa vurugu kuwasilisha sauti ya watu

Rais Samia leo July 17, 2023 amefungua mkutano wa wadau wa demokrasia barani Afrika unaowahusisha viongozi wakuu wastaafu mjini Arusha. Sehemu ya hotuba yake ameongelea namna ambazo si nzuri katika kufikisha hisia za wananchi.

Rais Samia: Kushindwa kwa Serikali kuhudumia mahitaji ya msingi imeibua malalamiko kwenye sehemu ya bara la Afrika. Baadhi kudharau na kufanya baadhi ya watu kwenye jamii kupinga na kudharau mamlaka ya Serikali kwa kuanzisha mifumo ambayo inatumia vurugu kuwalisha sauti ya wananchi.

Hii inajumuisha wanaharakati, vikundi vya kigaidi na maandamano. Na hii ni sehemu baadhi ya vipengele vya demokrasia kama uhuru wa kukusanyika na kutoa maoni vinatumika vibaya.

Pia, Soma=> Rais Samia akifungua Mkutano wa Wadau wa Demokrasia Barani Afrika wa Viongozi wakuu wastaafu, leo Julai 17, 2023

Sasa kama Rais hajui vifungu vya katiba alivyoapa kuvilinda ikiwepo na haki ya maandamano,basi hii ni hatari.
 
UVCCM kuandamana nchi nzima kuunga mkono serikali, pia wamtaka msajili wa vyama vya siasa kuchukua hatua stahiki



Hayo yamefahamika wakati mwenyekiti wa UVCCM kada Mohamed Kawaida alipokuwa anaongea na viongozi wa UVCCM na kutangaza azma ya kuandamana kila kona ya nchi kuunga mkono alichoita makubaliano ya serikali ya Tanzania na Dubai kuhusu bandari ....

UVCCM wataanza maandamano yao mkoani Dar es Salaam hapo tarehe 18 Julai 2023 amesema Mohamed Kawaida mwenyekiti wa UVCCM taifa na kisha kuendelea kuandamana katika mikoa mingine kuunga mkono hatua za serikali kuhusu bandari ...
[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Mama anatamka
Rais Samia leo July 17, 2023 amefungua mkutano wa wadau wa demokrasia barani Afrika unaowahusisha viongozi wakuu wastaafu mjini Arusha. Sehemu ya hotuba yake ameongelea namna ambazo si nzuri katika kufikisha hisia za wananchi.

Rais Samia: Kushindwa kwa Serikali kuhudumia mahitaji ya msingi imeibua malalamiko kwenye sehemu ya bara la Afrika. Baadhi kudharau na kufanya baadhi ya watu kwenye jamii kupinga na kudharau mamlaka ya Serikali kwa kuanzisha mifumo ambayo inatumia vurugu kuwalisha sauti ya wananchi.

Hii inajumuisha wanaharakati, vikundi vya kigaidi na maandamano. Na hii ni sehemu baadhi ya vipengele vya demokrasia kama uhuru wa kukusanyika na kutoa maoni vinatumika vibaya.

Pia, Soma=> Rais Samia akifungua Mkutano wa Wadau wa Demokrasia Barani Afrika wa Viongozi wakuu wastaafu, leo Julai 17, 2023

Mama anatamka kizungu swaaafi kabisa. Siyo kama Tibaijuka na intonation yake ya kihaya.
 
Vipi tena zile 4R’s zake alizotuambia aziamini tena, si kuna ‘resilience’ mule imekuwaje.
 
Samia anayaogopa maandamano maana ameshaona hiyo ndio itakuwa njia ya mwisho kumzibua masikio yake, ili atusikie tukimwambia ule mkataba wa bandari ni mbovu unaomkandamiza mtanganyika na kuidhalilisha ardhi yetu, utu wetu, na mipaka yake, ameyataka mwenyewe kwa ukaidi wake.

Sasa ameona ayaweke maandamano kundi moja na vikundi vya kigaidi, hajui maandamano yapo kisheria, hiyo ni haki ya mtanganyika, kama anajua vilipo hivyo vikundi vya kigaidi aliagize jeshi la polisi likavikamate, asipoliagiza jeshi maana yake anafumbia macho vikundi vya kihalifu, hatufai.

Lakini asijaribu kutuchezea "mind games" ili kupunguza nguvu za kuzidai bandari zetu zote waTanganyika walizopewa waarabu, kwa huu mpango wake amefeli tayari, muhimu namshauri tu aliagize jeshi la polisi litoe ulinzi kwa waandamanaji hiyo siku ikifika, sasa ndio anavuna matunda ya ukaidi wake mwenyewe.
Anajua yeye ndo sheria.

Mungu anapita nao kimya kimya
 
Watanzania tuna akili na ni wengi na tunao uwezo wa kujitokeza hadharani tofauti na watanganyika wenye ukosefu wa jeuri ya kutoka huko nje wakaonekana.

Watanganyika wengi ni mashujaa wa nyuma wa keyboard.
Usije siku moja ukashangaa huyo huyo atajitokeza na kulalamika juu ya hawa "Watanganyika wengi, mashujaa wa nyuma ya keyboard."

BTW: upo hapa" nyuma ya keyboard" kwa vile unauelewa umuhimu wa kuwepo, au siyo?

Sasa jaribu kutumia akili vizuri zaidi; ili usiwe unajinyesha kuwa kigeugeu.
 
Rais Samia leo July 17, 2023 amefungua mkutano wa wadau wa demokrasia barani Afrika unaowahusisha viongozi wakuu wastaafu mjini Arusha. Sehemu ya hotuba yake ameongelea namna ambazo si nzuri katika kufikisha hisia za wananchi.

Rais Samia: Kushindwa kwa Serikali kuhudumia mahitaji ya msingi imeibua malalamiko kwenye sehemu ya bara la Afrika. Baadhi kudharau na kufanya baadhi ya watu kwenye jamii kupinga na kudharau mamlaka ya Serikali kwa kuanzisha mifumo ambayo inatumia vurugu kuwalisha sauti ya wananchi.

Hii inajumuisha wanaharakati, vikundi vya kigaidi na maandamano. Na hii ni sehemu baadhi ya vipengele vya demokrasia kama uhuru wa kukusanyika na kutoa maoni vinatumika vibaya.

Pia, Soma=> Rais Samia akifungua Mkutano wa Wadau wa Demokrasia Barani Afrika wa Viongozi wakuu wastaafu, leo Julai 17, 2023


Hakuzungumzia la bandari kuwa yeye ameshindwa kuwasikiliza wananchi? Kumbe anajua ni nini kitafuata pale ambapo wananchi watachoshwa na mfumo mbovu wa kiutawala?
 
Usije siku moja ukashangaa huyo huyo atajitokeza na kulalamika juu ya hawa "Watanganyika wengi, mashujaa wa nyuma ya keyboard."

BTW: upo hapa" nyuma ya keyboard" kwa vile unauelewa umuhimu wa kuwepo, au siyo?

Sasa jaribu kutumia akili vizuri zaidi; ili usiwe unajinyesha kuwa kigeugeu.
Harakati za kuidai Tanganyika nyingi zinatokana na ubaguzi ulio katika mawazo yetu sisi tunaoficha majina yetu halisi.

Bado Tanganyika haina nguvu wala sababu ya kudaiwa kwa kigezo chepesi cha suala la bandari. Hilo ni suala la kiuchumi zaidi kuliko la kianaharakati.

Wanaharakati wamelivamia kwa wingi, wengi wao wakitumika na wapigaji wa muda mrefu wa hapo bandarini. Kwa makusudi kabisa wakitambua namna wanavyowakwaza wafanyabiashara wa kweli wanaoagiza na kusafirisha mizigo bandarini kila siku.
 
Harakati za kuidai Tanganyika nyingi zinatokana na ubaguzi ulio katika mawazo yetu sisi tunaoficha majina yetu halisi.

Bado Tanganyika haina nguvu wala sababu ya kudaiwa kwa kigezo chepesi cha suala la bandari. Hilo ni suala la kiuchumi zaidi kuliko la kianaharakati.

Wanaharakati wamelivamia kwa wingi, wengi wao wakitumika na wapigaji wa muda mrefu wa hapo bandarini. Kwa makusudi kabisa wakitambua namna wanavyowakwaza wafanyabiashara wa kweli wanaoagiza na kusafirisha mizigo bandarini kila siku.
Nilikuelewa vizuri sana nilipokusoma bandiko lako la mwanzo kabisa humu JF na kukuona jina ulilojipachika ili uwe mtoa fikra zako humu jukwaani.

Swala la kuidai Tanganyika, kama ujuavyo halikuanza na uwepo wa DP World hapa. Ila watu wa aina yako kila mara mnakimbilia upande huo wa kundi mnalojitambulisha nalo zaidi kuliko uTanzania unaotuhusu sote bila ya hayo makundi yanayotengeneza jamii yetu ya kiTanzania.
Tatizo linalotuandama ni hilo la vikundi, na hapa ni wazi kabisa upo hapa tokea uingie JF kwa sababu hiyo hiyo.

Hutetei maslahi ya Tanzania kwa ujumla wetu, bali wewe ni mshirika wa mpambano ya vikundi maalum.
 
Nilikuelewa vizuri sana nilipokusoma bandiko lako la mwanzo kabisa humu JF na kukuona jina ulilojipachika ili uwe mtoa fikra zako humu jukwaani.

Swala la kuidai Tanganyika, kama ujuavyo halikuanza na uwepo wa DP World hapa. Ila watu wa aina yako kila mara mnakimbilia upande huo wa kundi mnalojitambulisha nalo zaidi kuliko uTanzania unaotuhusu sote bila ya hayo makundi yanayotengeneza jamii yetu ya kiTanzania.
Tatizo linalotuandama ni hilo la vikundi, na hapa ni wazi kabisa upo hapa tokea uingie JF kwa sababu hiyo hiyo.

Hutetei maslahi ya Tanzania kwa ujumla wetu, bali wewe ni mshirika wa mpambano ya vikundi maalum.
Sio kweli, Tanganyika inatumiwa kama ngao ya kukwepesha mjadala mzima wa DPW. Wanajua wakija na mada nzito kipindi hiki cha rais mzenji watasikilizwa na mjadala mzima utahamia huko na suala la bandari litakuwa ni secondary tu.

Wameweza kuwapata baadhi ya watu wepesi wepesi na ndio hawa wanaosema SSH ni mwarabu anayetaka kuuza nchi hii kwa wajomba zake, huko UAE, Ni upuuzi mtupu.

Hayati JPM angekuwa hai mpaka muda huu tungetia saini na hawa hawa DPW na hakuna mtu ambaye angeweza kuinua mdomo wake kusema eti ni waarabu. Imejengwa hoja ya uarabu kwa sababu rais wetu wa sasa ni mzenji, angekuwepo mjenzi mwenyewe wa SGR muda mrefu tu tungeshamaliza hii biashara.
 
Sio kweli, Tanganyika inatumiwa kama ngao ya kukwepesha mjadala mzima wa DPW. Wanajua wakija na mada nzito kipindi hiki cha rais mzenji watasikilizwa na mjadala mzima utahamia huko na suala la bandari litakuwa ni secondary tu.

Wameweza kuwapata baadhi ya watu wepesi wepesi na ndio hawa wanaosema SSH ni mwarabu anayetaka kuuza nchi hii kwa wajomba zake, huko UAE, Ni upuuzi mtupu.

Hayati JPM angekuwa hai mpaka muda huu tungetia saini na hawa hawa DPW na hakuna mtu ambaye angeweza kuinua mdomo wake kusema eti ni waarabu. Imejengwa hoja ya uarabu kwa sababu rais wetu wa sasa ni mzenji, angekuwepo mjenzi mwenyewe wa SGR muda mrefu tu tungeshamaliza hii biashara.
Swala la Tanganyika limekuwepo muda mrefu sana, na Samia kalipa uzito zaidi kwa matendo yake mbalimbali, na siyo hilo la Bandari pekee.
Sasa swala hilo haliondoki tena, na wala halififishwi kwa njia yoyote.

Mtu unapokuwa kiongozi wa nchi, kitu muhimu cha kuzingatia katika uongozi wako ni pamoja na kutambua maswala yenye kuleta mtafaruku katika nchi unayoiongoza. Unakuwa mwangalifu sana na maswala hayo, ili unapoyagusa yasilete kutokuelewana ndani ya nchi yako. Kiongozi unapojifanyia tu mambo yako, kwa msukumo wa maslahi yako, au ya makundi yanayokuhimiza ufanye hayo, kiongozi huyo anakosa weledi katika uongozi wake.
Haya sasa ndiyo yaliyomfika Samia. Hakuna njia tena ya kuyafumbafumba.

Kuhusu hilo la JPM, unaweza kuwa sahihi kwa upande wa "kutia saini na hawa hawa DPW"; lakini kama ilivyo kawaida yenu kwa upande wa kundi hilo, mnajifanya kujisahaulisha tu kwamba kinachozungumziwa hapa siyo DPW.
JPM asingkubali "Makubaliano/Mkataba" unaowahusu hao DPW. Hili ndilo jambo muhimu zaidi, pamoja na nyinyi kutotaka lifahamike hivyo kwa kupotosha tu kwa maksudi.
 
Rais Samia leo July 17, 2023 amefungua mkutano wa wadau wa demokrasia barani Afrika unaowahusisha viongozi wakuu wastaafu mjini Arusha. Sehemu ya hotuba yake ameongelea namna ambazo si nzuri katika kufikisha hisia za wananchi.

Rais Samia: Kushindwa kwa Serikali kuhudumia mahitaji ya msingi imeibua malalamiko kwenye sehemu ya bara la Afrika. Baadhi kudharau na kufanya baadhi ya watu kwenye jamii kupinga na kudharau mamlaka ya Serikali kwa kuanzisha mifumo ambayo inatumia vurugu kuwalisha sauti ya wananchi.

Hii inajumuisha wanaharakati, vikundi vya kigaidi na maandamano. Na hii ni sehemu baadhi ya vipengele vya demokrasia kama uhuru wa kukusanyika na kutoa maoni vinatumika vibaya.

Pia, Soma=> Rais Samia akifungua Mkutano wa Wadau wa Demokrasia Barani Afrika wa Viongozi wakuu wastaafu, leo Julai 17, 2023


Hilo ni wazi kabisa na ni ukweli 100%.


Ni vikundi na watu wasikubalika wasiyo na na mvuto ndivyo huishia kuwa hivyo.
 
Swala la Tanganyika limekuwepo muda mrefu sana, na Samia kalipa uzito zaidi kwa matendo yake mbalimbali, na siyo hilo la Bandari pekee.
Sasa swala hilo haliondoki tena, na wala halififishwi kwa njia yoyote.

Mtu unapokuwa kiongozi wa nchi, kitu muhimu cha kuzingatia katika uongozi wako ni pamoja na kutambua maswala yenye kuleta mtafaruku katika nchi unayoiongoza. Unakuwa mwangalifu sana na maswala hayo, ili unapoyagusa yasilete kutokuelewana ndani ya nchi yako. Kiongozi unapojifanyia tu mambo yako, kwa msukumo wa maslahi yako, au ya makundi yanayokuhimiza ufanye hayo, kiongozi huyo anakosa weledi katika uongozi wake.
haya sasa ndiyo yaliyomfika Samia. Hakuna njia tena ya kuyafumbafumba.

Kuhusu hilo la JPM, unaweza kuwa sahihi kwa upande wa "kutia saini na hawa hawa DPW"; lakini kama ilivyo kawaida yenu kwa upande wa kundi hilo, mnajifanya kujisahaulisha tu kwamba kinachozungumziwa hapa siyo DPW.
JPM asingkubali "Makubaliano?Mkataba" unaowahusu hao DPW. Hili ndilo jambo muhimu zaidi, pamoja na nyinyi kutotaka lifahamike hivyo kwa kupotosha tu kwa maksudi.
Unapouongelea mkataba ni kama vile mstari fulani wa kwenye kitabu kitakatifu cha ZABURI, au Matendo ya Mitume.

Wanasheria kila siku wanaelimisha kuhusu huo huo mkataba tofauti na hawa kina Mwabukusi wanaochagua kifungu kimoja au viwili badala ya kuuchambua mkataba mzima ili mwananchi wa kawaida apate ufahamu sahihi.

Samia amekuwa ni rais msikivu sana tofauti na waliomtangulia, ameifufua demokrasia na kuleta uhuru na uwazi wa kusema chochote mtu anachojisikia.

Hafanyi kwa msukumo wa maslahi yake, sio kweli. Ni lazima mamlaka ya nchi iheshimu mchango wa wafanyabiashara kwa mfano. Ni lazima nchi iongozwe na weledi katika kila sekta.

Kuna hawa lobbyist wamekuwa na nguvu sana awamu hii, na yeye kama rais amewapa uhuru. Sioni kama hilo ni kosa au ni udhaifu wa uongozi wake.

Hayupo ikulu kuridhisha kila mtu kutoka katika kila taasisi, yupo pale kutimiza zile ahadi zote ambazo CCM waliziahidi kupitia ilani ya uchaguzi. Na anazitimiza moja baada ya nyingine.

Ndio maana wakubwa wa zile taasisi nyeti za kiserikali hakutaka kuwabadilisha, alitaka wamalize kazi walizoanza awamu ya tano. Hata salamu ya Kazi iendelee ni tafsiri ya hali halisi aliyoachiwa na mtangulizi wake hayati JPM.
 
Back
Top Bottom