Rais Samia Usiache Kufanya Haya katika Kipindi cha Uongozi Wako

Rais Samia Usiache Kufanya Haya katika Kipindi cha Uongozi Wako

Dan Zwangendaba

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2014
Posts
5,814
Reaction score
8,118
Miongoni mwa mambo makubwa atakayokumbukwa nayo Rais wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Kikwete ni ujenzi wa shule za Kata na Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma. Licha ya changamoto zilizopo, bado wazo la ujenzi wa shule ya sekondari kila kata limekuwa na msaada mkubwa kwenye jamii tofauti na huko nyuma. Na kwa upande wa Chuo Kikuu cha Dodoma, hakika ile ni legacy ya milele kwa comrade Jakaya.

Rais Samia naye anaonekana kuipenda sekta ya Elimu kwa ujumla wake na huenda hii inatokana na kauli yake aliyoitoa hivi karibuni alipoulizwa unataka kuiona Tanzania ya namna gani na yeye kusema angependa kuiona Tanzania yenye watu wenye uelewa na maarifa/ujuzi (skilled and knowledgeable society). Hili ni jawabu mujarabu kabisa.

Msingi wa maendeleo tunayoyaona leo Ulaya, Amerika, East Asian countries, China, Japan na kwingineko, SIRI yake kubwa ni kutengeneza jamii yenye ujuzi na uelewa. Full stop. Na kwa hakika, jamii yetu ya kitanzania kama kuna biggest "binding constraint" inayodumaza maendeleo ya Tanzania basi ni watanzania wenyewe. Uelewa, maarifa, ujuzi, nidhamu na yanayohusiana na hayo ni tatizo kubwa kwa jamii ya Kitanzania. Dawa ya matatizo haya ni Elimu tu, si kingine.

Rais Samia ameanza kwa vitendo safari ya kuijenga jamii ya kitanzania yenye uelewa na ujuzi wa mambo kwa kufanya uwekezaji mkubwa kwenye ujenzi wa miundombinu ya elimu na upatikanaji wa vifaa vya elimu, ikiwa pamoja na ujenzi wa vyuo vya ufundi kwa kila Wilaya. Sambamba na hilo Rais Samia ameshaanza kujenga Chuo Kikuu cha TEHAMA kule Dodoma. Natamani chuo hiki kiwe katika kiwango cha "world class" vifanane na vyuo kama Hong Kong University of Science and Technology (HKUST), kule Hong Kong au Georgia School of Technology (Georgia Institute of Technology) aka Georgia Tech cha Marekani. Ujenzi wa vyuo vya namna hii utaleta ubunifu katika jamii ya Kitanzania.

Ombi na ushauri sasa kwa Mama. Katika jitihada hizohizo, tafadhali usiache kujenga vyuo vikuu viwili, kimoja Mtwara na kingine Bagamoyo. Cha Mtwara kiwe maalum kwa masuala ya Gesi na bidhaa za petrol kinaweza kuitwa Mtwara University of Gas and Petroleum Products. Bagamoyo ni kutekeleza ule mpango wa siku nyingi wa kuboresha chuo cha Mbegani na hiki kinaweza kuitwa Bagamoyo University of Fisheries and Marine Products (BUF).

Kwanini vyuo hivi? Ni kwasababu katika hayo maeneo hayo tuna FURSA (potential) ya kutosha ambapo kuna wigo mpana wa kutafiti na kuzalisha brains zitakazoweza kusaidia nchi kuanzishwa kwa projects nyingi na kuleta ajira kwa watanzania. Huko kuna utajiri wa kutisha. Bahari ina mambo mengi na tafiti zake still ni highly demanded duniani.
Kuwa na ukanda wa Bahari mrefu wa aina yetu (takribani km 1400+) si jambo la afya kutokuwa na chuo cha kisasa Ili kuchochea tafiti katika maeneo hayo. Halikadhalika, ni wakati sasa wa kuandaa vijana wenye skills katika maeneo ya Gas na petro- industries na mazao yake.

Ukifanya haya, utakuwa ungeacha alama ya milele kwa nchi yako hii na Rais ajaye tutamuomba ajenge vyuo vya michezo kila Wilaya Ili kuitumia fursa ya Dunia ya kuzalisha wanamichezo katika fani mbalimbali. Aisha anaweza kujenga Chuo Kikuu pia cha michezo na ingefaa chuo hiki kijengwe Arusha au Manyara.

Ni jambo la aibu kila siku kuwaona Kenya, Ethiopia kwenye riadha na kuwaona kwa wingi kina Mane, Kanoute nk. Utajiri ulioko kwenye michezo ni mkubwa na hauna dalili ya kuporomoka kwa utajiri huo.
Kazi iendelee.
 
Miongoni mwa mambo makubwa atakayokumbukwa nayo Rais wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Kikwete ni ujenzi wa shule za Kata na Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma. Licha ya changamoto zilizopo, bado wazo la ujenzi wa shule ya sekondari kila kata limekuwa na msaada mkubwa kwenye jamii tofauti na huko nyuma. Na kwa upande wa Chuo Kikuu cha Dodoma, hakika ile ni legacy ya milele kwa comrade Jakaya.

Rais Samia naye anaonekana kuipenda sekta ya Elimu kwa ujumla wake na huenda hii inatokana na kauli yake aliyoitoa hivi karibuni alipoulizwa unataka kuiona Tanzania ya namna gani na yeye kusema angependa kuiona Tanzania yenye watu wenye uelewa na maarifa/ujuzi (skilled and knowledgeable society). Hili ni jawabu mujarabu kabisa.

Msingi wa maendeleo tunayoyaona leo Ulaya, Amerika, East Asian countries, China, Japan na kwingineko, SIRI yake kubwa ni kutengeneza jamii yenye ujuzi na uelewa. Full stop. Na kwa hakika, jamii yetu ya kitanzania kama kuna biggest "binding constraint" inayodumaza maendeleo ya Tanzania basi ni watanzania wenyewe. Uelewa, maarifa, ujuzi, nidhamu na yanayohusiana na hayo ni tatizo kubwa kwa jamii ya Kitanzania. Dawa ya matatizo haya ni Elimu tu, si kingine.

Rais Samia ameanza kwa vitendo safari ya kuijenga jamii ya kitanzania yenye uelewa na ujuzi wa mambo kwa kufanya uwekezaji mkubwa kwenye ujenzi wa miundombinu ya elimu na upatikanaji wa vifaa vya elimu, ikiwa pamoja na ujenzi wa vyuo vya ufundi kwa kila Wilaya. Sambamba na hilo Rais Samia ameshaanza kujenga Chuo Kikuu cha TEHAMA kule Dodoma. Natamani chuo hiki kiwe katika kiwango cha "world class" vifanane na vyuo kama Hong Kong University of Science and Technology (HKUST), kule Hong Kong au Georgia School of Technology (Georgia Institute of Technology) aka Georgia Tech cha Marekani. Ujenzi wa vyuo vya namna hii utaleta ubunifu katika jamii ya Kitanzania.

Ombi na ushauri sasa kwa Mama. Katika jitihada hizohizo, tafadhali usiache kujenga vyuo vikuu viwili, kimoja Mtwara na kingine Bagamoyo. Cha Mtwara kiwe maalum kwa masuala ya Gesi na bidhaa za petrol kinaweza kuitwa Mtwara University of Gas and Petroleum Products. Bagamoyo ni kutekeleza ule mpango wa siku nyingi wa kuboresha chuo cha Mbegani na hiki kinaweza kuitwa Bagamoyo University of Fisheries and Marine Products (BUF).

Kwanini vyuo hivi? Ni kwasababu katika hayo maeneo hayo tuna FURSA (potential) ya kutosha ambapo kuna wigo mpana wa kutafiti na kuzalisha brains zitakazoweza kusaidia nchi kuanzishwa kwa projects nyingi na kuleta ajira kwa watanzania. Huko kuna utajiri wa kutisha. Bahari ina mambo mengi na tafiti zake still ni highly demanded duniani.
Kuwa na ukanda wa Bahari mrefu wa aina yetu (takribani km 1400+) si jambo la afya kutokuwa na chuo cha kisasa Ili kuchochea tafiti katika maeneo hayo. Halikadhalika, ni wakati sasa wa kuandaa vijana wenye skills katika maeneo ya Gas na petro- industries na mazao yake.

Ukifanya haya, utakuwa ungeacha alama ya milele kwa nchi yako hii na Rais ajaye tutamuomba ajenge vyuo vya michezo kila Wilaya Ili kuitumia fursa ya Dunia ya kuzalisha wanamichezo katika fani mbalimbali. Aisha anaweza kujenga Chuo Kikuu pia cha michezo na ingefaa chuo hiki kijengwe Arusha au Manyara.

Ni jambo la aibu kila siku kuwaona Kenya, Ethiopia kwenye riadha na kuwaona kwa wingi kina Mane, Kanoute nk. Utajiri ulioko kwenye michezo ni mkubwa na hauna dalili ya kuporomoka kwa utajiri huo.
Kazi iendelee.
Chuo Cha Masuala ya gas kutajengwa Lindi na hili limepitishwa..

Hoja ya chuo Cha Uvuvi Lina make sense ila mambo ya Uvuvi hayahitaji kuwa na chuo Kikuu bali vyuo vya Kati ngazi ya Diploma kushuka chini ..

Kinachotakiwa ni kuviimarisha kwenye tafiti na utaalamu .
 
Chuo Cha Masuala ya gas kutajengwa Lindi na hili limepitishwa..

Hoja ya chuo Cha Uvuvi Lina make sense ila mambo ya Uvuvi hayahitaji kuwa na chuo Kikuu bali vyuo vya Kati ngazi ya Diploma kushuka chini ..

Kinachotakiwa ni kuviimarisha kwenye tafiti na utaalamu .
Hilo la chuo cha masuala ya gas kama limeshapitishwa ni jambo jema ila kisijengwe Lindi badala yake kijengwe Mtwara (kwa maoni yangu). Ukuaji wa miji wakati mwingine pamoja na people-based lakini kina natural-based environment. Tunahitaji kuwa na plan ya kuifanya miji yetu iwe majiji siku hata siku. Kwa mazingira ya Kusini, Mtwara imejitokeza kuwa hub na kuweza kuwa Jiji kwa siku zijazo, ila siioni hiyo fursa kwa Lindi. Kama hiki chuo kitajengwa Mtwara itakifanya kiwe vibrant na kuufanya mji wa Mtwara kuwa Jiji kwa siku za usoni. Ubinafsi uwekwe pembeni, tujenge hiki chuo Mtwara ambapo tayari kuna Bandari, Uwanja wa Ndege, Benki Kuu na Taasisi nyingine kubwa tofauti na Lindi. Tuifanye Mtwara kuwa Hub ya Kusini kama ilivyo Arusha Hub ya Kaskazini, Mbeya Hub ya Nyanda za Juu, Mwanza hub ya Kanda ya Ziwa. Tusifanye kosa hili, tuongeze miundombinu na kuifanya Mtwara liwe Jiji kwa kujenga Taasisi kubwa kubwa kama vyuo, Hospital, Kumbi za mikutano za kimataifa na makao makuu ya Taasisi kadhaa kwa kanda ya Kusini. LNG plant na associated industries kwa Lindi inatosha chuo cha masuala ya Gas, chondechonde msijenge Lindi. Kitakuwa dormant mnoo.

Kuhusu chuo Kikuu cha Uvuvi, kimsingi shughuli zote zinahitaji kada za kati (ufundi nk) lakini pia zinahitaji ubobezi katika utafiti ili kulisha (to feed) hivyo vyuo vya Kati. Chuo pendekezwa ni kuwa Taasisi kubwa ya kufanya tafiti katika masuala ya Uvuvi na mazao ya Bahari kwa ukamilifu wake bila kuathiri zaidi kuboresha vyuo vya kati vya masuala ya Uvuvi. Kwanza natumai, vyuo vya VETA katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Mwanza, Pwani, Kigoma, Lindi, Mtwara, na maeneo yote ya Zanzibar vitakuwa na kozi za masuala ya Uvuvi. So, kwa maoni yangu tunahitaji Taasisi kubwa sana ya masuala ya Uvuvi na na mazao ya Bahari itakayokuwa na uwezo wa kutafiti, kubuni na hata kuzalisha vifaa vya Uvuvi kama Boti na engine zake. Nazungumzia chuo cha kubuni projects za kufanywa kimataifa, nazungumzia chuo cha kuzalisha wabobezi wa masuala ya Uvuvi na Bahari wataoweza kutumika pembe zote za Dunia, nazungumzia chuo kitakachoweza kuzalisha fisheries systems; ambapo naamini vyuo vya chini na kati havina uwezo huo.
 
Katiba mpya ndio itakuwa legasi yake ya kudumu isiyo na utata wowote.
Miongoni mwa mambo makubwa atakayokumbukwa nayo Rais wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Kikwete ni ujenzi wa shule za Kata na Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma. Licha ya changamoto zilizopo, bado wazo la ujenzi wa shule ya sekondari kila kata limekuwa na msaada mkubwa kwenye jamii tofauti na huko nyuma. Na kwa upande wa Chuo Kikuu cha Dodoma, hakika ile ni legacy ya milele kwa comrade Jakaya.

Rais Samia naye anaonekana kuipenda sekta ya Elimu kwa ujumla wake na huenda hii inatokana na kauli yake aliyoitoa hivi karibuni alipoulizwa unataka kuiona Tanzania ya namna gani na yeye kusema angependa kuiona Tanzania yenye watu wenye uelewa na maarifa/ujuzi (skilled and knowledgeable society). Hili ni jawabu mujarabu kabisa.

Msingi wa maendeleo tunayoyaona leo Ulaya, Amerika, East Asian countries, China, Japan na kwingineko, SIRI yake kubwa ni kutengeneza jamii yenye ujuzi na uelewa. Full stop. Na kwa hakika, jamii yetu ya kitanzania kama kuna biggest "binding constraint" inayodumaza maendeleo ya Tanzania basi ni watanzania wenyewe. Uelewa, maarifa, ujuzi, nidhamu na yanayohusiana na hayo ni tatizo kubwa kwa jamii ya Kitanzania. Dawa ya matatizo haya ni Elimu tu, si kingine.

Rais Samia ameanza kwa vitendo safari ya kuijenga jamii ya kitanzania yenye uelewa na ujuzi wa mambo kwa kufanya uwekezaji mkubwa kwenye ujenzi wa miundombinu ya elimu na upatikanaji wa vifaa vya elimu, ikiwa pamoja na ujenzi wa vyuo vya ufundi kwa kila Wilaya. Sambamba na hilo Rais Samia ameshaanza kujenga Chuo Kikuu cha TEHAMA kule Dodoma. Natamani chuo hiki kiwe katika kiwango cha "world class" vifanane na vyuo kama Hong Kong University of Science and Technology (HKUST), kule Hong Kong au Georgia School of Technology (Georgia Institute of Technology) aka Georgia Tech cha Marekani. Ujenzi wa vyuo vya namna hii utaleta ubunifu katika jamii ya Kitanzania.

Ombi na ushauri sasa kwa Mama. Katika jitihada hizohizo, tafadhali usiache kujenga vyuo vikuu viwili, kimoja Mtwara na kingine Bagamoyo. Cha Mtwara kiwe maalum kwa masuala ya Gesi na bidhaa za petrol kinaweza kuitwa Mtwara University of Gas and Petroleum Products. Bagamoyo ni kutekeleza ule mpango wa siku nyingi wa kuboresha chuo cha Mbegani na hiki kinaweza kuitwa Bagamoyo University of Fisheries and Marine Products (BUF).

Kwanini vyuo hivi? Ni kwasababu katika hayo maeneo hayo tuna FURSA (potential) ya kutosha ambapo kuna wigo mpana wa kutafiti na kuzalisha brains zitakazoweza kusaidia nchi kuanzishwa kwa projects nyingi na kuleta ajira kwa watanzania. Huko kuna utajiri wa kutisha. Bahari ina mambo mengi na tafiti zake still ni highly demanded duniani.
Kuwa na ukanda wa Bahari mrefu wa aina yetu (takribani km 1400+) si jambo la afya kutokuwa na chuo cha kisasa Ili kuchochea tafiti katika maeneo hayo. Halikadhalika, ni wakati sasa wa kuandaa vijana wenye skills katika maeneo ya Gas na petro- industries na mazao yake.

Ukifanya haya, utakuwa ungeacha alama ya milele kwa nchi yako hii na Rais ajaye tutamuomba ajenge vyuo vya michezo kila Wilaya Ili kuitumia fursa ya Dunia ya kuzalisha wanamichezo katika fani mbalimbali. Aisha anaweza kujenga Chuo Kikuu pia cha michezo na ingefaa chuo hiki kijengwe Arusha au Manyara.

Ni jambo la aibu kila siku kuwaona Kenya, Ethiopia kwenye riadha na kuwaona kwa wingi kina Mane, Kanoute nk. Utajiri ulioko kwenye michezo ni mkubwa na hauna dalili ya kuporomoka kwa utajiri huo.
Kazi iendelee.
 
Katiba mpya ndio itakuwa legasi yake ya kudumu isiyo na utata wowote.
Ukiwa na Katiba halafu atokee kiongozi kama malaika wa Chato hiyo Katiba itakuwa na msaada gani. Legacy kubwa ni kuacha jamii inayojitambua
 
Back
Top Bottom