TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

Status
Not open for further replies.

Gone too soon, lakini historia itakubeba... Rest in eternal peace, Jemedari![emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
R.i.p my president Magu,hakika mwendo umepiga, Watanzania tutaenzi na kuyalinda yale yote ulopigania kuifanya Tz iinuke kiuchumi.Pumzika kwa Amani Baba yetu
 
R.I.P PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA.

POLE ZA DHATI ZIFIKE KWA FAMILIA NA MH. SAMIA HASSAN SULUHU.

AUTOMATICALLY mama SAMIA NI RAIS.

Swali, je, atapewa pia uenyekiti wa chama? Au Ccm itahamisha magoli? najua ni mapema ila nauliza nijue.
 
Dunia tunapita, nimeamini sasa
R.I.P. The late John Joseph Pombe Magufuli.
  1. Utakumbukwa kwa uchapaji wako wa kazi na miradi lukuki.
  2. Utakumbukwa pia kwa chuki,uonevu na ukandamizaji wa Haki za raia hasa Wapinzani, Wastaafu,Vyeti fake n.k
  3. Utakumbukwa pia na wale ambao ndugu zao walipotezwa katika mazingira ya kutatanisha kama Ben Saanane, Azory Gwanda, Alphonce Mawazo n.k.
  4. Utakumbukwa kwa tukio ovu kabisa la kushambuliwa kwa Mhe. Antipas Tundu Lissu mchana ,kweupe pale Dom viwanja vya Bunge na hadi leo hakuna aliyekamatwa!
  5. Utakumbukwa pia kwa kutengeneza Wakimbizi nje ya nchi kwa uonevu uliowatendea baadhi ya Watz wenzako.
Huu ni msiba ambao unaweza kuwa somo na fundisho kwa Utawala wa CCM na wote walokuwa wafuasi wa Magufuli. Wakti mwingine Mungu anaingilia kati kukatisha uhai wa Mtawala pale uovu wake unapopitiliza mipaka. People may ask questions like: Kwanini Rais huyu wa A5 amekatizwa Uhai wake hata kabla hajamaliza muda wa Awamu yake ya 5 phase 2....Why?

Tulianza na 1st Term alimaliza peacefully(J.K. Nyerere), 2nd Term alimaliza peacefully(Mzee A.H.Mwinyi), 3rd Term peacefully(Ben W. Mkapa) na 4th Term peacefully(J.M.Kikwete).

Biblia inasema: TAKENI AMANI NA WATU WOTE. Wakti mwingine ukiwatendea watu ubabe na jeuri inakutengenezea mazingira ya kuihama dunia soonest.
 
JPM IS MY SON'S LEGACY
JPM IS MY SON'S LEGACY

Naomba COMMENT yangu iwe Shahidi Siku za huko mbele TUTAKUJA kumkumbuka Raisi MAGUFULI

"hauwezi jua thamani ya kitu mpaka kipotee "
 
Tumepoteza. Lakini hatutapotea

Tumefiwa na atakayeishi nasi milele

Nani nyuma ya Magufuli?

Jibu. Mamilioni ya Watanzania

Nalia nalia nalia nalia nalia nalia sana. Ila naona furaha mpya ya milele.

Kwa hisani ya mtu wa tanzania!
 
Pumzika kwa amani kamanda mkuu.Ahsante kwa yote,kwangu umeacha legacy kwa uamuzi wako mgumu na sahihi kuhusu corona,na umekugharimu maisha yako baba.dah!!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…