TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

Status
Not open for further replies.
Matendo ya utumishi wa Hayati JPM ni wazi yanastahili kumuweka katika ukurasa wa Mwenye Heri na pengine kuwa Mtakatifu..

Angalia alivokuwa Mchamungu, mzalendo, mwajibikaji, mwenye huruma na aliyejali Masikini na aliyeleta maendeleo kwa muda mfupi.

Anaondoka bila kunyonga wafungwa, kapewa kitubio dk za mwisho na mafuta ya wagonjwa.

Alimwogopa na kumtanguliza Mungu. Sitashangaa Korona hii tena itapotea ghafula kama last year kwa maombi na sayansi kiasi (despite mikusanyiko hii) . Je hiyo siyo miujiza wkt nchi zingine wanateseka sana pamoja na masharti magumu?

Huyu mkuu naamini tutakutana mbinguni.
Afanyiwe uchambuzi wa kuwa Mwenye Heri.
 
[emoji375][emoji375][emoji375][emoji375][emoji375][emoji375]
 
Kuwa wenye Kheri eee bac Sawa, ila labda atakayemtangaza awe Ben saanane na Azory!!
 
Kwa dini yenu hlo jepesi sana
 
Ndugu zangu,
Niseme tu ukweli, mama ni kama vile nilikuwa siamini kama atafuata nyayo za mwamba, ila kwa hotuba yake ya leo Dodoma, inaakisi uwejo wa JPM ndani yake na inanipa tumaini ya kuona maono aliyokuwa nayo JPM kutekelezeka na inawezakana ikawa zaidi ya hapo.

Maombi yangu kwa mama yetu, ajihadhari sana na remote control kutoka Msoga na lile genge la ccm maslahi binafsi that's fadhira oriented. Akiruhusu genge hili likawa karibu naye, watu tutaanza kummiss JPM mapema sana.

Kauli yake hii, imenipa tumaini ukweli na hofu niliyokuwa nayo kuanza kupungua.

Wale mlio kuwa na wasi wasi mama amesema, "Kwa wale mliokuwa na Mashaka, mwanamke huyu ataweza kuwa rais wa Tanzania! Nataka niwaambie Aliye simama hapa ni Rais wa JAMUHURI ya MUUNGANO wa TANZANIA" ~ Mh Samia Hasan Suluhu.

Mama yetu kaza, tena nenda speed ya supersonic, ili utufute machozi.

All the best mama yetu
Kejuu
 
Habarini wanajukwaa!!

Tukiwa tunaendelea na maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Rais wa JMT Hayati John P. Magufuli naona sasa hivi Musiba unataka kuwa kama kampeni za siasa yani kuna kundi linakaa linasifia mnaona NYOMI hatukatai museme hio NYOMI lakini inaonyesha dhahiri kabisa kauli hii imeanza kutumika kama siasa, kuwa nanga wapinzani eti Rais Magufuli alikua anapendwa tofauti na wao walivyokua kua wanasema.

Nikumbushe tu yule aliefariki ni RAIS tena wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania(JMT)sio KIBAKA Wa Mtaani na kifo chake kimeshitua wengi hata waliokua hawampendi wameguswa ndio maana wanaenda kuangalia wasiamini kama ni kweli kafariki, pia ijulikane Kifo hakijawahi zoeleka kinauma hata kama mtu ulikua humpendi akifariki lazima uumie kwa sababu kila mtu ashawahi kupatwa na msiba kwa hio anapofariki mtu yeyote unaemfahamu utaguswa tu hata kama Adui yako.

Hebu niwaombe tuache kufanya siasa kwenye hili swala.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…