Rais Samia: Waziri hutakiwi kujitoa kwenye maamuzi ya Serikali

Rais Samia: Waziri hutakiwi kujitoa kwenye maamuzi ya Serikali

Rais Samia akiwaapisha mawaziri leo, Oktoba 3 amesema waziri hatakiwi kusema hakubaliani na maamuzi ya serikali. Au kusema kuwa nimeelekezwa hivi ila sikubaliani. Hatakiwi kujitoa bali kuwa sehemu ya maamuzi.

Sijui ni waziri gani aliyesema haya ni maamuzi ya serikali sio yangu?
Ndio maana Mwigulu hataondolewa anasimamia walichokubaliana
 
Naona exposure inawaponza wasaidizi wa Rais, Rais anataka kila mteule wake afanye vile anavyotaka yeye hata kama hana ujuzi wa jambo husika, hii sio sawa, anakosea.

Mulamula alikuwa na exposure na mambo ya nje toka enzi za JK, na hiyo exposure yake naamini ndio iliyochangia Rais kumpa kile cheo, leo iweje amuondoe yule aliyegoma kuburuzwa kwenye jambo alilo na experience nalo? lililofanya akaaminiwa na kupewa kazi? Rais hajui anachofanya.

Kuwa na wasaidizi maana yake ni kumsaidia Rais, na sio tu kufanya kazi wanazopangiwa, bali hata kwa ushauri pia, hii kauli aliyoitoa Rais itazidi kuzalisha chawa wengi zaidi, wajinga, majeuri, na viburi.

Matokeo yake kina Mwigulu wanazidi kutuburuza na tozo, huku Makamba na Nape na kauli zao za hovyo kila wakati; yeye anataka jambo lolote wakishakaa na kukubaliana serikalini lisipingwe, vyema atambue hata wajinga huwa wana maamuzi yao na yasipoangaliwa mapema yatatuumiza.

Awaache wenye uzoefu wamsaidie, unaweza kuwa na kundi kubwa la wajinga wasiojua chochote kasoro mmoja wao, na kiongozi mzuri anatakiwa kumtambua huyo mmoja.
 
Huyu mama akilazimisha kubakia madarakani hiyo 2025, basi mchele utauzwa elfu 6 kwa kilo! Na mafuta ya petrol na dizeli lita itakuwa elfu 6 pia! Vifaa vya ujenzi ndiyo kabisaa!! Vitaendelea kupanda mara dufu.

Nitafurahi kama atakaa pembeni.
 
Rais Samia akiwaapisha mawaziri leo, Oktoba 3 amesema waziri hatakiwi kusema hakubaliani na maamuzi ya Serikali au kusema kuwa nimeelekezwa hivi ila sikubaliani. Hatakiwi kujitoa bali kuwa sehemu ya maamuzi.

Sijui ni waziri gani aliyesema haya ni maamuzi ya Serikali sio yangu?

Aliye kinyume chetu hayupo upande wetu
Tumemuelewa rais
 
Waziri halazimiki kutii kila kitu endapo anaona kuna vitu haviko sawa, alipokosea ni kuendelea kubakia madarakani, alipaswa kujiuzulu baada kuona hakuna muafaka. Kusubiri kuondolewa ni kama kuonesha kiburi.
Unajuaje aliomba kujiuzulu mwenyewe?
 
Naona exposure inawaponza wasaidizi wa Rais, Rais anataka kila mteule wake afanye vile anavyotaka yeye hata kama hana ujuzi wa jambo husika.

Kuwa na wasaidizi maana yake ni kumsaidia Rais, sio tu kufanya kazi wanazopangiwa, bali hata kwa ushauri pia, hii kauli aliyoitoa Rais itazidi kuzalisha chawa wengi zaidi.
Unataka raisi maamuzi yake yasiheshimiwe?
 
Huyu mama akilazimisha kubakia madarakani hiyo 2025, basi mchele utauzwa elfu 6 kwa kilo! Na mafuta ya petrol na dizeli lita itakuwa elfu 6 pia! Vifaa vya ujenzi ndiyo kabisaa!! Vitaendelea kupanda mara dufu.

Nitafurahi kama atakaa pembeni.
Hatogombea, usiumize KICHWA.
 
Back
Top Bottom