TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

Status
Not open for further replies.
hakika kifo ni funzo kwa binaadamu wote, hakuna atakaye ishi milele, haijalishi wewe ni kijana, mzee, bibi, mama au mtoto, una nguvu au dhaifu sote tutarejea kwa Mungu.

Jambo la msingi tuishi kwa kumu hofu Mungu na pia tutende mema kwa binaadamu wenzetu. kila kiongozi ktk nafasi yake asifikirie kuiba au kudhulumu au kufanya ubadhirifu kwa mali ya umma.

Moyo wangu umeumia sana lkn nimekubaliana na kilichotokea.
tuwe imara, haswa viongozi wetu ktk nafasi mbalimbali .
 
Utawala wa John Magufuli utakumbukwa kwa Uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu, Ni utawala uliokuwa wa kikatili sana, ni utawala ulioshindwa kuleta umoja katika nchi, Utawala uliojifanya unajua kila kitu. Wajinga walikuwa wengi mnoo.
Hakika nchi ianze upya. Mtaani huku kilo kama kawaida na mambo hasi tu. Huwezi amini hakuna hata mmoja naona anasikitika.
 
Utawala wa John Magufuli utakumbukwa kwa Uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu, Ni utawala uliokuwa wa kikatili sana, ni utawala ulioshindwa kuleta umoja katika nchi, Utawala uliojifanya unajua kila kitu. Wajinga walikuwa wengi mnoo.

Aliyotuepusha nayo ni mengi kuliko izo haki za mabeberu nk! Kila binadamu anamakosa yake hata mimi na wewe
 
Mzena ni Hospitali ya nani?
Ni hospitali ya kumbukumbu ya mzee Emilio Mzena ambae alikuwa ni mkurugenzi mkuu wa kwanza wa TISS enzi ya Mwalimu Nyerere.

Hapo wanatibiwa maofisa wote na familia zao.
 
Walidanganya Watanzania. Badala wangesema ukweli ili aombewe. Yaani viongozi hadharani kusema uongo wakati inajulikana wazi alilazwa. I will never trust a politician.
Hivi kweli kiongozi Mkubwa kabisa anatudanganya hadharani halafu leo wanatwambia alikuwa anaumwa! Hivi kuna kauli watakuja kutwambia tukawaamini?
 
Walidanganya Watanzania. Badala wangesema ukweli ili aombewe. Yaani viongozi hadharani kusema uongo wakati inajulikana wazi alilazwa. I will never trust a politician.
Ni bora hata mama Samia alisema kukaguliwa kaguliwa lakini Majaliwa Kwa kweli huyu Baba anapwaya.
 
❤️ problem! Hivi kweli walikosa moyo wa kumpa kipenzi chetu kweli!
 
Ni hospitali ya kumbukumbu ya mzee Mzena ambae alikuwa ni mkurugenzi mkuu wa kwanza wa TISS Enzi ya Nyerere (kama sikosei).

Hapo wanatibiwa maofisa wote na familia zao.
Basi tuboreshe Hospitali za Umma.
 
Hivi ningali naota, au kweli imetimu!

Haya yanayonipita, kwenye wangu ufahamu,

Jemedari amekata, hatunaye muadhamu!

Natamani iwe ndoto!
 
Walidanganya Watanzania. Badala wangesema ukweli ili aombewe. Yaani viongozi hadharani kusema uongo wakati inajulikana wazi alilazwa. I will never trust a politician.
ALIE SEMA UONGO ALIE SEMA UONGO tupo hapa! Hii sasa kuna watumishi wa mungu wanakufuru kwa sababu ya uongo wa watu wachache MLIFANYA UONGO NI MAZOEA mmetugharimu.

Wengine wanasema mungu hapangiwi. John alikuwa mtu wa dini. soma biblia yako musa alivyo ongea na mungu kuhusu watu wa sodoma walitoka watu 50 mpaka 10 watakao kuwa na imani mji usichomwe.

REHEMA HII TUNGEIPATA KAM LUTU NAAMIN.
 
JPM had a huge vision for his country, now walaji wamemuua. These people should be locked up! Eti heart problems, the guy was so fit, he looked Like a 25 year old man.

Angalia hiyo miradi mikubwa itakavyosimama. They have been planning how to divide the massive cake among themselves.

It is possible he died 2 weeks ago! Tell us the truth you corrupt leaders.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…