Rasmi: Simba wamtangaza Mreno Zoran Manojlovic kuwa kocha wao mkuu

Rasmi: Simba wamtangaza Mreno Zoran Manojlovic kuwa kocha wao mkuu

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1656426098979.png


Wameandika mwenye mafanikio yake amefika. Ingawa watu wengi wanahisi atatangazwa Manzoki lakini inadaiwa kuwa atatangazwa kocha raia wa Ureno.

Tusubiri hapa mbivu na mbichi
===

Confirmed

Zoran ni 𝗠𝗡𝗬𝗔𝗠𝗔 🦁

Kwa furaha kubwa tunapenda kumtangaza kocha wa makombe, Zoran Manojlovic (@zoran_manojlovic_maki) kuwa Kocha Mkuu wa timu yetu. Kujua zaidi kuhusu mafanikio yake kwenye soka la Afrika.

1656440681269.png


MFAHAMU KOCHA MPYA SIMBA SC
Kabla ya kutua Simba Zoran Maki (60) alikuwa anaifundisha Al Tai FC ya Saudi Arabia 🇸🇦 ambayo alijiunga nayo aikitokea CR Belouizdad ya Algeria 🇩🇿 na kuiwezesha kufika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Zoran pia amewahi kuinoa Wydad Athletic Club ambayo ni miamba ya soka nchini Morocco 🇲🇦 Mwaka 2018 aliifikisha Primeiro De Agosto ya Angola 🇦🇴 Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo.

Kocha Zoran si mgeni kwa Tanzania 🇹🇿 amewahi kuja na Timu ya Al Hilal ya Sudan 🇸🇩 na kushiriki mashindano ya Super Cup yaliyoandaliwa na Simba mwaka jana.
 
View attachment 2275574

Wameandika mwenye mafanikio yake amefika. Ingawa watu wengi wanahizi atatangazwa Manzoki lakini inadaiwa kuwa atatangazwa kocha raia wa Ureno.

Tusubiri hapa mbivu na mbichi
Binafsi makocha wazawa waache uswahili leo nchi kama Burund na Rwanda kwel wa kutupatia makocha ??? sitaki kabisa kuamini Makocha wazawa wajitafakari na sijui shida ipo wap shule au nini hasa ??
 
Nani anasajili wachezaji?

Kama mchezo utakuwa ni huo huo, unganisha wachezaji uliowakuta/waliosajiliwa, hakuna maajabu ya kutegemewa kwa kocha awaye yeyote.

Wenzao kwasasa wanatembelea UTAWALA WA NCHI, mpira hakuna ila fedha ya kununua matokeo na ubavu wa kulazimisha mambo yawe watakavyo. Ngoja tuone kama hii mbinu itatusaidia na huko mataifani.
 
Nani anasajili wachezaji?

Kama mchezo utakuwa ni huo huo, unganisha wachezaji uliowakuta/waliosajiliwa, hakuna maajabu ya kutegemewa kwa kocha awaye yeyote....
Hawa waliochukua ubingwa msimu huu hapo Yanga, Nabi aliwakuta? Unajua kuna vitu vingine maongea tu kama mmekatwa vichwa[emoji23].

Mazingira ya yetu Africa ni magumu sana kufanyika huo utaratibu mnaoutaka, kocha atoke BELGIUM, SPAIN AU taifa lingine la nje kisha aje kupendekeza wachezaji wa africa ambao watafit mfumo wake ilhali hawajui hao wachezaji? Au unahisi hata huko ulaya wanafatilia soka letu la kijinga??

Let's Simba Sc ingeajiri kwanza kocha ili aje afanya mapendekeze yeye .wenyewe, angewezaje kuwapata ndani ya muda mfupi na ikiwa ligi nyingi za Africa zimeisha (angefanyaje acessment ya hao wachezaji)? ACHENI UJUAJI.

Kwa mpira wa Africa, kikubwa ni kuwepo kwa team nzuri ya scouting basi, kocha atawakuta wachezaji na atawaacha.
 
Back
Top Bottom