RC Chalamila: Tunaweza kuwa na ‘Magufuli Ruling Party’ na mambo yakaenda vizuri kabisa

RC Chalamila: Tunaweza kuwa na ‘Magufuli Ruling Party’ na mambo yakaenda vizuri kabisa

Kama kuna mtanganyika/mtanzania anaona hizi kauli ni bahati mbaya akapimwe akili. Ukweli ni kua Vibaraka wa Shetani a.k.a Mapoyoyo yameandaliwa waseme wanayosema na kutenda wanayotenda. Shetani MKUU anawatuma hao. KATIBA itabadirishwa kibabe na propaganda itakua, "wananchi/wazalendo wamenisukumia humo milele, nimesikia kilio chenu sitawaangusha, fanyeni kazi" .
 
Huwa najiuliza hiki cheo alipataje huyu kijana? Yaani dah akili yangu huwa inatatizika sana!
Alikipata kupitia CCM, ndo alikuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa. Alivyoteuliwa ukuu wa mkoa akaambiwa achague cheo kimoja, akachagua ukuu wa mkoa.
 
Hivi ni dada yake rayc mana wamefanana sana mpka majina
Mwalimu wa kiswahili huyo, bingwa wa kuchomekea maneno. wanambeya wanamkubali sana huyo mwamba wa lugha, hapo kawaacha CHADEMA , ACT, na wengine kuitafakari kauli hiyo bila majibu
 
Upambe umezidi hadi nuksi.Mwanaume unamsifia vipi mwanaume mwenzio eti nae ni msomi INA Maana ajui faida za vyama vingi. Haya mambo wayafanyayo ni sababu ya pressures ya upinzani.
 
Hao walioteuliwa kwa ajili ya kupambana na chadema wana tabu kweli kweli awajui hata job description ndo madhara ya kuondoa seminar elekezi. Wanachojua ni kupambana na upinzani tu.
 
Alikipata kupitia CCM, ndo alikuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa. Alivyoteuliwa ukuu wa mkoa akaambiwa achague cheo kimoja, akachagua ukuu wa mkoa.

Alishindwa kumng'oa msigwa IRINGA je ataweza kumng'oa sugu Mbeya?Ni kati ya ma rc watakaopigwa chini kwa kushindwa kuwapa ushindi.
 
Alishindwa kumng'oa msigwa IRINGA je ataweza kumng'oa sugu Mbeya?Ni kati ya ma rc watakaopigwa chini kwa kushindwa kuwapa ushindi.
Huyu RC hakuletwa kwa ajili ya kumng'oa Sugu, aliyeletwa kwa ajili hiyo ni Vurugu Jackson. Huyu Chalamila hajui fitna na figisu za siasa ndo maana hotuba zake zina ukakasi wa tamaa za mwili tu.
 
Mwalimu wa kiswahili huyo, bingwa wa kuchomekea maneno. wanambeya wanamkubali sana huyo mwamba wa lugha, hapo kawaacha CHADEMA , ACT, na wengine kuitafakari kauli hiyo bila majibu
Hivi Magufuli Ruling Party ni Kiswahili? Sasa mwalimu wa Kiswahili anapendekeza chama kipya kwa jina la lugha nyingine. Halafu ndio mnasema Kiswahili kitumike kufundishia kwenye ngazi zote za elimu wakati walimu wenyewe wa Kiswahili hawakitaki Kiswahili badala yake wanapendekeza majina ya Kiingereza. Chema chajiuza Kibaya chajitembeza. Naona Kiingereza kinajiuza chenyewe hata kwa walimu wa Kiswahili
 
mnasema maendeleo hayana chama,na mimi nasema kujikomba hakuna chama
 
Nimeisikia hii kupitia ITV huko mkoani Mbeya wilayani Kyela.

Ngoja niitafakari kidogo hii kauli ya RC Chalamila....... Nijiridhishe alichomaanisha.

Maendeleo hayana vyama!

ALICHOJIBU RAIS:

Rais Magufuli amesema mkuu wa mkoa Albert Chalamila anatamani tuwe na mfumo wa chama kimoja lakini yeye (Dr Magufuli) matamanio yake ni kuwa na mfumo wa vyama vingi lakini CCM iendelee kupata ushindi.

Rais Magufuli Magufuli anasema katika hilo anatofautiana na Mkuu wa Mkoa na kwa maana hiyo kila mmoja wao abakie na msimamo wake.

Hongera Rais Magufuli kwa kulitolea ufafanuzi wa haraka sana swala hili!

====================

Habari zaidi kutoka kwa Mdau mwingine

Katika ziara ya Raisi inayofanyika leo hapa Kyela, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amesikika akisema "Natamani kuwe na Chama kimoja Magufuli Ruling Party".

Akifafanua kauli hiyo Mkuu wa mkoa amesema "Kila mwezi unatusaidia kuwalipa watumishi 2471 wanao lipwa zaidi ya bil.1, pesa ambazo wewe mh. raisi Magufuli unazileta katika mji wa Kyela.

Ninacho shangaa unapokuta tunaendeleza malumbano katika mazuri hayo unayoyafanya, ambayo hatuna mahali popote pakuyalinganisha. Sioni sababu ya kua na mfumo wa vyama vingi Kyela zaidi ya kua na chama kimoja kinachoitwa "Magufuli Ruling party katika mazuri"

Akijibu hoja hiyo mh: raisi amesema "Mkuu wa mkoa anatamani kuwa na chama kimoja, lakini mimi natamani kuwe na vyama vingi sana vitakavyoleta ushindani lakini siku zote Ccm ndio iwe inashinda kwasababu ni kwa mujibu wa katiba yetu".
Vyama vya upinzani vipo kikatiba na ni muhimu kuvilinda ili viendelee kuwepo, ila CCM ndiyo inatakiwa iendelee kutawala daima.
 
Ndio tatizo la kulewa sifa hadi kuvimbewa, unabaki kutoa harufu mbaya pande zote zenye matundu hewa chafu inatoka tuu
 
Mwalimu wa kiswahili huyo, bingwa wa kuchomekea maneno. wanambeya wanamkubali sana huyo mwamba wa lugha, hapo kawaacha CHADEMA , ACT, na wengine kuitafakari kauli hiyo bila majibu
Na wewe kwa kusifia vitu vya hovyo hovyo umejaliwa
 
Nimeisikia hii kupitia ITV huko mkoani Mbeya wilayani Kyela.

Ngoja niitafakari kidogo hii kauli ya RC Chalamila....... Nijiridhishe alichomaanisha.

Maendeleo hayana vyama!

ALICHOJIBU RAIS:

Rais Magufuli amesema mkuu wa mkoa Albert Chalamila anatamani tuwe na mfumo wa chama kimoja lakini yeye (Dr Magufuli) matamanio yake ni kuwa na mfumo wa vyama vingi lakini CCM iendelee kupata ushindi.

Rais Magufuli Magufuli anasema katika hilo anatofautiana na Mkuu wa Mkoa na kwa maana hiyo kila mmoja wao abakie na msimamo wake.

Hongera Rais Magufuli kwa kulitolea ufafanuzi wa haraka sana swala hili!

====================

Habari zaidi kutoka kwa Mdau mwingine

Katika ziara ya Raisi inayofanyika leo hapa Kyela, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amesikika akisema "Natamani kuwe na Chama kimoja Magufuli Ruling Party".

Akifafanua kauli hiyo Mkuu wa mkoa amesema "Kila mwezi unatusaidia kuwalipa watumishi 2471 wanao lipwa zaidi ya bil.1, pesa ambazo wewe mh. raisi Magufuli unazileta katika mji wa Kyela.

Ninacho shangaa unapokuta tunaendeleza malumbano katika mazuri hayo unayoyafanya, ambayo hatuna mahali popote pakuyalinganisha. Sioni sababu ya kua na mfumo wa vyama vingi Kyela zaidi ya kua na chama kimoja kinachoitwa "Magufuli Ruling party katika mazuri"

Akijibu hoja hiyo mh: raisi amesema "Mkuu wa mkoa anatamani kuwa na chama kimoja, lakini mimi natamani kuwe na vyama vingi sana vitakavyoleta ushindani lakini siku zote Ccm ndio iwe inashinda kwasababu ni kwa mujibu wa katiba yetu".
Pipa na mfuniko!!!
Kutarajia maendeleo endelevu katika fikra za aina hii itakuwa sawa na ndoto ya mchana...
Tunapaswa kujifunza
 
Ubaguzi umeenea sana kwenye jamii yetu.
FB_IMG_1556633975670.jpeg
 
Back
Top Bottom