Uchaguzi 2020 Rajab Abdul "Harmonize" kugombea ubunge Tandahimba

Uchaguzi 2020 Rajab Abdul "Harmonize" kugombea ubunge Tandahimba

Kuingia bungeni unatakiwa kujua kusoma na kuandika tu chief
Bungeni ni kisima kama sio chem chem za fikra kwa taifa

Mijadala mipana na maazimio mbali mbali yanayopitishwa bungeni yana athari za moja kwa moja kwenye taifa

Ili kupata athari chanya kwenye matokeo ya maazimio na mijadala hiyo tunahitaji watu wenye weledi mkubwa kujadili mambo hayo!

Majadiliano ya kijinga hushirikisha watu wajinga na matokeo yatakuwa ya kijinga

Majadiliano na maazimio ya aina hiyo ndio yaliyolifikisha taifa hapa
 
Kama Taifa tumefikia pabaya
Kama Kingwendu alijaribu ndipo utambue tunarudi nyuma miaka 50 kila miaka mitano
 
Kwani hao wabunge wana kipi kipya kumzidi Harmonizer?
Kwanza yeye ni creative kuliko wengi
Ubora wa bunge unaamua mustakabali wa taifa lolote kwa kuwa bungeni ni kisima cha mijadala na maazimio yanayoliathiri taifa moja kwa moja

Bunge lenye wabunge wapumbavu litakuwa linajadili ajenda za kipumbavu na kupitisha maazimio ya kipumbavu hivyo kufanya taifa kupoteza muelekeo
 
hahahahah aliyesema wanawake hatupendani hakukosea, haya weka papa lako tuone, mbona unalionea wivu la kwangu?? mala.ya mbovu wewe!
Hahah daah naona kweli umenogewa, genious wa JF huyo.

So photogenic
 
Hebu tuweni serious kidogo na uongozi wa nchi yetu. Sidhani kama msanii Harmonize anajua hata majukumu ya mbunge.

Hajawahi hata kuwa na wazo la kugombea ubunge hapo kabla, lakini toka Rais Magufuli "Amtanie" jukwaani kuwa angependa awe mbunge ameichukulia serious hiyo kauli kana kwamba ni agizo au amri.

Mheshimiwa Rais ni mtu wa utani sana; alikuwa akitania tu kunogesha hotuba na siyo vinginevyo.

Bwana mdogo anawaambia watu kuwa kama Rais amesema basi yeye hana budi kukubali na kugombea ubunge? Kwani anayekwenda kuwatumikia wananchi ni Rais?

Hana mikakati yoyote ile wala nia, kampeni yake kubwa itakuwa "Magufuli kasema nigombee".
Mbona Sugu Prof Jay na Mzee Yusuf wamo bungeni na wamefanya vizuri?!

Sifa kuu ya mbunge ni kujua kusoma na kuandika!
 
Spika ajaye atapata tabu sana kuwavua heleni na kuwapandisha suruali juu ya kiuno, aina hii ya Wabunge iwapo kwa 'bahati mbaya' wataingia huko mjengoni.

Bado na wale wa Bongo Muvi!🤔 Hakika patachimbika.
 
Back
Top Bottom