Wanasiasa wanadai haki zao,
Wakulima, wafugaji na wafanyakazi hawana mtetezi.
Katiba mpya ni gharama siyo sawa na kuandika vitabu vyako uchwara vya kijasusi. Huwezi kuacha kutekeleza miradi ya kimkakati au kupelekea watu maji na umeme ukakimbilia kuandika Katiba Mpya kwa ajili ya kuwaridhisha watu fulani kwa maslahi yao ya kisiasa.
Kikwete alivyokubali mchakato wa Katiba mpya tuliona madhara yake, fedha zilitumika nyingi lakini pia baadhi ya watu hawakukubaliana na maoni ya wengi wakataka ya kwao ya wachache ndo yazingatiwe. Mwisho wa siku taifa likasimama, tukaingia kwenye mgogoro.
Uzuri Mhe. Rais anajua huu mchakato ulivyo kwasabbu alishiriki kikamilifu. Kwahiyo, anajua kinachokwenda kutokea ni KUPOTEZA MUDA NA RASILIMALI huku mambo mengi ya msingi yakisimama.
After all, mchakato wa Katiba mpya ulishakamilika na Katiba inayopendekezwa tayari ipo, kilichobaki ni kupigiwa kura tu. Sasa sijui kinachodaiwa hapa ni nini?
Sent from my SM-A730F using JamiiForums mobile app
Mkuu katba nzr ni ipi?? Yaan toa mfano hyo katiba mpya unayo itaka iweje?? Eleza tu kwa lugha rahisi..
1)-Katiba mnataka nyie wanasiasa Mnahis labda ndo mtakuwa viongoz lkn sisi Wananchi Tunataka Maendeleo Na huduma za kijamii zpatikane...
2)-Mchakato wa Katiba enz za JK mliuharibu Nyie Ukawa mlipotoka Bungen..
Hakuna muda wa kupoteza pesa Zetu Wananchi..
3)-Kama Katiba Rais ataawaachia Wataalam washauri iweje Cyo Nyie Wanasiasa Njaa Mnaotaka Posho za Bunge la Katiba
Mimi napenda nchi yetu iwe na katiba mpya, na isiyo na mafungamano kwa namna yoyote ile na ccm! Kwanini?
Kwa sababu katiba ya mwaka 1977 iliandaliwa mahsusi kwa ajili ya Tanzania ya chama kimoja, na tena cha kijamaa! Yaani ccm.
Ni katiba hii ndiyo iliyo kifanya chama cha mapinduzi kuwa chama dola, lakini pia ni katiba hii hii ndiyo iliyompa mamlaka makubwa Rais kiasi cha kumfanya kuwa Rais Mfalme (Imperial President).
Katiba mpya imependekeza kupunguzwa kwa mamlaka ya Rais! Na pia iliweka mazingira mazuri ya nchi kuwa na tume huru ya uchaguzi, kuliko hii ya sasa ambayo Rais wa nchi anamteua yeyote kuwa mwenyekiti/mkurugenzi wa tume! Hata kama ni mwanachama wa ccm! Ushahidi uko wazi!
Ni katiba hii hii inayotambua mpaka leo vyeo vya ulaji na tulivyorithi kwa wakoloni vya ukuu wa mikoa, wilaya, nk! Katiba mpya (na hasa ile rasimu ya Jaji Warioba) ililenga kupunguza matumizi mbalimbali yasiyo na ulazima serikalini. Mfano kupunguza ukubwa wa bunge, nk.
Leo hii tuna bunge kubwa na lisilo na tija yoyote ile. Tuna wabunge wa majimbo, wabunge wa viti maalum, wabunge wa kuteuliwa na Rais, wabunge kutoka Zanzibar, nk. Kwa ufupi tu, katiba mpya kwa upande wangu ina tija zaidi kuliko hii ya sasa ya mwaka 1977, ambayo kimsingi inaipendelea zaidi ccm na pia inawaongezea tu mzigo watanzania walipa kodi, kwenye uendeshaji wa serikali.
Wanaodai katiba mpya sio wananchi ni wanasiasa.
Na unapodai katiba mpya sio conundrum ya kuku na yai (kipi kimetangulia duniani). Ideas zinaanza katiba iweje, then mchakato unaweza anzishwa.
Wahusika (wanasiasa) wanao push hii agenda sasa hivi wangekua wana highlight areas zinazo wasukuma kudai katiba mpya, mfano:
Ni mfumo gani wa decentralisation (ata kwa bara tu) wanataka utumike na kwanini uliopo unamapungufu based on management perpspectives.
Limitations zipi wanataka kuona kati ya viongozi na wananchi kwenye madaraka yao, wakionyesha mapungufu ya sasa.
Rights zipi za wananchi (realistically) uwezi kusema kila mkulima apewe hela ya pembejeo that is unrealistical.
Etc na mambo yanayotoa legitimising of powers, protection of freedom, government stability and so forth with the principles of national constitution.
Lakini uwezi kuamka asubuhi ukadai tu katiba ukiulizwa iweje unasema hujui tuwaachie wananchi; wananchi kweli wanajua mambo ya sheria au hata wamedai katiba?
Hili swala la constitution ni kupoteza muda ata kuli entertain ni usumbufu scrap kama alivyofanya Magufuli.
You can’t please everyone it’s impossible.
kama ikitokea wizi wa mali ya umma na ubadhilifu ukarudi tena, au kujipatia fursa kwa hila na upendeleo balada ya fair process. Hilo litakuwa doa kubwa. Kuna mambo yakifanyika huwa yanaweza kuangusha falme hata kubwa kubwa, ikiwemo hili la rushwa na upendeleo
Umesema kweli kabisa, lakini chama sio bendera mkuu ni watu wenye chama chao pamoja na ninyi mashabiki wa haki na siasa, chama kinahitaji kuungwa mkono na watu wote wenye uchungu na nchi yao, badala yake mnasubiri mfanyiwe na viongozi wa vyama, haiwezekani. Mfano mzuri ni harakati za ukuta mlivyoitwa barabarani nani alitokea?Tatizo mlimsifia sana mkasahau kama huyo ni kiongozi wa CCM, vyovyote iwavyo maslahi yake na chama chake lazima ayaweke mbele, sasa mnasubiri hisani toka kwake kwa kumbembeleza hata kama anavunja sheria wazi, mnatakiwa muamke sasa mjue ni njia gani mtaitumia kudai haki yenu, muache na ule ushamba wa mapambio yasiyo na maana.
Let’s just say unachanganya apples and pears.
Raisi/Serikali ina mandate ya kuchagua priority za nchi kama akiamua kununua ndege regardless of weaknesses on the decision by electing him we have bestowed him/her those powers.
Any president is not always going to make the best decision for the nation that’s why a constitution gives time to choose after a time.
The latter part in conclusion ni kwamba unazungumzia influence za raisi kwenye kusimamia uwajibikaji wa teuzi zake; I can agree there is a need of mechanimism to eliminate protectionism ya raisi. Lakini jambo hilo aliitaji katiba mpya but changing areas on how constitution could be amended.
Listen realistically katiba is an evolving document either codified or uncodified depending on the needs of a nation given the time; kwa sababu moja tu sababu za kuweka mambo kadhaa kwenye katiba zina badilika with time and evolution of several things such as morality and interpretation of rights.
Tatizo la watu wanaodai katiba mpya don’t have an argument zaidi ya kudai mpya wanaweza sema chochote before you know watakwambia we need a federal constitution kwa sababu US is doing so. Waulize sasa managerial system zake hawajui lolote zaidi ya kuleta fujo tu.
Mama anatakiwa kuifunga hii chapter akutakuwa na katiba mpya watanyamaza tu maana hiyo sio hoja ya wananchi.
Wala sio kosa kumsafisha mtu kama anatenda vizuri. Na badp ji wajibu wetu kumshauri pale inapobidiTatizo mlimsifia sana mkasahau kama huyo ni kiongozi wa CCM, vyovyote iwavyo maslahi yake na chama chake lazima ayaweke mbele, sasa mnasubiri hisani toka kwake kwa kumbembeleza hata kama anavunja sheria wazi, mnatakiwa muamke sasa mjue ni njia gani mtaitumia kudai haki yenu, muache na ule ushamba wa mapambio yasiyo na maana.
masalia ya jiwe mnahangaika sana.kama hawa ndio think tankers wetu hata samia hana haja ya kutusikiliza
You can do that but you have to remember sababu moja nchi zinakiongozi mkuu mmoja ni kwa sababu tunahitaji mtu wa kufanya decision kwa niaba ya nchi ya wote ipo ivyo duniani kote.
Kazi ya bunge ni kutunga sheria sio kumpangia raisi, wanachoweza kufanya ni ku challenge maamuzi ya raisi based on law. But then there is politics uwezi kuondoa factor hata bungeni maamuzi ya raisi kama yanabaraka ya wabunge wake and if they form the majority ni halali regardless of your feelings.
Tatizo lenu ni kulazimisha mambo nje ya siasa; mambo mengi mnayo mlaumu nayo JPM ni ya mfumo wa CCM kushinda katiba wakibariki wao inatosha that’s how party politics work.
Ni kama CDM walivyoamua Mbowe afanye atakavyo that’s part politics; the difference raisi is doing it national level. Sasa uwezi pangia maamuzi ya chama cha siasa wakishabariki.
Hila sakata la katiba ni waste of time; CCM wawapelekee jaji Werema sioni wa kujibizana nae kwenye constitutional law.
kwani hiyo iliyopo inaleta ugali mezani? Umeambiwa tunatafuta ugali hapo? we need justice and rights that we deserve. Pamoja na kulaaniwa na kulaanika hadi jiwe na genge lake wanateketea bado hamjifunziWewe katiba mpya haikuletei ugali mezani, wananchi hatutaki siasa tunataka pesa.
Ila wewe huwezi kuelewa maana kila kitu anakuhudumia mumeo
Katiba mpya sio vita vya marungu na mawe inadaiwa mahali popoteTundu Lisu anadai katiba akiwa Ubelgiji!
Una point nzuri sana mimi ni CCM na mwana fikra huru. Mtazamo ama fikra yaweza kuwa katika namna ifuatayo.Mh Rais, Kwasiku 100 ulizoongoza nchi zimekuwa za kutukuka sana, Taifa limepumua na kuonyesha mageuzi makubwa sana, Kwahakika nakupongeza sana sana, Umewathibitishia wazi unaweza kwa wale waliodhani huwezi kuongoza nchi.
Jambo la msingi leo naomba kuzungumzia kikao chako cha jana, ambapo nimesikiliza mazungumzo yako na Wahariri vya Vyombo vya habari nchini ambayo ni mazuri sana,
Pamoja na uzuri huo, Majibu yako kuhusu shughuli za kisiasa na mchakato wa Katiba Mpya yamenitia hofu huko tuendako kama kweli tutatibu tatizo la nchi ama tunafunika kombe la utawala uliopita.
Kimsingi jana tulitaraji utengue AMRI YA KIRAIS iliyotolewa na utawala uliopita kuhusu kusitisha shughuli za kisiasa (za wapinzani). Lakini pia tulitaraji utupe mwelekeo wa lini mchakato wa katiba mpya utaanza, Japo la Katiba ulilijibu lakini jibu lake limekuwa lilelile alilotwambia Rais Magufuli wakati anaingia madarakani.
Suala la shughuli za kisiasa ni la kikatiba na kisheria sio la hisani ya Rais, Nimelazimika kwenda kusoma sheria ya vyama vya siasa iliyofanyiwa marejeo 2019, kifungu cha 11, haki ya chama cha siasa kufanya mikutano ipo sio hisani ya mtu yoyote bali ni utekelezaji wa sheria tu.
Sasa rais wangu UMEAPA KUILINDA KATIBA NA SHERIA ZAKE, Ninakuomba sana, liangalie hili kwa umakini, huenda kuna wasaidizi wanakupotosha kuwa shughuli za vyama vya siasa zinakwamisha maendeleo, Hao wanakugombanisha na umma.
Watanzania sisi ukitaka tusikusumbue tuache tuongee, tulie na kucheka, tutanyamaza wenyewe, lakini sio utulazimishe tuongee, utulazimishe tulie wala utulazimishe kunyamaza. Kwahakika tutakusumbua kwelikweli, si jela wala mahakama havitatutibu. Shahidi utawala uliopita.
Labla nirejee nyuma kidogo, Msingi wa mpasuko wa taifa hili hadi kufika kuvuruga uchumi na mengineyo, ulitokana mwanzo kabisa kuzuia haki za watu kukutana na kutoa mawazo yao ambayo ni haki ya kikatiba na kisheria, Waliozuia walikuja na hoja hiyohiyo ambayo leo Rais umesema kuwa unanyoosha nchi.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete alipoanzisha mchakato wa Katiba nchi ilikuwa hivihivi wala hakuwa na kigezo cha nchi imenyooka au imepinda, na alipoahirisha nchi ilibaki vilevile, Mchakato wa Katiba mpya hauwezi kuzua miradi ya maendeleo nchini wala hauwezi kukuzuia Mh Rais kuendesha nchi. Vivyo hivyo shughuli za kisiasa.
Katiba mpya ndio msingi wa mambo yote katika nchi, Tukipata katiba mpya itaondoa kazi ya kunyoosha uchumi wa nchi unayoifanya leo Mh Rais kwakuwa hakuna atakayekuja kuipindisha nchi tena.
Na Yericko Nyerere
View attachment 1834432View attachment 1834433
Mkuu, unachoshangaa hapa si nilichouliza mimi hapo juuHivi wewe una kumbukumbu au huna?
Tume ya Warioba ilifanya kazi gani? Yaani huna hata ufahamu kuwa unachokiuliza, kilimalizwa na Tume ya Warioba?