Leo tuangalie upande ambao SEBULE na VYOO vinapotakiwa vikae
Katika pande zote nne yaani Kaskazini, Kusini, Mashariki na Magharibi, upande wa Kaskazini ndio upande ambapo unapokea jua ama joto kwa kiasi kidogo na upande wa Kusini ndio upande ambao unapokea jua ama joto kwa kiasi kikubwa katika masaa yote ya siku (asubuhi mpaka jioni). Upande wa Mashariki hupokea joto jingi kuanzia asubuhi mpaka mida ya mchana, na upande wa Magharibi hupokea joto jingi kuanzia mchana mpaka jioni
Sebule inatakiwa ielekee Kaskazini kwa sababu ni sehemu ambayo muda mwingi watu watakuwa hapo (asubuhi mpaka jioni) hivyo haitakiwi iwe upande ambao utakuwa sio rafiki kukaa katika mazingira hayo
Tukija upande wa Kusini ambao unapokea joto jingi zaidi katika masaa yote ya siku, kitu ambacho unaweza kuweka upande huu (kusini) ni vyoo na mabafu. Hii ni kwa sababu chooni sio mahali ambapo watu hukaa muda mrefu, watu hukaa muda mfupi na pia ni kwa mara chache.
Ramani, Makadirio na Ushauri wa kitaalam tuwasiliane +255(0)624068809