Rais Samia unajiandalia majuto ambayo hutayasahahau kwenye maisha yako ya kisiasa

Rais Samia unajiandalia majuto ambayo hutayasahahau kwenye maisha yako ya kisiasa

Mie nilisema mapema, Mh. Rais wangu SSH achana na wapinzani, piga kazi, hao watukuzodoa, watakudharau, watakutukana, watakuona huna maana hata uwafanyie nini, Mh. Rais akianza kutaka kuwadhirisha wapinzani ni sawa na kujaza maji gunia.

Umeona Lissu alivyogeuka, umeenda kumuona, umempatia passport, umeahidi uso kwa uso kushughulikia maslahi yake aliyokuwa analilia kutwa, bado anasema ww sio alivyokufikuria, kasema vibaya sana juzi kati ulivyokutana na ile tume ya kutoa maoni ya vyama vya siasa.

Lissu au Mbowe hata ufanye nini, ni bure kabisa, huwezi kuwaridhisha. Achana nao. Umeona juzi Mbowe kwenye jukwaa akikunanga.
Ndio siasa zilivyo ni lazima kiongozi uwe na ngozi ngumu. Ni wapinzani hawawezi kukuunga mkono mpaka suala liwe la wazi sana ambalo hawawezi kulipinga.

Pia tukumbuke kuwa roho mbaya huzaa mabaya baadae, cha muhimu ni kuwa wavumilivu siku zote. Kumbuka SSH kachukua pesa nyingi za wazungu hivyo kwa namna moja ama nyingine analo deni la kuongoza nchi yenye haki na usawa kwa hao hao wahisani.
 
Mhe. Rais wewe ni mzoefu kwenye siasa za Tanzania. Kwa sasa ni kama unatafuta huruma ya wapinzani na unafanya vya kuwafurahisha lakin jua hii kitu itakugharimu

Kuachiwa kwa Mbowe, kukutana na Lisu ubeligiji, kujipanga kuruhusu mikutano ya kisiasa nk yote unatafuta kuonekana unajali ila ujue wapinzani hawaonagi jema.

Lisu sasa anademand utoe kauli ya kumkaribisha nyumbani na kwamba atakuwa salama, ni kama anakuamuru vile

Mbowe iko siku atasimama jukwaani na kukutukana live

Stay tuned hutaamini kama ni wao. Ule msemo wa shukrani ya punda unatimizwa vizuri na hao jamaa
Hatuna compromise kwenye haki za watu. Mnaojiona kwa kuwa mpo CCM mnafaidika sana mnajidanganya sana na mnajivika ujinga.

Nchi hii ni moja, ubovu wa siasa unapelekea ubovu wa serikali, na serikali ikiwa mbovu, kila kitu katika nchi kitakuwa kibovu.

Madhara ya Ubovu wa nchi hayachagui vyama. Wote mtasoma elimu duni, mtaamrishw na wala rushwa na mafisadi, mtapigwa na ugumu wa maisha, mtakosa huduma hata zile za kawaida kabisa kama maji, umeme, huduma za matibabu na madawa hospitalini, mtauliwa kwa sumu (Mto Mara), mtaporwa mali zenu mlizozitolea jasho, mtaishi kwenye makazi holela, nk.

Kwa ufupi, mtakufa mkiwa mmechoka sana, na mbinguni huenda msifike kwa kuwa mlikubali kuishi chini ya mfumo wa kishetani (unaoamini katika kuwanyima watu haki) huku duniani.

Taifa linalotaka kuendelea halipaswi kuongozwa kwa uongo uongo na ujanja ujanja kama CCM inavyofanya.

Chini ya hawa waliopo na wanaowashabikia, nchi itachelewa sana kupiga hatua ya kimaendeleo.
 
Back
Top Bottom