Rais wa Ujerumani awaomba radhi Watanzania kuhusu uhalifu wa Wajerumani wakati wa Vita vya MajiMaji
Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier siku ya Jumatano ameomba radhi na kueleza kufedheheshwa kwake na uhalifu uliofanywa wakati wa utawala wa kikoloni wa Ujerumani nchini Tanzania, wakati huo ikiitwa Tanganyika na kuahidi kuongeza uelewa kuhusu madhila hayo katika nchi yake, imerpoti tovuti ya DW.
Kadhalika taarifa hizo za Ujerumani kuomba radhi zimechapishwa na Makumbusho ya Taifa ya Tanzania katika ukurasa wake wa mtandao wa X, zamani Tweeter.
“Ningependa kuomba radhi kwa kile ambacho Wajerumani walikifanya kwa mababu zenu hapa,” alisema Steinmeier alipotembelea makumbusho ya vita vya Maji Maji, yaliyopo mji wa Songea, mkoani Ruvuma, Kusini mwa Tanzania.
Source: BBC
Halafu kuna watu fulani humu wanasema uhalifu Tanganyika umefanywa waarabu. Wanatumia neno waarabu kwa sababu ni waislam.
Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier siku ya Jumatano ameomba radhi na kueleza kufedheheshwa kwake na uhalifu uliofanywa wakati wa utawala wa kikoloni wa Ujerumani nchini Tanzania, wakati huo ikiitwa Tanganyika na kuahidi kuongeza uelewa kuhusu madhila hayo katika nchi yake, imerpoti tovuti ya DW.
Kadhalika taarifa hizo za Ujerumani kuomba radhi zimechapishwa na Makumbusho ya Taifa ya Tanzania katika ukurasa wake wa mtandao wa X, zamani Tweeter.
“Ningependa kuomba radhi kwa kile ambacho Wajerumani walikifanya kwa mababu zenu hapa,” alisema Steinmeier alipotembelea makumbusho ya vita vya Maji Maji, yaliyopo mji wa Songea, mkoani Ruvuma, Kusini mwa Tanzania.
Source: BBC
Halafu kuna watu fulani humu wanasema uhalifu Tanganyika umefanywa waarabu. Wanatumia neno waarabu kwa sababu ni waislam.