Rasmi Dar yakumbwa na uhaba wa Maji, RC Makalla athibitisha uwepo wa Mgao

Rasmi Dar yakumbwa na uhaba wa Maji, RC Makalla athibitisha uwepo wa Mgao

Kulikuwa na mgao alafu anaidhinisha mgao zaidi
Inasikitisha sana, Tanganyika tuna mito,bahari, maziwa, chemchem,mabwawa,visima vya kuchimba mita chachee tu
Ila bado maji ni ya mgao hata kipindi Cha masika
Sijui inchi za jangwani wao wasemeje!!😂
 
Akizungumza baada ya kutembelea vyanzo vya Ruvu Chini na Juu, Mkuu wa Mkoa Amos Makalla amesema mgao wa Maji umesababishwa na kupungua kwa uzalishaji kunakotokana na ukame.

Makalla amesema hali ya Maji sio nzuri kwenye kina cha maji cha vyanzo hivyo huku uzalishaji ukipungua kutoka lita za ujazo milioni 466 kwa siku hadi kufika lita milioni 300 sawa na 64% ya uzalishaji wote wa maji.

Amesema "Naomba niwaambie wananchi kuwa mgao haupekuki kutokana na ukame ambao unatokana na kunyesha kwa mvua chache msimu uliopita na kuchelewa kunyesha kwa mvua katika msimu huu wa vuli."

======================

Wakati Serikali ikitangaza kuanza kwa mgawo wa maji jijini Dar es Salaam, sababu ya kutokea shida ya maji kila unapofika mwisho wa mwaka imeelezwa.

Akizungumza leo Jumanne Oktoba 25 baada ya kutembelea vyanzo vya vya kuzalisha maji vya Ruvu Chini na Ruvu Juu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema sababu ni kupunguza kwa uzalishaji wa maji unaotokana na ukame.

Makalla aliyewawakilisha pia wakuu wa mikoa ya Pwani na Morogoro amesema hali sio nzuri kwani kina cha maji cha vyanzo hivyo vyote kimepungua huku uzalishaji ukipungua kutoka lita za ujazo milioni 466 kwa siku hadi kufika lita milioni 300 sawa na asilimia 64 ya uzalishaji wote wa maji.

"Naomba niwaambie wananchi kuwa mgao haupekuki kutokana na ukame ambao tayari TMA ilishatangaza kuwepo kwa hali hii muda mrefu kulikosabbisha na kunyesha kwa mvua chache msimu wa mvua uliopita na kuchelewa kunyesha kwa mvua katika msimu huu wa vuli.

"Pia watu waelewe hali hii haisababishwi na Serikali wala sera za CCM bali ni mipango ya Mungu, hivyo asitokee mtu huko akaanza kupotosha huko, kikubwa tuendelee kumuomba Mungu atuletee mvua za vuli na vyanzo vyetu vya maji viweze kujaa,” alisema Makalla.

Aidha jitihada nyingine ambazo serikali imezifanya Makalla alisema kuanzi Mkoa wa Morogoro, Pwani na Dar es Salaam, kamati zote za ulinzi na usalama zimewadhibiti watu wote ambao walikuwa wakichepusha maji na sasa kisingizo cha kuwa ni wao wanaosababisha uhaba wa maji hakipo.

Pia kwa wakazi wa Dar es Salaam na Pwani amewaomba kutumia vizuri maji yanayopatikana ili yaweze kuwafaa kwa nyakati hii.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji wa Dawasa, Cyprian Luhemeia alisema watatoa ratiba za mgao huo siku sio nyingi.

Kwa mujibu wa Dawasa kupitia maofisa Mtendaji wake, Luhemeja, Maji yanayohitajika kwa jiji la Dar es Salaam kwa siku ni lita za ujazo milioni 500 hivyo kufanya kuwa na uhaba wa lita 200 kwa sasa.

Katika ziara hiyo, Makalla aliongozana na bodi ya Dawasa pamoja na Wakuu Wilaya ne Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Lubigija, Mkuu wa Wilaya Kigamboni, Fatma Almas, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Heri James na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe.

Alipotafutwa Naibu Waziri wa Maji Maryprisca Mahundi kuzungumzia mikakati ya Serikali kukabiliana na adha hiyo ambayo inaonekana kuanza kuwa sugu katika miezi ya mwisho wa mwaka alijibu kwa kifupi,

“Kama ulimsikiliza vizuri aliyetangaza hiyo, majibu yako wazi hiyo ni natural calamities (majanga ya asili), hata hivyo nipo kikaoni,” alisema na kukata simu.

MWANANCHI
Yaani kiongozi wa serikali leo hii mwaka 2022 anasimama mvele
Akizungumza baada ya kutembelea vyanzo vya Ruvu Chini na Juu, Mkuu wa Mkoa Amos Makalla amesema mgao wa Maji umesababishwa na kupungua kwa uzalishaji kunakotokana na ukame.

Makalla amesema hali ya Maji sio nzuri kwenye kina cha maji cha vyanzo hivyo huku uzalishaji ukipungua kutoka lita za ujazo milioni 466 kwa siku hadi kufika lita milioni 300 sawa na 64% ya uzalishaji wote wa maji.

Amesema "Naomba niwaambie wananchi kuwa mgao haupekuki kutokana na ukame ambao unatokana na kunyesha kwa mvua chache msimu uliopita na kuchelewa kunyesha kwa mvua katika msimu huu wa vuli."

======================

Wakati Serikali ikitangaza kuanza kwa mgawo wa maji jijini Dar es Salaam, sababu ya kutokea shida ya maji kila unapofika mwisho wa mwaka imeelezwa.

Akizungumza leo Jumanne Oktoba 25 baada ya kutembelea vyanzo vya vya kuzalisha maji vya Ruvu Chini na Ruvu Juu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema sababu ni kupunguza kwa uzalishaji wa maji unaotokana na ukame.

Makalla aliyewawakilisha pia wakuu wa mikoa ya Pwani na Morogoro amesema hali sio nzuri kwani kina cha maji cha vyanzo hivyo vyote kimepungua huku uzalishaji ukipungua kutoka lita za ujazo milioni 466 kwa siku hadi kufika lita milioni 300 sawa na asilimia 64 ya uzalishaji wote wa maji.

"Naomba niwaambie wananchi kuwa mgao haupekuki kutokana na ukame ambao tayari TMA ilishatangaza kuwepo kwa hali hii muda mrefu kulikosabbisha na kunyesha kwa mvua chache msimu wa mvua uliopita na kuchelewa kunyesha kwa mvua katika msimu huu wa vuli.

"Pia watu waelewe hali hii haisababishwi na Serikali wala sera za CCM bali ni mipango ya Mungu, hivyo asitokee mtu huko akaanza kupotosha huko, kikubwa tuendelee kumuomba Mungu atuletee mvua za vuli na vyanzo vyetu vya maji viweze kujaa,” alisema Makalla.

Aidha jitihada nyingine ambazo serikali imezifanya Makalla alisema kuanzi Mkoa wa Morogoro, Pwani na Dar es Salaam, kamati zote za ulinzi na usalama zimewadhibiti watu wote ambao walikuwa wakichepusha maji na sasa kisingizo cha kuwa ni wao wanaosababisha uhaba wa maji hakipo.

Pia kwa wakazi wa Dar es Salaam na Pwani amewaomba kutumia vizuri maji yanayopatikana ili yaweze kuwafaa kwa nyakati hii.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji wa Dawasa, Cyprian Luhemeia alisema watatoa ratiba za mgao huo siku sio nyingi.

Kwa mujibu wa Dawasa kupitia maofisa Mtendaji wake, Luhemeja, Maji yanayohitajika kwa jiji la Dar es Salaam kwa siku ni lita za ujazo milioni 500 hivyo kufanya kuwa na uhaba wa lita 200 kwa sasa.

Katika ziara hiyo, Makalla aliongozana na bodi ya Dawasa pamoja na Wakuu Wilaya ne Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Lubigija, Mkuu wa Wilaya Kigamboni, Fatma Almas, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Heri James na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe.

Alipotafutwa Naibu Waziri wa Maji Maryprisca Mahundi kuzungumzia mikakati ya Serikali kukabiliana na adha hiyo ambayo inaonekana kuanza kuwa sugu katika miezi ya mwisho wa mwaka alijibu kwa kifupi,

“Kama ulimsikiliza vizuri aliyetangaza hiyo, majibu yako wazi hiyo ni natural calamities (majanga ya asili), hata hivyo nipo kikaoni,” alisema na kukata simu.

MWANANCHI
Yaani kiongozi wa serikali leo hii mwaka 2022 anasimama mbele ya watu na kusema kuna mgao sababu hakuna mvua, ni jinsi taifa hili lilivyo na watu wasio na akili. Ni reflection ya wananchi wengi akiwemo rais wao... haya makali ya hizi huduma ni kwa nini kuna kipindi ilikua nafuu sana licha ya mvua kutokuwapo???
Nakumbuka misemo ya
1. KUNA WATU WANAFUNGULIA MABOMBA MABWAWA USIKU MAJI YATOKE...
2. Luna tetesi ilisemekana nchivina njaa mwamba akakataa na kusema acheni upuuzi nchi haina njaa, kweli maisha yakaendelea bila hilo ianga la njaa...
2. Nakumbuka watu walisema kuna ugonjwa wa ZIKA mwamba akasema acheni ujinga hamna hicho kitu, akawa sahihi...
Hivyo kwa haya yanayotokea ni UDHAIFU wa mamlaka ya juu... migao ya huduma nyeti ni udhaifu wake...
 
Enzi ya JPM kulikuwa hakuna shida ya maji Dar es salaam? Au ngekuwepo yeye angefanya maji yaongezeke mto Ruvu ili uzalishaji upande toka 64% hadi 100%?
Ukishikiwa akili ni tatizo... wewe umeshikiwa au ni mnufaika wa hii migao...
 
Akili za kiboya... uneaminishwa na umekubali... bahari zipo, maziwa yapo, badobumekoaa na kukinga maji ya mvua... hili taifa asilimia kubwa akili zimelaamiwa...
Boya ni baba yako..

Wapelekee maji na huku waache kufa 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20221026-154255.png
    Screenshot_20221026-154255.png
    121.4 KB · Views: 4
Ukraine mabomu yanapotea kupiga raia wasio na hatia,moja si lipotee njia lielekee DDM huku
 
Ni ushauri tu

Mitaa ya kariakoo hali ni tete Hewa nzito Sana

Kadhalika kukojoa kichakani faini ni tsh 50,000

Mungu wa mbinguni atulinde
Ni ushauri tu

Mitaa ya kariakoo hali ni tete Hewa nzito Sana

Kadhalika kukojoa kichakani faini ni tsh 50,000

Mungu wa mbinguni atulinde
Jo naona tungeshauri mto uliokaribu zaidi ungetengenezewa njia upitie city center ili tufanye Kama wenzetu wa vijijini,unachukua kindooo unaenda kujichotea mwenyewe mtoni🏃🏃
 
Jo naona tungeshauri mto uliokaribu zaidi ungetengenezewa njia upitie city center ili tufanye Kama wenzetu wa vijijini,unachukua kindooo unaenda kujichotea mwenyewe mtoni🏃🏃
Kwa viongozi wapi na nchi ipi yenye chama kipi??🤣🤣🤣🤣 Yule mnyiramba ndio awaze hiki au Yule September??
 
Vipi hiyo taabu inawapata wanachama wa chadema pekee yake au hata wana ccm nao wamekosa maji?
 
Back
Top Bottom