Rais Tshisekedi siku zake zinahesabika

Rais Tshisekedi siku zake zinahesabika

Wakuu inakuaje? sasa twende kazi.

Siku mbili tatu hizi kumekuwa na hali ya sintofahamu kati ya serikali ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na ile ya Rwanda, kila mmoja akimtupia lawama mwenzake na kutishia kuvunjilia mbali uhusiano wao wa kidiplomasia nk.

Kwa upande wa Congo ndio wanaonekana kuwa wamechukia zaidi hadi kupelekea serikali yao kumfukuza nchini kwao balozi wa Rwanda, na pia kumwata balozi wao aliekuwa nchini Rwanda.

Kwa upande wa Rwanda yenyew haioneshi kupanic wala kuchukizwa kivile, inaonekana ime relax ikisubiria kuona kingine kitachojiri kutoka katika serikali ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Sasa basi... Rwanda ina uwezo wa kuichakaza na kuisambaratisha Congo kijeshi kwa njia zote, iwe kwa angani, majini au ardhini tena kwa muda mfupi sana.

Congo inaweza kuishinda Rwanda kwa maneno tu, maana wakongomani ni waimba miziki na wachezaji wakubwa, ila linapokuja swala la mapambano ya kijeshi na weupe sana wanashindwa hata na Burundi.

Kwanza toka Congo ilipopata uhuru jeshi lake halikuwahi kushinda vita yoyote ile. Wakati wa Mobutu jeshi la Congo lilichakazwa vibaya na waasi waliokuwa wanaongozwa na hayati Desire Kabila (father) na baadae jeshi hilo limeendelea kuchakazwa na makundi mbali mbali ya waasi wengi wao ni kutoka nchi jirani.

Sasa jiulize ikiwa nchi yenye raia zaidi ya milioni 1 inachakazwa na waasi wasiozidi elfu 5, huku waasi hao wakiwa na silaha za kuunga unga na mazoezi ya msituni yasiokuwa rasmi. Je watakapoingia kwenye vita na nchi yenyewe si ndo yatakuja kutokea yale ya Mobutu na Idi Amini!!

Hivi kweli Tshisekedi anaamini kuwa nchi yake inaweza kuipiga Rwanda au ndo kifo kinamwita, au wazee wa kazi (Kabila's team) wanamshauri ujinga ili akipigwa akikimbia Kabila arudi kuongoza Congo?

Maana katika hali ya kawaida haiwezekani nchi inayoshindwa vita na waasi elfu 3, ijidanganye kuwa inaweza kupambana na nchi yenye wanajeshi zaidi ya laki, wenye ueledi mkubwa wa kivita, silaha za kisasa na wanajeshi wa kutosha.

Katika EAC nzima, nchi ambazo Rwanda inaweza kuhofia kwa namna fulani kupambana nazo ni Tanzania na Kenya tu ambazo majeshi yao yameshafanya mambo makubwa ndani na nje ya mipaka yao Tanzania ikiwa inaongoza kwa kufanikiwa oparation mbali mbali katika nchi za Msumbiji, Zimbabwe, Angola, Namibia, Comoros nk. Ila hizo zingine Rwanda inaziona kama vile ni nchi zinazolindwa na makundi ya sungu sungu tu na sio wanajeshi kamili.

So chonde chonde Tshisekedi watu bado wanakuhitaji uendelee kuwa raisi wao. Usije kuingia kwenye mtego ambao utashindwa kujinasua. Kagame alimhofia Kikwete tu mjeshi mwenzake na anajua watu wa kicheka cheka kama JK maamuzi yao yanakuwaga na athari kubwa kwa wengine. Lakini nyinyi wengine anawaona vikaragosi wake.

Tena kwa Congo ndo kabisa hawezi kutuma jeshi lake kupoteza muda wao. Sana sana ataajiri vijana kutoka katika makampuni mbali mbali ya ulinzi waje kumaliza kazi.

Pichani juu ni jeshi la Rwanda na picha ya chini ni jeshi la Congo.

Siku njema kwa wasomaji na wachangiaji wote. Asanteni.
Vijana wa tolu lazima mfumuliwe safari hiii
 
Namshauri DRC aimarishe Kwanza ujasusi WA ndani na nje , akifanikisha hili mbona Rwanda anachapwa asubuh
Pia DRC akiimarisha ujasusi wa nje atasaudiwa na WA Hutu kumtoa kagame madarakani
Ndoto hii naona ilishindikana zaidi ya miaka 20 iliyopita. Sidhani kama itawezekana leo.
 
Nusu ya Jeshi la Congo DRC ni Wanajeshi hewa, na mishahara wale hewa ndio wanaingiziwa haraka kuliko Wanajeshi kamili inachelewa sana au hawapati kabisa.

Ammo wakipewa wanawauzia Mai mai FLDR na Vikundi vingine vya Waasi huko Ituri, sasa tuulizane kuna Jeshi hapo?

Hata ukiwajengea Jeshi Serious wanarudia kule kule Majenerali wako Kinshasha wanakata viuno kwa Fally Ipupa.
 
Ni ngumu sana, congo ina walinzi royal sana mfano bodyguards wa Rais Mobutu ukitazama mahojiano yao utaelewa,wale jamaa walipewa kiapo cha kufa kwa ajili ya Rais na walikuwa hawaogopi kifo

Kabila mkubwa alijichanganya akaweka vilinzi vitoto visivyo na mafunzo yoyote ndicho kilimuangusha
Kabila mkubwa kilichomuangusha ni kukubali Kagame kumchagaulia Walizni
 
Nusu ya Jeshi la Congo DRC ni Wanajeshi hewa, na mishahara wale hewa ndio wanaingiziwa haraka kuliko Wanajeshi kamili inachelewa sana.

Ammo wakipewa wanawauzia Mai mai FLDR na Vikundi vingine vya Waasi huko Ituri, sasa tuulizane kuna Jeshi hapo?

Hata ukiwajengea Jeshi Serious wanarudia kule kule Majenerali wako Kinshasha wanakata viuno kwa Fally Ipupa.
Ni sahihi,Wakati wa Mobutu alijua ana wanajeshi elfu 60, lakini mshauri wake wa usalama anadai idadi kubwa ilikuwa hewa,alitaka kuhesabu askari wote ila majenerali ambao ndio walipiga hiyo mishahara wakawambia wanajeshi wanataka kufukuzwa,then majenerali wakamuonya Rais kuna uhasi unakaribia hivo zoezi lile likafa
 
Maswala ya vita yaache tu yaani unaweza dharau Ila ukatembezewa kichapo Cha karne na underdog wa dunia kwenye vita na usiamini.

Hakuna vita nyepesi. Kama wamejiandaa kulea yatima na wajane wa kutosha basi wapigane.

Ni rahisi sana kuingia vitani sekunde tu ila vita haviishi ndani ya sekunde itachukua muda mrefu mambo kurudi kawaida
Bora wewe umeongea ukweli. Ukubwa wa nchi sio ndio uwezo wa kijeshi.
Nchi inaweza kuwa kubwa na ikachakazwa na kanchi kadogo kama wilaya yake, na watu wakashangaa.
 
We ni mmoja ya wale vijana wa slim mlio pandikizwa umu JF
Mimi sio na kamwe siwezi kuwa mmoja wao. Hapa naongelea uhalisia wa kile kitachotokea endapo Congo itathubutu kuingia vitani na Rwanda.
 
Hakuna kikindi cha waasi hapa Duniani kina weza shindana na Serikali yoyote na kikaweza!. Kinachofanyika ni Serikali za Nchi na Nchi zinapigana proxy wars kwa mgongo wa vikindi vya waasi.

Na jinsi siasa & chumi za Dunia zinavyoondesha kwa hadaha basi Wananchi wengi katika mataifa mengi,huamini uongo unaosema na kutangazw na vyombo vya habari kama ndio ukweli.

Ukweli ni kuwa Kagame na Rwanda yake wanatumiwa na western kuivuruga Kongo.
 
Mkuu endelea kumuingiza maboya Tshisekedi, mwisho wa siku yatakayomkuta ni yeye sio wewe mzungumzaji.
Hivi huwa mnaandika nyuzi kuelemisha na kuelemishwa au??,hivi inakuwaje MTU anaelimishwa kwa jambo ambalo watu wengi sana uelewa nalo kuliko wewe afu wewe unaendelea na maeneno ya shombo.unaonekana hauko serious!!
 
Wakuu inakuaje? sasa twende kazi.

Siku mbili tatu hizi kumekuwa na hali ya sintofahamu kati ya serikali ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na ile ya Rwanda, kila mmoja akimtupia lawama mwenzake na kutishia kuvunjilia mbali uhusiano wao wa kidiplomasia nk.

Kwa upande wa Congo ndio wanaonekana kuwa wamechukia zaidi hadi kupelekea serikali yao kumfukuza nchini kwao balozi wa Rwanda, na pia kumwata balozi wao aliekuwa nchini Rwanda.

Kwa upande wa Rwanda yenyew haioneshi kupanic wala kuchukizwa kivile, inaonekana ime relax ikisubiria kuona kingine kitachojiri kutoka katika serikali ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Sasa basi... Rwanda ina uwezo wa kuichakaza na kuisambaratisha Congo kijeshi kwa njia zote, iwe kwa angani, majini au ardhini tena kwa muda mfupi sana.

Congo inaweza kuishinda Rwanda kwa maneno tu, maana wakongomani ni waimba miziki na wachezaji wakubwa, ila linapokuja swala la mapambano ya kijeshi na weupe sana wanashindwa hata na Burundi.

Kwanza toka Congo ilipopata uhuru jeshi lake halikuwahi kushinda vita yoyote ile. Wakati wa Mobutu jeshi la Congo lilichakazwa vibaya na waasi waliokuwa wanaongozwa na hayati Desire Kabila (father) na baadae jeshi hilo limeendelea kuchakazwa na makundi mbali mbali ya waasi wengi wao ni kutoka nchi jirani.

Sasa jiulize ikiwa nchi yenye raia zaidi ya milioni 1 inachakazwa na waasi wasiozidi elfu 5, huku waasi hao wakiwa na silaha za kuunga unga na mazoezi ya msituni yasiokuwa rasmi. Je watakapoingia kwenye vita na nchi yenyewe si ndo yatakuja kutokea yale ya Mobutu na Idi Amini!!

Hivi kweli Tshisekedi anaamini kuwa nchi yake inaweza kuipiga Rwanda au ndo kifo kinamwita, au wazee wa kazi (Kabila's team) wanamshauri ujinga ili akipigwa akikimbia Kabila arudi kuongoza Congo?

Maana katika hali ya kawaida haiwezekani nchi inayoshindwa vita na waasi elfu 3, ijidanganye kuwa inaweza kupambana na nchi yenye wanajeshi zaidi ya laki, wenye ueledi mkubwa wa kivita, silaha za kisasa na wanajeshi wa kutosha.

Katika EAC nzima, nchi ambazo Rwanda inaweza kuhofia kwa namna fulani kupambana nazo ni Tanzania na Kenya tu ambazo majeshi yao yameshafanya mambo makubwa ndani na nje ya mipaka yao Tanzania ikiwa inaongoza kwa kufanikiwa oparation mbali mbali katika nchi za Msumbiji, Zimbabwe, Angola, Namibia, Comoros nk. Ila hizo zingine Rwanda inaziona kama vile ni nchi zinazolindwa na makundi ya sungu sungu tu na sio wanajeshi kamili.

So chonde chonde Tshisekedi watu bado wanakuhitaji uendelee kuwa raisi wao. Usije kuingia kwenye mtego ambao utashindwa kujinasua. Kagame alimhofia Kikwete tu mjeshi mwenzake na anajua watu wa kicheka cheka kama JK maamuzi yao yanakuwaga na athari kubwa kwa wengine. Lakini nyinyi wengine anawaona vikaragosi wake.

Tena kwa Congo ndo kabisa hawezi kutuma jeshi lake kupoteza muda wao. Sana sana ataajiri vijana kutoka katika makampuni mbali mbali ya ulinzi waje kumaliza kazi.

Pichani juu ni jeshi la Rwanda na picha ya chini ni jeshi la Congo.

Siku njema kwa wasomaji na wachangiaji wote. Asanteni.
Kagame mnamtukuza mno.
 
Kwa namna yoyote ile Rwanda hawezi ipiga Congo, ila Congo ni raisi sana kuipiga Rwanda. Njia pekee Rwanda anaweza shinda vita na Congo ni kwa kumu eliminate Tshekedi, otherwise Rwanda mwenyewe hayupo tayari Kigali ifumuliwe aanze ijenga na upya.
Kama wameshindwa kukifumua kikundi kidogo cha M23, basi wasahau kufanikiwa kuvuka hata mpaka wa Rwanda.
 
Wee Mnyarwanda. Haidhuru. Lakini fanya utafiti kabla ya kujiandikia tu, pia jaribu kusoma kwa uhakika trends za dunia. Miaka, mawiki na hata siku hazifanani.
Safari hii kama Rwanda haita climb down, huenda mambo yakawawia vibaya. Afrika ndiyo hivyo: Ngoma ikisifiwa sana hupasuka!
Mimi sina uhusiano wowote na wanyarwanda ila ninachofanya hapa ni kuandika uhalisia wa kile ambacho kitatokea endapo Tshisekedi ataingia mkenge kwa Paka.
 
Back
Top Bottom