Rasmi Dar yakumbwa na uhaba wa Maji, RC Makalla athibitisha uwepo wa Mgao

Rasmi Dar yakumbwa na uhaba wa Maji, RC Makalla athibitisha uwepo wa Mgao

Ndio tatizo la kuwa na viongozi wasanii na sio wana sayansi kama Magufuli.
 
Hizi ni sera za CCM ndio maana hakuna maji ya kutosha, akili mbovu za CCM hawajawahi kuweka investment yeyote ya maana kwenye maji, wanatumia sytem iliyojengwa na mkoloni ambayo ilikuwa una hudumia watu laki moja na sasa jiji lina watu milioni zaidi ya nne, jiji limekuwa mara zaidi ya 40, wanajua mitambo ya Ruvu haina uwezo hata wa kuhudumia watu milioni 1, Rufiji kuna maji kuliko Ruvu na inaweza kuhudumia jiji lote bila matatizo lakini akili fupi za kimaskini za watawala wa CCM haziwezi kuona hilo, nchi tajiri ina kila kitu lakini tumeponzwa na vilaza wa CCM.
Hapo tumeambiwa tusubiri mvua inyeshe, ndo imeisha hiyo.

Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 
Binafsi naona kama serikali ya ccm wangejenga reservoir kwenye mto wami,wangeweza kufua umeme na kupata maji ya kutumia Dar.
Lile bonde lilipo daraja jipya maeneo hayo yana kina kirefu ambayo yangeweza kuhifadhi maji ya kutosha jiji la Dar es salaam
 
Kukosekana chanzo cha uhakika cha maji dar es salaam ni kujitakia, kilomita 180 kutoka katikati ya jiji mpaka kufika daraja la mto rufiji kuna maji yanatiririka mamilioni ya lita kuingia baharini, hata siku moja sijasikia mpango wa kuhamisha yale maji yaje dar
 
Wizara ya maji lazima sasa ibadilike, isiwe inategemea chanzo kimoja tu cha maji (mto ruvu) ambao chanzo chake ni mvua, mvua zikiwa chache uhaba wa maji unaongezeka.

Wizara Ichimbe visima virefu ili visima hivyo viwe vinaokoa jahazi wakati wa ukame kama huu.

DAWASA inakusanya mapato ya kutosha hivyo wataalamu wake lazima wakune vichwa kuangalia njia mbadala
 
Kwa akili Zangu za kawaida nilizojaaliwa kiwa nazo ninawaza haya yafeatayo;

(1) 99% of tap water in Dubai comes from desalination plants. Kimsingi dubai inapata 99% ya mahitaji yake ya maji, kutoka baharini.

Sisi bahari tunayo lakini tunaiangalia tu. Dar es salaam ni commercial hub ya nchi, ni mkoa muhimu sana, haiwezekani mpaka leo tumekosa wataalamu wakutusaidia kuondokana na adha hii.

(2) sea water, Dar es salaam ina ground water aquifer kubwa kule kimbiji, je hii haiwezi kuwa altenative source ya maji kwa mkoa wa Dar es salaam, kwa kipindi kama hiki chenye uhaba wa maji?

(3) Rain water harvesting: Kuna kipindi nilisikia kulikua na mpango wa serikali kujenga mabwawa makubwa ya kukusanya maji yatakayovunwa wakati wa mvua, ili maji hayo yatunzwe kwaajili ya matumizi ya kawaida nyakati za shida ya maji. Wazo hili ni zuri ila sijui liliishia wapi.

(4) Recycling of sewage water for domestic use. Haya maji ya vyooni yanayojazwa na malori ya maji taka, kwenye oxidation ponds kama zile za mikocheni mabwawani, alafu yanatiririshwa kwenda baharini, badala ya kutiririshwa kwenda baharini yangekuwa ya akuwa recycled, treated, then yanaingizwa kwenye mfumo wa usambazaji maji Dar es salaam ili yaweze kutumika majumbani, yangesaidia sana nyakati kama hizi za ukame. Hili linawezekana kabisa na linafanyika sehemu nyingi tu huko duniani.

Tanzania tuache blah blah, its time tuwe serious na mambo ya msingi katika maisha yetu, sio kuwa bize kubeti na kucheza singeli kwenye mikutano ya siasa.
 
Aweso ataenda tena kutafuta maji na gumboots asivyokuwa na akili. 2035 Dar itakuwa na watu milioni 12 maji si itabidi yauzwe sheli?
 
Kutegemea maji ya Ruvu kwa Dar ni hatari sana, Dar inahitahi chanzo cha maji cha uhakika , either watoe maji hata Mwanza, ikishindikana hata Kigoma lake Tanganyika au Ziwa nyasa, au wasafishe maki ya Bahari ya hindi

Ila yale pale Ruvu ni hatari ya kufa mtu na vipi mvua zisipo nyesha hadi mwakani hali itakuwaje kwa Dar huko?View attachment 2397755
Hatutaki maji yetu ya mikoani myachukue. Safisheni ya bahari mkishindwa kunyweni kiswahili au maghorofa yenu
 
Akizungumza baada ya kutembelea vyanzo vya Ruvu Chini na Juu, Mkuu wa Mkoa Amos Makalla amesema mgao wa Maji umesababishwa na kupungua kwa uzalishaji kunakotokana na ukame.

Makalla amesema hali ya Maji sio nzuri kwenye kina cha maji cha vyanzo hivyo huku uzalishaji ukipungua kutoka lita za ujazo milioni 466 kwa siku hadi kufika lita milioni 300 sawa na 64% ya uzalishaji wote wa maji.

Amesema "Naomba niwaambie wananchi kuwa mgao haupekuki kutokana na ukame ambao unatokana na kunyesha kwa mvua chache msimu uliopita na kuchelewa kunyesha kwa mvua katika msimu huu wa vuli."

======================

Wakati Serikali ikitangaza kuanza kwa mgawo wa maji jijini Dar es Salaam, sababu ya kutokea shida ya maji kila unapofika mwisho wa mwaka imeelezwa.

Akizungumza leo Jumanne Oktoba 25 baada ya kutembelea vyanzo vya vya kuzalisha maji vya Ruvu Chini na Ruvu Juu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema sababu ni kupunguza kwa uzalishaji wa maji unaotokana na ukame.

Makalla aliyewawakilisha pia wakuu wa mikoa ya Pwani na Morogoro amesema hali sio nzuri kwani kina cha maji cha vyanzo hivyo vyote kimepungua huku uzalishaji ukipungua kutoka lita za ujazo milioni 466 kwa siku hadi kufika lita milioni 300 sawa na asilimia 64 ya uzalishaji wote wa maji.

"Naomba niwaambie wananchi kuwa mgao haupekuki kutokana na ukame ambao tayari TMA ilishatangaza kuwepo kwa hali hii muda mrefu kulikosabbisha na kunyesha kwa mvua chache msimu wa mvua uliopita na kuchelewa kunyesha kwa mvua katika msimu huu wa vuli.

"Pia watu waelewe hali hii haisababishwi na Serikali wala sera za CCM bali ni mipango ya Mungu, hivyo asitokee mtu huko akaanza kupotosha huko, kikubwa tuendelee kumuomba Mungu atuletee mvua za vuli na vyanzo vyetu vya maji viweze kujaa,” alisema Makalla.

Aidha jitihada nyingine ambazo serikali imezifanya Makalla alisema kuanzi Mkoa wa Morogoro, Pwani na Dar es Salaam, kamati zote za ulinzi na usalama zimewadhibiti watu wote ambao walikuwa wakichepusha maji na sasa kisingizo cha kuwa ni wao wanaosababisha uhaba wa maji hakipo.

Pia kwa wakazi wa Dar es Salaam na Pwani amewaomba kutumia vizuri maji yanayopatikana ili yaweze kuwafaa kwa nyakati hii.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji wa Dawasa, Cyprian Luhemeia alisema watatoa ratiba za mgao huo siku sio nyingi.

Kwa mujibu wa Dawasa kupitia maofisa Mtendaji wake, Luhemeja, Maji yanayohitajika kwa jiji la Dar es Salaam kwa siku ni lita za ujazo milioni 500 hivyo kufanya kuwa na uhaba wa lita 200 kwa sasa.

Katika ziara hiyo, Makalla aliongozana na bodi ya Dawasa pamoja na Wakuu Wilaya ne Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Lubigija, Mkuu wa Wilaya Kigamboni, Fatma Almas, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Heri James na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe.

Alipotafutwa Naibu Waziri wa Maji Maryprisca Mahundi kuzungumzia mikakati ya Serikali kukabiliana na adha hiyo ambayo inaonekana kuanza kuwa sugu katika miezi ya mwisho wa mwaka alijibu kwa kifupi,

“Kama ulimsikiliza vizuri aliyetangaza hiyo, majibu yako wazi hiyo ni natural calamities (majanga ya asili), hata hivyo nipo kikaoni,” alisema na kukata simu.

MWANANCHI
Hakuna sera zozote za utunzaji wa mazingira huko Morogoro
 
Hivi hamna mechanism yoyote kisayansi kutumia maji ya bahari na kuyageuza kuwa maji salama kwa matumizi ya mwanadamu,?

Miaka nenda rudi wanasayansi wamekwama wapi?
Mkuu waarabu ndo maji wanayitumia hada dubai huwezi sikia kuna mgao wa maji ...njooo mwetu sisi kina mwajuma ndala ndefu mto rufiji tu unamwaga mwaji kibao baharini lakini huku sisi tunalia na mgao wa maji ...hushangai km mwanza wanalia mgao na maji yapo pua na mdomo ....
 
Nchi ya kipumbafu hawataki hii kitu

Seawater Desalination
 
Hapa nilipo hatuna maji kwa week 2 sasa. Imebidi tuagize watu wa tank walete kwa sh 15 elf
 
Nchi ya maziwa matatu inalalamikia ukame dunia ya leo? Hivi kama 'think tank' zimechoka huko kwenye system si mpishe damu changa aisee?
Yani kuna mambo yanakera kupita maelezo.
Maana ya kuwa na ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa ni nini sasa?
 
Kyela na kigoma wanalalamika maji hii nchi ya mazombi..
 
Hivi hamna mechanism yoyote kisayansi kutumia maji ya bahari na kuyageuza kuwa maji salama kwa matumizi ya mwanadamu,?

Miaka nenda rudi wanasayansi wamekwama wapi?

Inawezekana kwa kufanya desalination, ni technology inayotumia nishati kubsa (energy intensive)
Nchi za kiarabu kama Saudi Arabia, UAE, Oman na nyinginezo pia hata Israel wameweza kufanya kwa kutumia gas kuzalisha umeme kufua maji ya chumvi
Hapa gas ya Mtwara ingeweza kusadia
 
Hivi misri wanakuwaga na uhaba wa maji kwao?

Ova
 
Kwa hiyo kaishia hapo.
Hawajali kwa sababu wanajua Rais hawezi kufanya kitu.
Maisha yangu yote sitakuja kumsahau JPM .....kwa hakika Makala angeshatumbuliwa asubuhi tu..hayuko serious...
Hivi kwanini wafuasi wa Jiwe akili zao ni kama zako?
 
Enzi ya JPM kulikuwa hakuna shida ya maji Dar es salaam? Au ngekuwepo yeye angefanya maji yaongezeke mto Ruvu ili uzalishaji upande toka 64% hadi 100%?
Angekuja na propaganda au vyombo vy habari visingeruhusiwa ku report hiyo habari
 
Back
Top Bottom