Zote ni Neno la Mung mkuu Gavana. Bwana Yesu hujifunua kwa jinsi na namna zote za mapenzi yake atakavyo ya timizwe. Kwa nini Biblia ziko kwa lugha nyingi? Mungu anataka kweli yake iwafikie wote. Shetani hataki kweli iwafikie wanadamu maana watamjua na watampinga na kumkimbia kuelekea mahali salama kwa ajili ya kuponya nafsi zao. Hii ya'kumpinga itakuwa ni kupitia kweli walio ijua kuhusu shetani na kuona kwamba anawalisha tango mwitu. Atatumia akili gani kuweka vikwazo hivi? Viko vingi ikiwemo na lugha. Ili achague mawakala wake wachache waijue lugha waendelee kuwalaghai walio wengi.
Mfano mzuri ni siku ile Roho Mtakatifu aliposhuka kutoka mbinguni. Inaitwa siku ya Pentekosti"50days" baada ya Yesu kutoka kaburini na kuishinda mauti/kifo na kaburi. "10days" baada ya Yesu kupaa na kuelekeacMbinguni. Roho Mtakatifu alishukia wanafunzi wa Yesu waliokutana kuabudu siku ile. (Matendo ya Mitume sura 2. Soma tafadhali, pengine utapato Neema ya Mungu uone huu ukweli unaopotoshwa). Uone ujasiri wa Petro aloupata baada ya kumpokea Roho Mtakatifu. Hakuwa tena yule Petro aliye mkana Bwana Yesu mara tatu. Alikuwa akijibishanavna kuwa shuhudia wanao weza kumchinja ama kumtundika kichwa chini miguu juu na kumuua.
Mipango ya Mungu siku zote ndivyo inavyoenda kwa upako wake. Kumbuka kipindi hicho walikuwepo watu kutoka pande zote za dunia wakiwa wamepanda Yerusalemi kuazimisha moja ya ibada iambatanayo na sherehe ya maashimisho ya dini ya Kiyahudi.
Gess what happened. Roho wa Mungu/ Mtakatifu aliwashukia kama Bwana Yesu alivyo wa ahidi na kuwa amuru wasubirie mpaka hapo atakapowashushia kutoka mbinguni Roho Mtakatifu. Ishara ya Roho ilikuwa na kwa kuonekana alama ya ndimi za moto angani na kuwaingi neno zuri kuwajaza wale wanafunzi walio kusanyika na walimanifesti kwa kunena kwa lugha za mataifa yote ya wale waliokuwa wakiwashuhudia.
Na walinena si maneno tu, bali walishudia Matendo Makuu ya Mungu wa Mbinguni aliyoyatenda kupitia Bwana Yesu. Unajua kwa nini muujiza ule ishara za ndimi za moto angani? Baada ya ibada ile wale walio kusanyika Yerusalemi kipindi kile walirudi huko walikotokea duniani kote kuanza kuihubiri Injili kwa kushudia walichokiona na kusikia kupitia karama ya kuneba kwa lugha ya Roho Mtakatifu. Neno la Mung lokarneo ulimwenguni kote kama vile moto usambaovyo nyikani. Mungu ni Neno la Uzima na tena ni Moto ulao., Upanga/ Jambia likatalo kuwili.
Hii ina kupa picha gani? Injili lazima iwafikiwe wote kwa namna ambayo Mungu anataka. Kabla ya siku ya mwisho wa dunia /kiama. Hii haiji mpaka Injili imehubiriwa pote duniani. Ili wa kudharau waseme tunao hubiri tumelewa mvinyo mpya tena asubuhi.
Hii uliyoleta hapa ni hoja tena ya wale ambao wengi wao hudanganywa na shetani kuwa Roho Mtakatifu ni nabii/ mtume flani . Ni uongo kwa mujibu wa imani ya Kikristo lakini. Ni uongo mweupe na bahati mbaya sana Biblia inatumiwa kama kilelezo chacl kujengea hoja. Kwanza hawana Roho Mtakatifu wa kuwasaidia kujua kwa ukamilifu kilicho kwenye Biblia. Kwa maana hiyo shetani ndiye huwasaidia kuijua nusu kweli ama robo na nusu ya ukweli wa Kibliia. Ili awatumie kuwapeleka jehanamu woa na watu watakao kuwa wame wadanganya.
Hivyo ni wito baada ya kuelewa haya basi Biblia na isitumike kuutetea huo uongo Waachwe watu waelewe na wakusaidika asidike aepushwe na Jehanamu lile tanuri la moto wa kuzimu usio zimika milele yote.
Ukristo una madhehebu mengi tofauti tofauti na ni vigumu kwa sasa kutambua imani sahihi ya Kikristo. Vyovyote ulivyo, katika muktadha wa sasa, hakuna aliye karibu zaidi na mafundisho asilia ya mitume.
Mungu pekee ndiye ajuaye ni lini Wakristo wataweza kutoa nakala sahihi (asilia) ya kitabu chao (Biblia).
Mtu atashangaa, juu ya idadi ya matoleo ya Biblia yaliyopo leo hii. Kila moja linatofautiana na jingine, ndio, kila moja linadai kuwa yeye ndio toleo asilia.
Matoleo yote hayo yameshawahi kutangaza duniani kuwa, yenyewe ni ufunuo mtakatifu.
Rejeo lao lililo tayari lipo katika (2 Timotheo 3:16), isemayo “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho...”
Lakini kile wasichokifahamu Wakristo ni kuwa, “Kwa hakika, yaliyomo katika Biblia zao si Maandiko matakatifu isipokuwa ni hekaya, fikra, matukio na tamaduni tu.”
Tatizo hilo linachanganya zaidi pale tunapojua kuwa baadhi ya matoleo ya Biblia yana vitabu vingi zaidi kuliko mengine.
Toleo la Orthodox (OVC), lina vitabu 86;
Toleo la Charismatic (CV), lina vitabu 76;
Toleo la Roman Catholic (RCV), lina vitabu 73;
na matoleo yote ya Kiprotestanti yana vitabu 66, likiwemo The New World Translation of the Holy Scripture [1984] (NW), linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova na matoleo mengine kama vile the King James [1611-1942] (KJ),
American Standard [1901-1944] (AS), Rivised Standard [1971] Second Edition (RS) Jerusalem Bible [1966] (JB), Good News Bible (1954: iliyochapwa 1956), Ronald A, Knox (Kx), New International Version (NIV), na motoleo mengine yasiyo na idadi.
Zaidi ya hayo, vipi kuhusu hoja ya Warejeaji wanosifika wa Biblia ya the Rivised Standard Version (RS), Rivised Edition ya 1952, na kwa Agano Jipya, Second Edition ya 1971, by Wm. Collins Sons & Co. Ltd. Iliyochapwa na Canadian Bible Society, isemayo katika Utangulizi wake:
(1) “Naam, Toleo la King James lina dosari kubwa mno.... dosari hizo ni nyingi sana na hatari sana kiasi cha kupelekea kuitishwa wito wa kurekebishwa kwa tafsiri yake ya Kingereza.”
(2) “Toleo la King James la Agano Jipya liliegemea katika mandiko ya Kigiriki yaliyoharibiwa kimakosa” Vipi kuhusu hoja ya Mashahidi wa Yehova katika chapa ya Mwamko ya Septemba 1951 inayoeleza; “Biblia ina makosa 50,000!”
Na vipi kama nikisema, kinyume na imani yenu, kuwa “Katika Waandishi wanne wa Injili Hakuna hata mmoja aliyekuwa Mwanafunzi wa Yesu ”
Katika (Luka 6:14-16 na Marko 3:17) tunaona yametajwa majina ya wanafunzi kumi na wawili na Yesu (AS).
Huku majina Mathayo na Yohana yamo, na majina Marko, Luka na Paulo hayajatwaja.
Hata hivyo, kutokana na nkuu zifuatazo, utagundua kuwa hizo Injili mbili zinatajwa kuwa ni za Mathayo na Yohana kwa kuwaheshimu tu, kwani ziliandikwa na mtu wa tatu. Soma nakala halisi ya mstari wa (Mathayo 9:9):
"Naye Yesu alipokuwa akipita kutoka huko aliona mtu ameketi forodhani aitwaye Mathayo, akamwambia nifuate. Akaondoka akamfuata."
Na katika (Yohana 21:24):
"Huyu ndiye yule mwanafunzi ayashuhudiaye haya, na aliyeyaandika haya; nasi twajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli?"
Katika aya ya kwanza, mwandishi anasimulia tu kile kilichotokea kati ya Yesu (AS) na Mathayo, huku katika aya ya pili, ni wazi kuwa kiwakilishi “nasi” kinawakilisha mwandishi.
"Huyu ndiye yule mwanafunzi ayashuhudiaye haya, na aliyeyaandika haya; nasi twajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli?"
Katika aya ya kwanza, mwandishi anasimulia tu kile kilichotokea kati ya Yesu (AS) na Mathayo, huku katika aya ya pili, ni wazi kuwa kiwakilishi “nasi” kinawakilisha mwandishi.