Rais Samia, Watanzania kuruhusiwa kufanya kazi Kenya tuepushe na mtego huo

Rais Samia, Watanzania kuruhusiwa kufanya kazi Kenya tuepushe na mtego huo

Kuwekeza Kenya nishuguli pevu saaana kuliko kuwekeza Tanzania. Wakenya wanawinda ardhi . kumbukeni hata enzi za hayati, raisi wa Kenya aliwahisema watanzania ruksa kuoa Kenya . Mungu atupiganie
Tena mama anaona Rostam mwenyewe mwenye pesa zake wanavyomzingua sebuse sisi akina yakhee ? Mimi Nina marafiki kadhaa wakenya walikuja Tanzania kizembe tu na mitaji ya ngama mmojawapo alianzisha kibiashara kama vile vya forever living kuuza sijui virutubisho na ushauri nasaha sasa hivi ni milionea yaani ukienda ofisini kwake utakuta mitz kibao imejazana wengine wananunua vinavyoitwa virubisho sijui mchanganyiko wa miti shamba na vingine ambavyo hata wao wanaweza kujichanganyia tu huko mtaani wakatumia. Jamaa alichogundua ni kwamba watz wana stress nyingi kutokana na sababu mbalimbali na ni wazembe so ukienda kwake ni kama anakufundisha maisha kwa kisingizio cha ushauri nasaha basi unafanikiwa unaenda kuleta na likondoo jingine kama wewe ulivyokuwa yeye mfuko unaendelea kutuna.sasa mambo kama haya ni ngumu upande wa pili.
 
Mimi sioni mtego wowote hapo, Kama umeruhusiwa kwenda kufanya kazi kenya bila working permit bado vigezo vitazingatiwa lazima utakuwa na utambulisho wako wa wewe ni Nani?

Na sijaona sehemu wakisema ukanunue ardhi huko na wao pia siamini Kama wataruhusiwa kuja kununua ardhi huku, hayo ni mambo ya mahusiano ya kibiashara zaidi Ili kuchangamsha akili zetu na kuondoa uvivu wa watanzania na tunaogopa wasije Ili tuzidi kulala, wewe ukiwa na hela yako kenya ni sehemu ya kwenda kujifunza practical ya utengenezaji wa vitu au kuongeza thamani malighafi tulizonazo sasa hizo working permit huoni zitakukwamisha?

Angalia wenye mitaji wanavyo copy bidhaa kenya na kuzitengeneza hapa na sasa hivi tunawaita mamilionea, Sabuni za miche na unga, maziwa, viungo na jinsi ya kupaki, hebu twendeni kenya tukachue ujuzi tumepata hiyo nafasi, hata wao wakija watakuja na hela Kama ni nyumba watalipa kodi kwani watakuja kukaa huku bure? Na vigezo na mashariti vitazingatiwa huwezi kuambiwa ruhusa kufanya kazi wewe ukakimbilia kununua kiwanja.
 
Wakati wenyewe ardhi yote bado inamilikiwa na akina Lord Delamere na familia za kisiasa za akina Kenyata na oligarchs wengineo.

Cheza na watu wote lakini usicheze na Mkenya. Nilifanya kosa la kumtumia mmoja kama referee wangu kwenye kazi moja nzuri ajabu. Weeeh! Nilikosa ile kazi na nilipofuatilia memba mmoja wa hiring committee akaniambia kuwa kulikuwa na recommendation letter moja ilikuwa mbaya mno; na akamtaja jina yule Mkenya. Nilishangaa kwa sababu jamaa alikuwa mshikaji sana na tulikuwa tumefanya kazi pamoja sehemu mbalimbali duniani japo yeye alikuwa senior kidogo. Wana roho mbaya ajabu!
Duuuuh!!! Nimemkumbuka gafla jemadari na shujaaa wa Africa
 
Kuna maamuzi ambayo kihistoria unajua tu huo ni mtego mbaya sana! Hatuhitaji ruhusa kama hiyo ambayo ni nadharia tu! Kenya Mkikuyu hawezi kuajiliwa na Mluo. Mluo naye hawezi kuajiliwa na Mkikuyu. Ni hivyo hivyo kwa makabila mengine. Maana yake, hakuna ajira kwa M-TZ, labda kama ni kuzoa uchafu. Wakenya wanahofia TZ kiasi kwamba hawataki hata apewe ajira za ofisi za UN ambazo siyo za serikali yao. Mama Tibaijuka anaelwa alivyokuwa anapigwa vita na Wakenya. Wako tayari nafasi ichukuliwe na mtu wa nje ya EAC kuliko m-TZ.

Mtego huu uliwahi letwa hapa kwenye suala la ardhi eti waruhusiwe kumiliki ardhi TZ na wa-TZ waruhusiwe kumiliki ardhi Kenya. Ilishindikana maana TZ tulijua hakuna uwezekanao wa m-TZ kumiliki ardhi Kenya. Rais epuka mtego huo usio na faida kwa TZ.
Njoo uchukue dual-citizenship, uone ka hununui ardhi kulingana na uwezo wako. Nyie ndio Mh. Mama Samia anaongelea mbungeni kuwahusu. Mwache hiyo akili.
 
Mimi sioni mtego wowote hapo, Kama umeruhusiwa kwenda kufanya kazi kenya bila working permit bado vigezo vitazingatiwa lazima utakuwa na utambulisho wako wa wewe ni Nani? Na sijaona sehemu wakisema ukanunue ardhi huko na wao pia siamini Kama wataruhusiwa kuja kununua ardhi huku, hayo ni mambo ya mahusiano ya kibiashara zaidi Ili kuchangamsha akili zetu na kuondoa uvivu wa watanzania na tunaogopa wasije Ili tuzidi kulala, wewe ukiwa na hela yako kenya ni sehemu ya kwenda kujifunza practical ya utengenezaji wa vitu au kuongeza thamani malighafi tulizonazo sasa hizo working permit huoni zitakukwamisha? Angalia wenye mitaji wanavyo copy bidhaa kenya na kuzitengeneza hapa na sasa hivi tunawaita mamilionea, Sabuni za miche na unga, maziwa, viungo na jinsi ya kupaki, hebu twendeni kenya tukachue ujuzi tumepata hiyo nafasi, hata wao wakija watakuja na hela Kama ni nyumba watalipa kodi kwani watakuja kukaa huku bure? Na vigezo na mashariti vitazingatiwa huwezi kuambiwa ruhusa kufanya kazi wewe ukakimbilia kununua kiwanja.
Wewe mtu umesoma thrd inavyoweka wazi hali ya Kenya? Unawezaje kuitwa kufanyakazi kwenye nchi ya wenye tabia ya kutopenda wengine? anayekaribisha ni rais lakini wanaokuajili siyo rais. Utakwama tu!
 
Mimi sioni mtego wowote hapo, Kama umeruhusiwa kwenda kufanya kazi kenya bila working permit bado vigezo vitazingatiwa lazima utakuwa na utambulisho wako wa wewe ni Nani? Na sijaona sehemu wakisema ukanunue ardhi huko na wao pia siamini Kama wataruhusiwa kuja kununua ardhi huku, hayo ni mambo ya mahusiano ya kibiashara zaidi Ili kuchangamsha akili zetu na kuondoa uvivu wa watanzania na tunaogopa wasije Ili tuzidi kulala, wewe ukiwa na hela yako kenya ni sehemu ya kwenda kujifunza practical ya utengenezaji wa vitu au kuongeza thamani malighafi tulizonazo sasa hizo working permit huoni zitakukwamisha? Angalia wenye mitaji wanavyo copy bidhaa kenya na kuzitengeneza hapa na sasa hivi tunawaita mamilionea, Sabuni za miche na unga, maziwa, viungo na jinsi ya kupaki, hebu twendeni kenya tukachue ujuzi tumepata hiyo nafasi, hata wao wakija watakuja na hela Kama ni nyumba watalipa kodi kwani watakuja kukaa huku bure? Na vigezo na mashariti vitazingatiwa huwezi kuambiwa ruhusa kufanya kazi wewe ukakimbilia kununua kiwanja.
Haya unachozungumza ndio uhalisia wa huko Kenya?? Ni Kenya ipo hiyo?
Kenya mjaluo hataki hataa kumsikia mkikuyu achilia mbali mtanzania
Ukienda na kuondoka wa kwa sio shida, shida nenda kaishi rasmi.
Umesahau Jaguar na watu wake walivyotaka kuwatimua wamachinga wa kitanzania?
Imagine, wamachinga tu ambao hawapati chochote walikuwa wanawaonea wivu, Leo ije kuwa wewe kwenda kufanya kazi au kufungua kampuni kwao.
 
Kwa watu wenye akili na busara, kuna mambo mengi hutekelezwa bila kuzungumzwa au kuandikwa.
Uhusiano wa kimataifa ni muhimu lakini mambo yanavyozungumzwa na utekelezaji ni tofauti.
Kinachohitajika ni watendaji wenye akili nzuri kusimamia maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.
 
Njoo uchukue dual-citizenship, uone ka hununui ardhi kulingana na uwezo wako. Nyie ndio Mh. Mama Samia anaongelea mbungeni kuwahusu. Mwache hiyo akili.
Unatita, wewe ni Mkenya. Ununue ardhi wapi na ya nini? Ardhi ya kujenga nyumba utapata, sasa hiyo ndo inipeleke Kenya? Nataka ardhi ya kuzalisha maua na kahawa, ipo? Nani akuuzie. Acha udanganyifu.
 
Kuna maamuzi ambayo kihistoria unajua tu huo ni mtego mbaya sana! Hatuhitaji ruhusa kama hiyo ambayo ni nadharia tu! Kenya Mkikuyu hawezi kuajiliwa na Mluo. Mluo naye hawezi kuajiliwa na Mkikuyu. Ni hivyo hivyo kwa makabila mengine. Maana yake, hakuna ajira kwa M-TZ, labda kama ni kuzoa uchafu.

Wakenya wanahofia TZ kiasi kwamba hawataki hata apewe ajira za ofisi za UN ambazo siyo za Serikali yao. Mama Tibaijuka anaelewa alivyokuwa anapigwa vita na Wakenya. Wako tayari nafasi ichukuliwe na mtu wa nje ya EAC kuliko Mtanzania.

Mtego huu uliwahi letwa hapa kwenye suala la ardhi eti waruhusiwe kumiliki ardhi TZ na Watanzania waruhusiwe kumiliki ardhi Kenya. Ilishindikana maana TZ tulijua hakuna uwezekanao wa m-TZ kumiliki ardhi Kenya.

Rais epuka mtego huo usio na faida kwa Tanzania.
EeeenHeee!
Hapo hakuna mtego wa kumnasa yeyote mwenye akili timamu!

Hawa wakenya sijui huwa wanamtindio wa akili hata haieleweki; maana hawachoki kila mara kusisitiza mambo yaliyokwishakataliwa toka zamani!

Unamwekea mtu mtego ulio wazi namna hii ina maana mtu huyo karukwa akili na kusahau kila kitu?
 
Haya unachozungumza ndio uhalisia wa huko Kenya?? Ni Kenya ipo hiyo?
Kenya mjaluo hataki hataa kumsikia mkikuyu achilia mbali mtanzania
Ukienda na kuondoka wa kwa sio shida, shida nenda kaishi rasmi.
Umesahau Jaguar na watu wake walivyotaka kuwatimua wamachinga wa kitanzania?
Imagine, wamachinga tu ambao hawapati chochote walikuwa wanawaonea wivu, Leo ije kuwa wewe kwenda kufanya kazi au kufungua kampuni kwao.
Sema huna hela wala connection ya kufanya hayo unayoongelea, acha kuongea vitu usivyovijua. Ati mjaluo hataki kumsikia mkikuyu,... hivi wewe ndo unajua sana kutiliko au waishi huku? Acha kupotosha jamii, ka huna la kusema tulia. Watu wanaishi na amani huku, chuki haileti chakula mezani, dadeq!
 
Cheza na watu wote lakini usicheze na Mkenya.
And to be fair,it's a section of Kenyans from certain communities who consider themselves better-off than the rest of them.
A large chunk of deprived communities are not any different in terms of general outlook of life from an average Tanzanian.
 
Ununue ardhi wapi na ya nini? Ardhi ya kujenga nyumba utapata, sasa hiyo ndo inipeleke Kenya? Nataka ardhi ya kuzalisha maua na kahawa, ipo? Nani akuuzie. Acha udanganyifu.
Wewe huna hela, ungekuwa nazo, hata Ulaya unanunua ardhi ya kuzalisha utakacho. Narudia, tafuta hela, na sio kidogo! 🤣
 
Sema huna hela wala connection ya kufanya hayo unayoongelea, acha kuongea vitu usivyovijua. Ati mjaluo hataki kumsikia mkikuyu,... hivi wewe ndo unajua sana kutiliko au waishi huku? Acha kupotosha jamii, ka huna la kusema tulia. Watu wanaishi na amani huku, chuki haileti chakula mezani, dadeq!
Mkuu, sasa wewe hapa unakataa nini, jambo lililo wazi kabisa kwa mtu mwenye akili huru kuliona!
 
Kuna maamuzi ambayo kihistoria unajua tu huo ni mtego mbaya sana! Hatuhitaji ruhusa kama hiyo ambayo ni nadharia tu! Kenya Mkikuyu hawezi kuajiliwa na Mluo. Mluo naye hawezi kuajiliwa na Mkikuyu. Ni hivyo hivyo kwa makabila mengine. Maana yake, hakuna ajira kwa M-TZ, labda kama ni kuzoa uchafu.

Wakenya wanahofia TZ kiasi kwamba hawataki hata apewe ajira za ofisi za UN ambazo siyo za Serikali yao. Mama Tibaijuka anaelewa alivyokuwa anapigwa vita na Wakenya. Wako tayari nafasi ichukuliwe na mtu wa nje ya EAC kuliko Mtanzania.

Mtego huu uliwahi letwa hapa kwenye suala la ardhi eti waruhusiwe kumiliki ardhi TZ na Watanzania waruhusiwe kumiliki ardhi Kenya. Ilishindikana maana TZ tulijua hakuna uwezekanao wa m-TZ kumiliki ardhi Kenya.

Rais epuka mtego huo usio na faida kwa Tanzania.
Watanzania wengi hawaendelei kwa sababu ya negativity. Wao kila wakati, kila mahali wanafikiria kudhulumiwa tu. Matokeo yake hawawezi kufanya chochote maana kila wanapogusa, wanaona wataibiwa au wataonewa.

Mtanzania kuruhusiwa kufanya kazi Kenya bila kuhitajika kuwa na work permit ni opportumity nzuri, na wenye akili wataitumia vizuri ili kutengeneza maisha yao.

Maana yake ni kuwa leo hii nikienda kuanzisha kampuni yangu Kenya au biashara, naweza nikawaajiri wafanyakazi toka Tanzania bila ya usumbufu wowote.

Walio negative waendelee kuwa negative, wanaoona kila kitu ni opportunity, tusonge mbele. Dunia haisimami. Kuna faida kubwa kwenye tamko la Uhuru kuliko hasara.

Watanzania tubadilike, tuwe watu positive. Negativity hudumaza akili na maendeleo. Negativity hujenga chuki dhidi ya aliyefanikiwa au kukutangulia.

Ukitaka kuendelea haraka, shirikiana na aliye tajiri zaidi yako, siyo na aliye maskini zaidi yako.

Hongera sana Uhuru, hongera Kenya. Hongera zaidi Rais Samia maana bila wewe, hii fursa isingepatikana.
 
Mambo mengi ya ajabu yatatokea baada ya kifo cha mtu mwenye akili nyingi jpm.
Kuna haja ya kutilia mashaka uwezo wa akili yako. Kumtambua mwenye akili na asiye na akili, kunahitaji kiwango fulani cha akili.

Kwa kipimo chochote kilichosahihi, Tanzania haikuwahi kuwa na kiongozi mbaya wa kiwango cha marehemu. Kwa namna alivyokuwa akitenda, hakustahili kuwa Rais. Mungu amsamehe kwa maovu mengi aliyoyatenda dhidi ya Taifa na dhidi ya watanzania wenzake.
 
Kuna maamuzi ambayo kihistoria unajua tu huo ni mtego mbaya sana! Hatuhitaji ruhusa kama hiyo ambayo ni nadharia tu! Kenya Mkikuyu hawezi kuajiliwa na Mluo. Mluo naye hawezi kuajiliwa na Mkikuyu. Ni hivyo hivyo kwa makabila mengine. Maana yake, hakuna ajira kwa M-TZ, labda kama ni kuzoa uchafu.

Wakenya wanahofia TZ kiasi kwamba hawataki hata apewe ajira za ofisi za UN ambazo siyo za Serikali yao. Mama Tibaijuka anaelewa alivyokuwa anapigwa vita na Wakenya. Wako tayari nafasi ichukuliwe na mtu wa nje ya EAC kuliko Mtanzania.

Mtego huu uliwahi letwa hapa kwenye suala la ardhi eti waruhusiwe kumiliki ardhi TZ na Watanzania waruhusiwe kumiliki ardhi Kenya. Ilishindikana maana TZ tulijua hakuna uwezekanao wa m-TZ kumiliki ardhi Kenya.

Rais epuka mtego huo usio na faida kwa Tanzania.
Kwa uzoefu wake katika siasa na diplomasia ya hizi nchi, nahisi haya usemayo Mama anayajua vizuri sana tu. Katika biashara na mambo mengine, kukaa na adui yako au mnafiki ni kitu cha kawaida. Nadhani Mama anajua ni maslahi yapi anayoyapa kipaumbele kwa waTz na yapi hayapi kipaumbele (mf. nadhani sisi tunachotaka ni biashara zaidi na kuuza bidhaa zetu kwao, kuongeza utalii n.k, lakini sidhani kama tunahitaji ajira zao, wao wanataka kuingia na kuuza bidhaa na pia kumiliki ardh, hapa hawataruhusiwa) na huenda tukayaona haya mbeleni. Sisi wananchi wa Tz nasi tuwe makini na tuwe tayari kwa ushindani.
 
Back
Top Bottom