TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

Status
Not open for further replies.
Una uhakika huo wizi ulisimama/haukuwepo kipindi hiki? Au ulibadili tu uelekeo! Kutoka kundi la awali na kwenda kundi lingine?

Kutesa kwa zamu. Ngoja na nyinyi mrudi kwenu kuchunga ng'ombe.
 
Tunajua jamaa alikuwa anapiga yeye na team yake, ila wengine walikuwa wanakipata cha moto wakidokoa

Sasa ni mwendo wa

1. Wizi kwenye harimashauri
2. Wizi kwenye wizara kila mtu ataiba itajulikana mbeleni
3. Wizi kwenye mifuko ya jamii
4. Wizi kwenye mashirika ya umma

Nchi hii itakuwa mikononi mwa deep state wizi utakuwa wizi

Mafisadi wazungu watarudi na mikataba ya wizi deep state itauza nchi maana hawana huruma na nchi

Mark my words tutapoteana
Ndo mana tulikua tunataka katiba mpya kubadili ule mfumo lakini hata yeye alishindwa kusimamia mabadiliko ya mfumo nae ni mpigaji tu alikua
 
Tunajua jamaa alikuwa anapiga yeye na team yake, ila wengine walikuwa wanakipata cha moto wakidokoa

Sasa ni mwendo wa

1. Wizi kwenye harimashauri
2. Wizi kwenye wizara kila mtu ataiba itajulikana mbeleni
3. Wizi kwenye mifuko ya jamii
4. Wizi kwenye mashirika ya umma

Nchi hii itakuwa mikononi mwa deep state wizi utakuwa wizi

Mafisadi wazungu watarudi na mikataba ya wizi deep state itauza nchi maana hawana huruma na nchi

Mark my words tutapoteana
Ikiwa unakiri alikuwa anapiga na kundi lake kipi kipya sasa
Siinaweza kuwa vzr kwamba mzunguko utakuwepo kwa watu wengi badala ya genge la watu wachache

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Heart problems don’t just come, there are signs etc which can easily be detected various tests. Wamemua huyo ili wale nchi, alikuwa anakata corruption. Now they are rejoicing. 14 days for a sitting President. Masafari ya ulaya dada yataanza kwa ladies.
Ni wakati wa taifa kuungana na kuomboleza kwa pamoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiukwel gap ya Magufuli hakuna mtu ataliziba, kaacha viatu vikubwa mno hakuna vitakaemtosha.
Kuna wengine wanachukulia ‘Utani’ lakini seriously Tanzania tumepoteza mwanga uliokua unamulika mbali japo ulikua wenye kutuletea maumivu makali machoni petu.

Kuna siku tutasema wote kwa pamoja Bora Magufuli kwa sababu alikua mwenye maono mengi, makubwa na mazuri kiasi kwamba sidhani kama kuna mtu mwingine alie nchini mwenye maono kama yake

Rest In Peace Mr. President 😭
 
Sio rahisi, mzee ameacha legacyjapo sielewi kwa nn watu wameamka bila hofu na wanaelekea makazini.....wkt wa mwl tiki seace chumbani, watu kimya maredio yakaimba, yakatuomboleza nk
Mambo yamebadilika kipindi kile watu walikuwa wanahisi bila Mwalimu TZ haiwez kuwepo utatokea mpasuko ndiyo maana walijawa hofu.
 
Subiri wamachinga nao waanze kukipata!

Nakwambia machadema yataanza kuwa ya kwanza kummiss Magufuli
 
View attachment 1724937

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Joseph Magufuli amefariki dunia.

Taarifa rasmi iliyotolewa kwa umma na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan kupitia Televisheni ya Taifa (TBC) leo usiku Machi 17, 2021 saa 5 usiku imeeleza kuwa Rais Magufuli amefariki dunia leo majira ya saa 12 jioni kwa maradhi ya Moyo akiwa katika Hospitali ya Mzena jijini Dar. Rais Magufuli alilazwa tarehe 6 Machi katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa tatizo la moyo wa mfumo wa umeme ambalo limekuwa likimkabili kwa takirbani miaka 10.

Nchi itakuwa katika kipindi cha maombolezo kwa siku 14 na bendera zitapepea nusu mlingoti

View attachment 1728353




WASIFU:

Dkt, John Joseph Pombe Magufuli ni mwalimu na mtalaamu wa kemia akiwa na Shahada ya Uzamivu (PhD).

Kuzaliwa

Alizaliwa Oktoba 29 mwaka 1959 huko Chato mkoani Geita, Kaskazini magharibi mwa Tanzania.

Elimu

Magufuli alipata elimu ya msingi katika shule ya msingi Chato kuanzia mwaka 1967 hadi 1974.

Mwaka 1975 alijiunga na Seminary ya Katoke iliyo Biharamulo, Kagera kwa Elimu ya sekondari na kisha kujiunga na shule ya sekondari ya Lake iliyoko Mwanza hadi 1978 alipohitimu.

Mwaka 1979 alijiunga na shule ya Sekondari ya Upili ya Mkwawa, Iringa kwa ajili ya masomo ya kidato cha tano na sita na kuhitimu Mwaka 1981.

Mwaka 1981 hadi 1982 alisomea Stashahada (Diploma) ya Ualimu wa masomo ya Sayansi katika Chuo cha Ualimu cha Mkwawa, Iringa Masomo makuu yakiwa Kemia na Hisabati

Akiwa kazini, Magufuli aliamua kujiendeleza kwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka 1985 hadi 1988 alipotunukiwa Shahada ya Ualimu katika masomo ya Kemia na Hisabati.

Mwaka 1991 hadi 1994 alisomea Shahada ya Uzamili ya Kemia (Msc. Chemistry) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Tanzania na Chuo Kikuu cha Salford, Uingereza

Mwaka 2009 alitunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) ya Kemia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Mafunzo ya Kijeshi

Kati ya Mwaka 1983 na 1984, Magufuli alipitia mafunzo ya kijeshi kwa mujibu wa sheria kwenye Kambi za Jeshi la Kujenga Taifa Makutupora - Dodoma, Makuyuni - Arusha na Mpwapwa - Dodoma.

Kazi

Baada ya kufuzu Stashahada ya Ualimu, alifundisha masomo ya Hisabati (Mathematics) na Kemia (Chemistry) katika shule ya Sekondari Sengerema kuanzia mwaka 1983.

Baada ya hapo akafanya kazi kama Mkemia katika Chama cha Ushirika cha Nyanza huko Mwanza hadi mwaka 1995.

Siasa

Nyota ya Magufuli liana kung’aa katika siasa, alipogombea na kushinda ubunge eneo la Chato mwaka 1995. Mwaka huo huo aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi, nafasi aliyohudumu hadi Mwaka 2000.

Baada ya uchaguzi Mwaka 2000, aliteuliwa kura Waziri wa Ujenzi, nafasi aliyohudumu hadi Mwaka 2006 alipohamishwa kwenda Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi alipokaa hadi Mwaka 2008.

Mwaka 2010, aliteuliwa kawa Waziri wa ujenzi kwa mara ya pili na kudumu kwenye nafasi hiyo hadi Mwaka 2015.

Urais

Mnamo Tarehe 12 Julai 2015, alichaguliwa kuwa mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Akiwa na Samia Suluhu Hassani kama mgombea mwenza.

Tarehe 29 Oktoba 2015 alitangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushindi wa kura 8,882,935 sawa na 58.46%.

Magufuli aliapishwa kama Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 5 November 2015.

Muhula wa Pili

Mnamo tarehe 30 Oktoba 2020, Tume ya Uchaguzi Tanzania ilimtangaza John Pombe Magufuli kama rais kwa muhula wa pili kwa kupata kura milioni 12.5 hiyo ikiwa ni sawa na asilimia 84 akiwa amemshinda mshindani wake wa karibu, Tundu Lissu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) aliyepata kura milioni 1.9.

Baadhi ya Nukuu zake:

"Ni nafuu wakuchukie... uonekane wewe sio Mwanasiasa mzuri (Unpopular) kwasababu sikuja kutafuta Mchumba. Nimekuja Kufanya kazi za Watanzania." - Septemba 7, 2017


Soma pia:

1) Nukuu toka kwa Rais Magufuli (QUOTES)

2) Magufuli: Kila atakayetaka kuiokoa nafsi yake atapoteza...


VIDEO:



Baadhi ya Hotuba zake:

Hotuba ya Rais Magufuli kufungua Bunge la 12: Utumbuaji majipu utaendelea ili kuhakikisha Watumishi wanatenda kazi kwa mujibu wa Sheria na Kanuni - Novemba 13, 2020

Bungeni Dodoma: Rais Magufuli avunja Bunge la 11. Asema ajira 6,032,299 zimetengenezwa, Viwanda vipya 8,477 vimeanzishwa - Juni 16, 2020

apumzike kwa amani shujaa wetu historia ya Tanzania itamkumbuka daima, hakika tumepoteza kiongozi shupavu
 
Samia futilia mbali Uchaguzi wa serikali za Mitaa ili kuirudisha nchi kwenye mstari. Futa ubunge wa Covid-19 kupitia Chadema. Ondoa wakurugenzi , Ma-RAS, Ma-DAS wote ambao ni makada wa chama. Vyeo hivyo washike wataalamu ambao ni watumishi wa umma.
 
Tunajua jamaa alikuwa anapiga yeye na team yake, ila wengine walikuwa wanakipata cha moto wakidokoa

Sasa ni mwendo wa

1. Wizi kwenye harimashauri
2. Wizi kwenye wizara kila mtu ataiba itajulikana mbeleni
3. Wizi kwenye mifuko ya jamii
4. Wizi kwenye mashirika ya umma

Nchi hii itakuwa mikononi mwa deep state wizi utakuwa wizi

Mafisadi wazungu watarudi na mikataba ya wizi deep state itauza nchi maana hawana huruma na nchi

Mark my words tutapoteana
Huwa unawaza mabaya tu kwa wenzako?
Huna jema juu ya nchi hii?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom