Rais Samia: Waziri Mchengerwa amefanya kazi nzuri sana, sasa nimempeleka TAMISEMI mwakani kuna Kivumbi

Rais Samia: Waziri Mchengerwa amefanya kazi nzuri sana, sasa nimempeleka TAMISEMI mwakani kuna Kivumbi

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Rais Samia amemsifu Waziri Mchengerwa kwamba kafanya kazi nzuri sana kwenye Wizara alizopita ndio maana amemhamishia Tamisemi Ili akasimamie kivumbi Cha mwakani yaani uchaguzi wa Serikali za mitaa kwani anajua anaweza.

-
"Kwa mfano Mchengerwa nilipompeleka utumishi mwanzo kaingia na kasi kelele zikawa nyingi, nikasema labda waziri wangu kazidi kapandisha mabega nimpeleke michezo, kaenda michezo kazi aliyoifanya mmeiona, kaacha kazi nzuri sana, katoka michezo nimempeleka utalii, mipango aliyoiweka sekta ile unayeenda ukienda ukafuata yaliyowekwa utalii unakwenda kupanda"- Rais Dkt.


My Take
Wacha tusubirie yetu macho,binafsi najua sifa ya Mchengerwa ni kujali watu wa chini zaidi.

“Mchengerwa sasa nimempeleka TAMISEMI mwakani kuna Kivumbi na mimi nakujua najua unaweza, Kivumbi kile kinafanana na kifua chako najua unaweza, kwahiyo nimekupeleka TAMISEMI ni kazi kazi,” Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza leo, Septemba 1, 2023 Ikulu ndogo Zanzibar baada ya shughuli ya uapisho wa viongozi mbalimbali wa Serikali.
 
Rais Samia amemsifu Waziri Mchengerwa kwamba kafanya kazi nzuri sana kwenye Wizara alizopita ndio maana amemhamishia Tamisemi Ili akasimamie kivumbi Cha mwakani yaani uchaguzi wa Serikali za mitaa kwani anajua anaweza.

View: https://twitter.com/eastafricatv/status/1697525199304839595?t=LwsEyExScs3-Ft_sJLsOtg&s=19


My Take
Wacha tusubirie yetu macho,binafsi najua sifa ya Mchengerwa ni kujali watu wa chini zaidi.

Nimeona walimu wengi wakilia na uhamisho,akifanikiwa kwenye hiyo kero ya walimu basi hana baya.....
 
Halafu sometimes tujitahidi kutumia Akili kidogo hata kama hatukubarikiwa kuwa nazo.
Hivi anayefanya vizuri mahala fulani unatakiwa kumuacha hapo hapo ili apaimarishe au ahamishwe Kwingineko na baada ya muda unamtoa tena?

Tafadhali hebu acheni Kutulazimisha akina GENTAMYCINE tuwadharau hata kama tunajua mna Udhaifu wa Kifikra achilia mbali wa Kiutendaji.

Mtu anaharibu Wewe unamsifia tu!!!
 
raia walikua wanaeshimu mamlaka na kuziamini,ila kwasasa wanaona n mzaa mzaa tu
sasa suala la bandari ambalo limewagusa wengi mkuu wetu anatoa majibu eti kaamua kukaa kmya si aseme mchakato ulikuaje ili watu waelewe

sasa nimeamini anapokea maelekezo ili kutekeleza majukumu yake
 
raia walikua wanaeshimu mamlaka na kuziamini,ila kwasasa wanaona n mzaa mzaa tu
sasa suala la bandari ambalo limewagusa wengi mkuu wetu anatoa majibu eti kaamua kukaa kmya si aseme mchakato ulikuaje ili watu waelewe

sasa nimeamini anapokea maelekezo ili kutekeleza majukumu yake
Wakenya kupitia KOT ( Kenyans On Twitter ) Siku hizi Mtandao wa X wanatusaidia Kumdharau kwa Niaba yetu na wanamchambua vilivyo huko sijui kama Wasaidizi wake huwa wanamuonyesha.
 
Back
Top Bottom