Rais Uhuru Kenyatta: Nchi jirani zinahitaji siasa ambazo ushindani si uadui na vita

Rais Uhuru Kenyatta: Nchi jirani zinahitaji siasa ambazo ushindani si uadui na vita

Tatizo kuingia mtaani kwa sasa tumeshashindwa bado tunavumilia.Hivyo for the time being wabunge waende tu bungeni. Hii ya kuingia mtaani itakuja yenyewe pale Magufuli atakuwa katika mwaka wake wa 14 akitawala. Hata wana CCM wenyewe wengi watakuwa wamemchoka. Hapo ndo saa ya ukombozi wa kweli itatimia.
Mwana CCM yupi wa kumchoka Magu!?
A. H. Mwinyi ambaye mwanawe kapewa uraisi Zanzibar!?
J.M. Kikwete ambaye amenyamazishwa kwa bangaloo na kupewa ubunge kwa mwanae na mkewe!?
Hao ndio wanaitwa wana CCM,sio hawa wana CCM - tumbo - maslahi ambao hata katiba ya TANU - CCM hawaijui, miiko ya uongozi hawaijui, Azimio la Arusha hawalijui, misingi ya itikadi ya Ujamaa hawaijui.
Mwana CCM mwenye uwezo wa kumpinga Magu ni marehemu kwa sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kenyatta kasahau zile fitna alizofanya kwenye uchaguzi mpaka yule jamaa kuuwawa na kisha kukatwa mkono.
Sijui alikua mwenyekiti wa tume ya uchaguzi kama sikosei
 
Kumbe ndio maana hakuja kwenye lile igizo la kumuapisha akawaachia wasanii wengine kina Museveni.

Jamaa ana uelewa wa juu sana hasa linapokuja suala la mahusiano kati ya wanasiasa, amepevuka sana kidiplomasia, kagonga pale pale hajataka unafiki.

Kwa kauli zake anaonesha jinsi alivyo mwepesi kujirudi na kufanya mazungumzo na mahasimu wake kisiasa, sio hapa kwetu, ni uadui tu miaka yote.

Haya yanayotokea hapa kwetu atakuwa anayaona mambo ya kishamba sana, kutofutiana itikadi ndio unamuona mwenzio adui, mpaka anakimbia nchi aliyozaliwa upo kimya husemi chochote?!
Yaliyomkuta Miguna Miguna huko Kenya kufukuzwa nchi kimabavu na amri zake 13 za mahakama kisa tofauti za kisiasa na kumwapidha Odinga huoni!
 
Uko sahihi, je sisi tunaweza kuwacheka? Au itakuwa ni mwenye chongo kucheka kengeza? Kabla Magu hajaingia madarakani tulikuwa afadhali kwa nchi zote za Afrika mashariki, je kwa sasa tunaweza kujivunia nini dhidi ya nchi nyingine zinazotuzunguka?
Huwezi kusema tulikuwa afadhali wakati nchi hii ina mifumo mibovu ya kiutawala toka taifa letu lianzishwe. Afrika mashariki yote imefeli kwenye good governance tusichekane wala kunyosheana vidole. Muda ukifika tutabadilika.
 
Huwezi kusema tulikuwa afadhali wakati nchi hii ina mifumo mibovu ya kiutawala toka taifa letu lianzishwe. Afrika mashariki yote imefeli kwenye good governance tusichekane wala kunyosheana vidole. Muda ukifika tutabadilika.
Mmmhh, huo muda ni lini?
 
Siasa zinatofautiana,Huyo huyo Kenyatta Ikulu yake imemeguka vipande viwili.......wao pia siasa zao zimejaa ukabila,undugu,urafiki etc......kila nchi inawikinesi zake
 
Katika kile unachoweza kutafsiri kama ni Kenya kuguswa na siasa mpya za Tanzania, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesistiza ustahimilivu wa kisiasa hasa kwa nchi zilizoizunguka. Amesema uchaguzi unafaa kuleta utangamano wa nchi na siyo kinyume chake.

Amedai kuwa siyo siri nchi zinazoizunguka Kenya hazina utulivu mzuri wa kisiasa kama ilivyozoeleka. Amedai kuwa kukosekana kwa utulivu kwa jirani ni hatari kwa Kenya.

Huku akipigiwa makofi na wabunge Rais Kenyatta, amesisitiza kuwa wanasiasa wazee wasiwachokoze wanasiasa vijana badala yake wawalee kwa upendo.

=======

Katika hotuba yake Bungeni, Rais Kenyatta amesema:

Nchi nyingi jirani zetu leo zinahitaji kupeana mikono. Wanahitaji siasa ambazo ushindani haugeuki uadui na vita. Wanahitaji viongozi wa kisiasa waliolenga kujumuisha vijana na waliokata tamaa, bila kuwachochea kuasi dhidi ya nchi zao na wazee wao.

Tumejifunza kama Wakenya kwamba uchaguzi pekee hauwezi kuleta amani na umoja kwa watu waliogawanyika. Kwa hilo, viongozi lazima waafikiane na kuwa madaraja ya kuwavusha watu keuelekea kwenye usalama na ustawi.

------------

Many neighboring countries today need a handshake. They need politics in which competition is not turned into enmity and war. They need political leaders focused on including the young and desperate, not inciting them to revolt against their countries and their elders.

We have learned as Kenyans that elections alone cannot bring peace and unity to a divided people. For that, leaders must reach out to each other and build bridges over turbulent waters to allow the people to cross into safety and prosperity.


Demokrasia Kenya? Ulikwishafika Kenya wewe?
Hivi mtanzania kweli kweli uliyezoea maisha ya Amani, utulivu na ustaarabu wa Tz unaweza ishi Kenya ukazoea kabisa wewe? Wale wanaitwa "Nyang'au". Unajua maana ya Nyang'au Wewe? Acheni masihara. Afadhali maisha ya Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi, unaweza kuzoea. Wananchi wastaarabu. Wakarimu. Kenya!? Hovyo kabisa.

Hao akina Uhuru, Odinga, Ruto; unawajua wewe?
Tanzania nenda sehemu yoyote utapata ardhi ya kulima, kufugia, kujenga, biashara na maisha yanaendelea. Nenda Kenya ukaone! Maskini ni maskini kweli mpaka kiama; na tajiri hali Kadhalika. Ulikwishafika Kibera wewe. Wapi ktk miji ya Tanzania kuna slums kama zilizopo Kenya. Acheni bwana. Kenya kuna watu wa hovyo usipime, wengine wako huku Wakikuyu na Wajaruo, wanatusimulia pia. Wapo wengi tu, na kwa siasa nzuri za Tanzania wengi wana hali nzuri ya maisha. Ni matajiri wala hawabughudhiwi. Ukiwaambia warudi Kenya wanasema afadhali uwaue kuliko kurudi kule "motoni". Acheni bwana.

Nenda Kenya uone kama utapata ardhi ya kulima au kufugia. Ardhi yote imehodhiwa na akina Uhuru. Ni "miungu watu" wa Kenya ... The untouchables. Ati loyal families!
Maendeleo ya TZ yanakwenda sawia ktk maeneo yote mijini hadi vijijini. Nenda Kenya Kaskazini ukaone. Aibu!

Acheni kutulinganisha TZ na Nchi ya unyonge kama Kenya bwana. Ni jamaa wana publicity hao usipime! Nawafananisha na waingereza wanaoshinda kombe la dunia magazetini!

Ni suala la muda tu; Kwa mwendo tunaokwenda TZ, Kenya watakuja kutupigia magoti miaka si mingi. Hata hivyo, mbona tunawalisha mahindi na maharage mara nyingi tu. Hawana uwezo wa kujitosheleza kwa chakula.

Tanzania ni Nchi pekee Duniani iliyo na Serikali zinazojitegemea kuanzia ngazi ya kitongoji/mtaa.
Ardhi ni mali ya Serikali. Hakuna ubaguzi wa aina yoyote, hata Wakenya waliopo TZ wanapewa nafasi za uongozi almradi wanafaa, nk. Je, Kenya mambo haya yapo? Tunapendana hatubaguani. TZ imekwishakuwa fashion ya zamani kuoa au kuolewa na kabila lako! Kenya ipo hiyo?

Kenya wakitaka kupiga hatua sasa ya maendeleo wakubali kuja kujifunza Tanzania kwani kwa sasa hatuna la kujifunza kutoka Kenya.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU MBARIKI JPM
MUNGU IBARIKI AFRIKA
 
'Huku akipigiwa makofi na wabunge Rais Kenyatta amesema watapokea watu watakaokimbilia Kenya ili waweze kuishi kwa amani.'

'Amesisitiza kuwa wanasiasa wazee wasiwachokoze wanasiasa vijana badala yake wawalee kwa upendo.'

Soon utasikia mkuu wa PORTLAND akisema ndege za KQ ni marufuku hapa na Mahindi hakuna kuwauzia.

'Yaani Mtu unampa ndege tausi lkn bado haridhiki tu,nasema uongo ndg zangu?

[emoji1787]nimecheka sana hako ka quote, maneno uliyotunga yana maana kubwa mno, Dangote juzi kati amesema ana namba ya jiwe ya simu lakini bado Dangote huyo huyo analalamika hali ngumu ya uwekezaji, nilijiongeza tu kwamba yawezekana Dangote huwa anampigia simu jiwe na analalamika lakini jiwe anajidai kuwa mwema na aliyefanya kila awezalo anajibu “hali ya uwekezaji ni nzuri , tuna mazingira mazuri sana ndio maana nimekupa na namba yangu ya simu,alafu huku kwetu kuna vibinti vizuri vyeupe..” mazungumzo yanaisha
 
Kumbe ndio maana hakuja kwenye lile igizo la kumuapisha akawaachia wasanii wengine kina Museveni.

Jamaa ana uelewa wa juu sana hasa linapokuja suala la mahusiano kati ya wanasiasa, amepevuka sana kidiplomasia, kagonga pale pale hajataka unafiki.

Kwa kauli zake anaonesha jinsi alivyo mwepesi kujirudi na kufanya mazungumzo na mahasimu wake kisiasa, sio hapa kwetu, ni uadui tu miaka yote.

Haya yanayotokea hapa kwetu atakuwa anayaona mambo ya kishamba sana, kutofutiana itikadi ndio unamuona mwenzio adui, mpaka anakimbia nchi aliyozaliwa upo kimya husemi chochote?!
Nenda huko, ameshawafungulia mipaka shida nini kutoa uharo hapa jamvini.
 
Katika kile unachoweza kutafsiri kama ni Kenya kuguswa na siasa mpya za Tanzania, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesistiza ustahimilivu wa kisiasa hasa kwa nchi zilizoizunguka. Amesema uchaguzi unafaa kuleta utangamano wa nchi na siyo kinyume chake.

Amedai kuwa siyo siri nchi zinazoizunguka Kenya hazina utulivu mzuri wa kisiasa kama ilivyozoeleka. Amedai kuwa kukosekana kwa utulivu kwa jirani ni hatari kwa Kenya.

Huku akipigiwa makofi na wabunge Rais Kenyatta, amesisitiza kuwa wanasiasa wazee wasiwachokoze wanasiasa vijana badala yake wawalee kwa upendo.

=======

Katika hotuba yake Bungeni, Rais Kenyatta amesema:

Nchi nyingi jirani zetu leo zinahitaji kupeana mikono. Wanahitaji siasa ambazo ushindani haugeuki uadui na vita. Wanahitaji viongozi wa kisiasa waliolenga kujumuisha vijana na waliokata tamaa, bila kuwachochea kuasi dhidi ya nchi zao na wazee wao.

Tumejifunza kama Wakenya kwamba uchaguzi pekee hauwezi kuleta amani na umoja kwa watu waliogawanyika. Kwa hilo, viongozi lazima waafikiane na kuwa madaraja ya kuwavusha watu keuelekea kwenye usalama na ustawi.

------------

Many neighboring countries today need a handshake. They need politics in which competition is not turned into enmity and war. They need political leaders focused on including the young and desperate, not inciting them to revolt against their countries and their elders.

We have learned as Kenyans that elections alone cannot bring peace and unity to a divided people. For that, leaders must reach out to each other and build bridges over turbulent waters to allow the people to cross into safety and prosperity.


Hii uliileta kwa sababu ipi nzuri? kuna hii tabia ya kuamini kwamba tunastahili kusikiliza majirani wanasemaje juu yetu, hata kama ubora wa majirani hao ni uchafu tui! TZ leo hii ina chochote cha kujifunza kutoka Kenya? Kweli unaamini Kenya kuna siasa za kujifunza? Una tatizo kichwani!
 
Siasa zetu zemekua za kishamba sana, kura zilizoandaliwa kwaajili ya watu fulani zinapenyezwa kwenye sanduku la kura na tukihoji tunapewa kibano na vyombo vya dola.
Zile za sauti ya zege aliprint hana jipya[emoji23][emoji23][emoji23] askofu ulikuwa wakati wake
 
Jamaa alikuwa anapenda ugomvi na ujeuri mpaka kwa majirani. Imagine mpaka mtu wa nje ya nchi anaona kijamaa ligomvi tu sembuse tulioishi nae mzee wa kuzurura na mabulungutu ya pesa?

Sijawahi kuona Rais anazurura na mahela kwenye begi, ule ushamba aisee ni zaidi ya kuwa papaa wa kwenye bendi za kikongo.
 
Demokrasia Kenya? Ulikwishafika Kenya wewe?
Hivi mtanzania kweli kweli uliyezoea maisha ya Amani, utulivu na ustaarabu wa Tz unaweza ishi Kenya ukazoea kabisa wewe? Wale wanaitwa "Nyang'au". Unajua maana ya Nyang'au Wewe? Acheni masihara. Afadhali maisha ya Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi, unaweza kuzoea. Wananchi wastaarabu. Wakarimu. Kenya!? Hovyo kabisa.

Hao akina Uhuru, Odinga, Ruto; unawajua wewe?
Tanzania nenda sehemu yoyote utapata ardhi ya kulima, kufugia, kujenga, biashara na maisha yanaendelea. Nenda Kenya ukaone! Maskini ni maskini kweli mpaka kiama; na tajiri hali Kadhalika. Ulikwishafika Kibera wewe. Wapi ktk miji ya Tanzania kuna slums kama zilizopo Kenya. Acheni bwana. Kenya kuna watu wa hovyo usipime, wengine wako huku Wakikuyu na Wajaruo, wanatusimulia pia. Wapo wengi tu, na kwa siasa nzuri za Tanzania wengi wana hali nzuri ya maisha. Ni matajiri wala hawabughudhiwi. Ukiwaambia warudi Kenya wanasema afadhali uwaue kuliko kurudi kule "motoni". Acheni bwana.

Nenda Kenya uone kama utapata ardhi ya kulima au kufugia. Ardhi yote imehodhiwa na akina Uhuru. Ni "miungu watu" wa Kenya ... The untouchables. Ati loyal families!
Maendeleo ya TZ yanakwenda sawia ktk maeneo yote mijini hadi vijijini. Nenda Kenya Kaskazini ukaone. Aibu!

Acheni kutulinganisha TZ na Nchi ya unyonge kama Kenya bwana. Ni jamaa wana publicity hao usipime! Nawafananisha na waingereza wanaoshinda kombe la dunia magazetini!

Ni suala la muda tu; Kwa mwendo tunaokwenda TZ, Kenya watakuja kutupigia magoti miaka si mingi. Hata hivyo, mbona tunawalisha mahindi na maharage mara nyingi tu. Hawana uwezo wa kujitosheleza kwa chakula.

Tanzania ni Nchi pekee Duniani iliyo na Serikali zinazojitegemea kuanzia ngazi ya kitongoji/mtaa.
Ardhi ni mali ya Serikali. Hakuna ubaguzi wa aina yoyote, hata Wakenya waliopo TZ wanapewa nafasi za uongozi almradi wanafaa, nk. Je, Kenya mambo haya yapo? Tunapendana hatubaguani. TZ imekwishakuwa fashion ya zamani kuoa au kuolewa na kabila lako! Kenya ipo hiyo?

Kenya wakitaka kupiga hatua sasa ya maendeleo wakubali kuja kujifunza Tanzania kwani kwa sasa hatuna la kujifunza kutoka Kenya.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU MBARIKI JPM
MUNGU IBARIKI AFRIKA
Asante sana mkuu 🙏. Umenifanya nitokwe na machozi kweli kweli kwa kuwakosa viongozi wetu wanne Wazalendo number one, Waasisi wa nchi yetu; Hayati Mwalim Nyerere (The Teacher) na Abed Aman Karume (Rais wa Mapinduzi ya Zanzibar, Hayati Magufuli (The Buldozer) na Hayati Waziri wetu Mkuu, Moringe Sokoinne (Mpinga Ulanguzi mkubwa Tanzania).
Watanzania tuko safiiii!
 
Back
Top Bottom