RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

hapo fika and hope ibaki as is. Tanzania kwa watu wake ni poa na kujitambulisha inaridhia.!!
good suggestion.
Sasa mkuu tatizo ni kwamba licha ya kwamba wote bado tunaipenda Tanzania na tungependa tuendelee kuitwa watanzania, lakini sasa kwa mueleke wa katiba ijayo (kama ikipita) tutakuwa na serikali tatu , ambapo ni lazma sisi wa huku (iliyokuwa Tanganyika) ama tukubali kujiita tena Tanganyika; au tujitafutie jina jengine tulipendalo.Nje ya hapo hakuna chaguo.Mimi nilipendekeza serikali moja ili kuondoa mambo haya ila wazo langu halijapitishwa na tume.
 
Hili lenyewe la Tanzania ukiwa nje ya nchi mtu akauliza unatoka wapi ukasema Tanzania swali linalofuata hama ni Where is Tanzania au Is Tanzania near Nigeria. Njia rahisi huwa ni kusema Tanzania is near Kenya. Sasa ikiitwa hiyo Tanzanite si ndo watasema, Is Tanzanite one of the Caribbean Islands? Hapo ndo tutachoka kabisa. Bora tubaki na hiyo Tanzania kiugumu ugumu
Wengi wanaijua bongo ilipo ila hawa wazungu hua wanajidai tu kukudhalilisha na wewe unaamini.
 
Lakini mkuu, ukumbuke kwamba Jaji Warioba alisema, namnukuu, "Tume ilifikia uamuzi wa kupendekeza mfumo wa Serikali tatu. Yaani Serikali ya Shirikisho, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar."

Angalia vizuri ktk rangi nyengundu, tume inapendekeza serikali ya "Tanzania Bara." Imekwepa kusema "Tanganyika." Kwa nini? Labda tushauri kwanza kwamba katika rasimu warekebishe mahali hapo ili pasomeke kwamba "Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar." La sivyo, jina litakalorejeshwa kwa bara litakuwa hilo lililopendekezwa na tume.
Sasa mkuu hapo kutakuwa na mkanganyiko.Utakaposema "Serikali ya shirikisho" si lazma useme serikali ya shirikisho ya wapi? Sasa si kutakuwa na serikali ya "Shirikisho ya Jamuhuri ya Tanzania" na "Serikali ya Jamuhuri ya Tanzania bara"? hii ndio itakaaje?
 
Miiko ya uongozi wa Umma sehemu ile ya pili kifungu 21 (3) ; Bado imekaa kuwalinda baadhi ya watu; Na kifungu Kimekaa Kifadhira zaidi, kwa wastaafu ktk swala la kupata uraji kwenye mashirika ya Umma hata baada ya kustaafu; Haiwezekani tuendelee kufanya Recycling ya watumishi wa Umma kwenye mashirika ya Umma. kifungu kisomeke hivi; Hairuhusiwi/ marufuku kwa mtumishi wa Umma aliyestaafu kwa mjibu wa sharia kupewa nafasi tena kwenye chombo cha Umma. Taifa Tunasema ajira ni tatizo , je inakuwaje mtu astaafu halafu aendelee kuwa na umuhimu, tena wa kubana nafasi kwa kazazi kilichoko chini yake.Basi labda turefushe umri wa kustaafu mtumishi wa Umma, vinginevyo tutakula matapishi ya katiba ya sasa, Kifungu kirekebishwe na hakionyeshi kuwajali watu wasiokuwa na ajira . Hii ni ujanja ujanja wa kupata mianya ya kupeana fadhira zilizozoeleka baada ya watu kustaafu. HAPANA HAIWEZEKANI TUACHE MAZOEA, LAZIMA TWENDE NA WAKATI, MTUMISHI AMESTAAFU BASI APUMZIKE NA KULA PENSION YAKE KWISHA.
 
Lakini mkuu, ukumbuke kwamba Jaji Warioba alisema, namnukuu, "Tume ilifikia uamuzi wa kupendekeza mfumo wa Serikali tatu. Yaani Serikali ya Shirikisho, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar."

Angalia vizuri ktk rangi nyengundu, tume inapendekeza serikali ya "Tanzania Bara." Imekwepa kusema "Tanganyika." Kwa nini? Labda tushauri kwanza kwamba katika rasimu warekebishe mahali hapo ili pasomeke kwamba "Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar." La sivyo, jina litakalorejeshwa kwa bara litakuwa hilo lililopendekezwa na tume.
tazama hapa,Nadhani tusome vema.4.Tanganyika itaitwa jimbo la Tanganyika na Zanzibar itaitwa jimbo la Zanzibar na kila jimbo litaongozwa na Gavana.
 
Sasa mkuu hapo kutakuwa na mkanganyiko.Utakaposema "Serikali ya shirikisho" si lazma useme serikali ya shirikisho ya wapi? Sasa si kutakuwa na serikali ya "Shirikisho ya Jamuhuri ya Tanzania" na "Serikali ya Jamuhuri ya Tanzania bara"? hii ndio itakaaje?

Ndiyo mapendekezo ya tume hayo. Tungoje wataalamu watatufafanulia. Lakini nafikiri hapajakaa vizuri hapa.
 
tazama hapa,Nadhani tusome vema.4.Tanganyika itaitwa jimbo la Tanganyika na Zanzibar itaitwa jimbo la Zanzibar na kila jimbo litaongozwa na Gavana.
Basi sasa tatizo lipo hapo kwenye Jimbo la Tanganyika.Hapo ndio pananipa shida.
 
Sasa mkuu hapo kutakuwa na mkanganyiko.Utakaposema "Serikali ya shirikisho" si lazma useme serikali ya shirikisho ya wapi? Sasa si kutakuwa na serikali ya "Shirikisho ya Jamuhuri ya Tanzania" na "Serikali ya Jamuhuri ya Tanzania bara"? hii ndio itakaaje?

Kutakuwa na serikali ya shirikisho yaani fedaral Republic of Tanzania iliyotokana na muungano wa tanganyika na zanzibar. pia kutakuwepo na serikali ya tanganyika na ile ya zanzibar ambayo yataitwa majimbo na yataongozwa na Governors.

Hapa Nimenukuu "TANGAZO LA JAMHURI
[FONT=Bookman Old Style,Bookman Old Style][FONT=Bookman Old Style,Bookman Old Style]1. (1) Nchi yetu ni Tanzania na ni jamhuri ya shirikisho iliyoundwa kutokana na muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar na itaitwa Jamhuri ya Shirikisho ya Tanzania;
(2) Eneo la Jamhuri ya Shirikisho ya Tanzania ni eneo lote la Tanganyika na bahari yake pamoja na eneo lote la Zanzibar na bahari yake;
(3) Jamhuri ya Shirikisho ya Tanzania ni nchi moja yenye dola moja na vyombo mbalimbali vya utekelezaji wa mamlaka ya dola;
(4) Tanganyika itaitwa jimbo la Tanganyika na Zanzibar itaitwa jimbo la Zanzibar na kila jimbo litaongozwa na Gavana.
[/FONT]
[/FONT]
 
Basi sasa tatizo lipo hapo kwenye Jimbo la Tanganyika.Hapo ndio pananipa shida.

Mi naelewa kuwa hakutakuwa na nchi ya Tanganyika wala nchi ya zanzibar bali majimbo Ya tanganyika na zanzibar yatakayoongozwa na governors. Hii ina maana tutakuwa na rais mmoja tu, wa Federal Republic of Tanzania.
 
hii inaonyesha ni jinsi gani wananchi hawakujipanga kuwa na serikari 3 maana huku mtaani maswali hayaishi kwa kweli hapa wanasiasa wametubuluza
 
Naipongeza tume kwa kazi nzuri. Rasimu imeyatendea haki maoni ya wananchi wengi. Sasa mimi najiuliza hivi wale walioamua kuitengea kamati Shilingi milioni 18 eti za vyakula maalum kwa wajumbe wa tume watakao pata UKIMWI walifikiri hawa wajumbe serious kama Warioba, Baregu na wengineo ni wapenda ngono sana kama wao???!!! Kama wangekuwa wanaendekeza ngono wangeleta rasimu iliyotulia kama hii?? Kwanini watunga bajeti huwa mnakuwa na mawazo ya kingono ngono hivi. Kwanza mapendekezo yenu yalikuwa yakuwadhalilisha wajumbe. Mshindwe mlegee na mnyong'onyee kabisa katika katiba mpya
 
Haki za
Wanawake

46.-(1) Kila mwanamke ana haki ya:
(a) kuheshimiwa utu wake;
(b)kuwa salama dhidi ya unyonyaji na ukatili;
(c)kushiriki bila ya ubaguzi katika chaguzi na ngazi zote za
maamuzi;
(d)kupata ujira sawa na mwanaume katika kazi;
(e)kulindwa dhidi ya ubaguzi, uonevu na mila zenye madhara;
(f) kulindwa kwa ajira yake wakati wa ujauzito na pale
anapojifungua; na
(g)kupata huduma ya juu ya afya inayopatikana.
(2) Mamlaka husika za nchi zitaweka utaratibu wa kisheria
utakaosimamia masuala yanayohusu utekelezaji wa masharti ya Ibara hii
ikiwa ni pamoja na kukuza utu, usalama na fursa za wanawake wakiwemo
wajane.
Ibara hiyo hapo juu imewekwa kwa muktadha wa kutafuta usawa wa wanawake sawa, lakini haya maswala ya haki hubadilika kwa nyakati leo wanawake baada ya muda wanawake wakipata wanachokihitaji wanaume nao wataanza kudai haki hiyo, hivyo kwa kuwa katiba hii ni maisha ya watanzania tena miaka mingi inayokuja bora ibara hiyo ikasomeka kama ifuatavyo (Marekebisho ya pendekezo langu nimeandika kwa rangi nyekundu), na ninawaomba watakoingia kwenye mabaraza ya katiba kuliona hili

Haki za
Jinsia

46.-(1) Kila Jinsia ina haki ya:
(a) kuheshimiwa utu wake;
(b)kuwa salama dhidi ya unyonyaji na ukatili;
(c)kushiriki bila ya ubaguzi katika chaguzi na ngazi zote za
maamuzi;
(d)kupata ujira sawa na Jinsia nyingine katika kazi bila ya kuathiri Ibara ya 35-(1)(b);
(e)kulindwa dhidi ya ubaguzi, uonevu na mila zenye madhara;
(f) Kwa Jinsia ya Kike, kulindwa kwa ajira yake wakati wa ujauzito na pale
anapojifungua; na
(g)kupata huduma ya juu ya afya inayopatikana.
(2) Mamlaka husika za nchi zitaweka utaratibu wa kisheria
utakaosimamia masuala yanayohusu utekelezaji wa masharti ya Ibara hii
ikiwa ni pamoja na kukuza utu, usalama na fursa za Jinsia wakiwemo
wajane. Mjane ni Jinsia moja iliofiwa na mwenza
 
Tunashukuru Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa kuja na Rasimu ya Katiba Mpya iliyosheheni mapendekezo lukuki namna ya kuendesha nchi yetu siku za mbeleni.
Itapaswa katika mabaraza ya katiba kuangalia mambo yafuatayo kuhusiana na uwajibikaji wa mbunge kwa wapiga kura wake:-
1. Mbunge akiwa bungeni aweke maslahi ya jimbo mbele
2. Mbunge apimwe kwa ushiriki wake katika vikao vya baraza la halmashauri husika na bunge
3. Mbunge apigwe marufuku kuvamia jimbo lisilo lake na kuanza kupiga siasa
4. Mbunge awe mstari wa mbele kuhimiza makusanyo ya mapato ya halmashauri na serikali kwa ujumla

Nafikiri wa utaratibu huu wabunge kama Lema, Wenje, Mbilinyi, Joseph Nyerere na yule wa Ilemela watakuwa hawamalizi kipindi cha miaka 5 kutokana na utendaji wao usioleta tija kwa wapiga kura.
Nawasilisha
 
Kiukweli msajili wa vyama vya siasa hatumuhitaji kwa sasa. Tume huru ya uchaguzi itafanya kazi hiyo.
 
Ikumbukwe, tume ya Warioba ilikuwa na 50% wazanzibar ambao hawana mamlaka ya kujadili mambo ya Tanganyika.

Najua hilo kabisa, tena nalijua sana. Ninachosema ni kuwa, maoni ya katiba wanayo, na ndio maana kwenye hotuba yake mwenyewe, alitaja mambo ambayo alisema kuwa haya yatakuwa chini ya washirika wa muungano. Nina maana kuwa, hakuna haja tena ya kuzunguka Tanzania nzima ili kukusanya maoni ya katiba ya Tanganyika wakati maoni wanayo tayari ni kuya analyse.

Ningekuwa mimi raisi wa Tanzania, ningefanya uteuzi wa wajumbe wa katiba ya Tanganyika chap chap na kuwaambia wachukue maoni ya yaliyokusanywa na tume ya katiba ya muungano ili kwamba siku ya referendum iwe moja ili kupunguza gharama. Kwa namna hali ilivyo, hii rasimu itachakachuliwa lakini suala la serekali tatu halitazuilika
 
Back
Top Bottom